Rais Samia: Tunazaliana wengi mno, mahitaji makubwa mno ndio maana kila tukiajiri Watumishi hawatoshi

Tanzania hata tuzaliane Kila family iwe na watoto15 hatuwezi banana kamwe! Walishindwa wazee wenu kutujaza walikuwa na nguvu nk


Shida kubwa hatuna viongozi wenye maono. Viongozi tulio nao maono Yao ni ufisadi tu.

Hawa wazi kesho ya vitukuu vyao. Iwapo tu tukajariwa akiri tukawa na viongozi dhabiti Kwa Mali tulizo nazo hata kulipwa tunaweza kuwa tunalipwa

Kwa uchache tu

Tuna madini ya Kila aina
Maziwa yenye samaki tele
Mbuga za wanyama
Ges
Makaa ya mawe/chuma
Tuna mashamba yenye rutuba yanayoweza kulimwa Kwa kipindi chote bila kutegemea mvua!
Nk nk

Lakini akiri ndo hatuna kabisa.

Huwa nilisafiri Hadi nawaza ni lini Tz tutabanana.

Mfano Kuna route Moja ukitoka babati unaenda Arusha huoni nyumba ni mashamba na miti hata ukiona nyumba za mbalimbali sana

Tz tuna maeneo makubwa sana huenda eneo lisilo kaliwa na watu na lisilo limwa ndo kubwa hata 57%
 
mkoa wa simiyu dogo wa miaka 29 ana watoto 5 hata nyumba hana ukimuuliza sababu za kuzaliana kwa pupa hana sababu za maana

wanaona kuzaliana sana kunakuza brand
Wewe jamaa umetumia data gani kuchagua Simiyu au umbumbumbu na kukariri unakusumbua

Nikusaidie tuu Top 10 ya mikoa inayoongoza kwa kuzaliana na rate ya ongezeko la kwa mwaka,takwimu za sensa ya 2022 na Simiyu haipo hapo,

1. Katavi-7.1
2. Pwani-6.1
3. Geita-5.4
4. Rukwa-4.3
5. Tabora-3.9
6. Dodoma-3.9
7. Shinyanga-3.8
8. Singida-3.8
9. Morogoro-3.7
10. Arusha-3.3
 
Sasa mbona mama anataka vijana tuoe alafu hataki tena tuzaliane.

Ila hata kama tukiwa wengi, kama tukiwa na afya njema tatizo litakuwa wapi kwa kada ya afya?

Labda tupambane na vyanzo vya magonjwa zaidi ili kupunguza idadi ya watu watakaougua
 
Ndio maana yeye Rais na Serikali wapo kuhakikisha mambo yanaenda na kila kitu kinakuwa under control.

Maana ya kuwa kiongozi ni kufanya kazi na kuumiza kichwa na Kesho ya Taifa sio kulalama kama wananchi wanavyolalama
 
Ukiona hivo jua tunaongozwa na watu wasio na maarifa. Hzo census mnafanyaga za kaz gani..?
 
Unataka kutuambia nchi hii imevumbuliwa na Columbus muongo mmoja uliopita?
Columbus hajaivumbua hii nchi, wakati wakoloni wanafika Africa hakukuwa hata na nchi ya Tanganyika, kulikuwa na ardhi za makabila tu.
 
Kuiba waibe wao alafu lawama walete kwetu 🤔 ajira hazitoshelezi mahitaji kwa sababu wizi ni mkubwa kuliko matumizi, sisi tutaendelea kufyatua tuu wataishi vipi tutajua wenyewe
 
Tajiri na pesa zake masikini na watoto wake, serikali iache kutafuta visingizio waboreshe huduma za msingi huo ni wajibu wao na sio hisani.
 
Bila kusahau Rukwa na katavi
 
upungufu wa watumishi ila tuna msafara wa raisi una magari zaidi ya 150 unatarajia serikali isipopunguza matumizi ya kifahari hao watumishi wanaajiriwaje pesa za mikopo zinanunulia magari 🤣🤣🤣🤣 tutafika tunatambaa
 
Mbona hatuwaelewi?!
Aliyekuwa bosi wake alisisitiza kuzaliane kwa wingi kwakuwa sisi ni matajiri..
Tena akisema fyatua...
Yeye leo analalamika! Msimamo wa nxhi ni upi?
N.B tuwe na dira ya nchi.
Kwani nani kakakutaza kuzaliana?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…