Rais Samia: Uchumi wetu unakua lakini tunachokusanya kingi kinaingia mifukoni kwa Watu

Rais Samia: Uchumi wetu unakua lakini tunachokusanya kingi kinaingia mifukoni kwa Watu

Kwanza aibu sana mtu kma rais ana lalamika eti haoni kodi ni kitu cha hovyo sana na ajabu kweli
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan akizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi Dar es Salaam, leo tarehe 04 Oktoba, 2024.
RAIS SAMIA: UCHUMI WETU UNAKUA LAKINI HAUAKISI TUNACHOKIPATA
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi lakini hauakisi mapato ambayo Wananchi wanayapata, amesema hayo wakati akizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi Dar es Salaam, leo Oktoba 4, 2024.

RAIS SAMIA: UCHUMI WETU UNAKUA LAKINI HAUAKISI TUNACHOKIPATA
Akizungumza wakati akizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi Dar es Salaam, leo Oktoba 4, 2024, Rais Samia Suluhu Hassan amesema mchakato wa ulipaji kodi unatakiwa kuwa rafiki ili kumwezesha mlipa kodi kukamilisha zoezi hilo ikiwemo mifumo inayotumika.

Amesema kuna umuhimu wa kutoa elimu zaidi kwa walipa kodi ili wajue wanamlipa nani na kiwango gani, akitoa mfano amesema alikutana na changamoto Mkoani Ruvuma ambapo alisema kuna Mama Lishe waliokuwa wakilalamika kuhusu kulipishwa kodi na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).


=========================

RAIS SAMIA: HATUA MPYA KATIKA MABORESHO YA MFUMO WA KIKODI TANZANIA

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa kiongozi wa kwanza tangu Rais Benjamin Mkapa kuboresha mfumo wa kikodi nchini Tanzania, baada ya kuunda Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi. Tume hii ina lengo la kuangazia changamoto mbalimbali zinazokabili mfumo wa kodi na kutoa mapendekezo yanayoweza kuboresha ukusanyaji wa kodi na ufanisi wa matumizi yake.

Moja ya mambo makuu ambayo Rais Samia anatarajia kuyatekeleza kupitia tume hii ni kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa kodi. Hii ni muhimu katika kujenga imani ya wananchi kwa serikali na mfumo wa kodi, ambao mara nyingi umekuwa ukikabiliwa na malalamiko kuhusu ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Pia, tume hiyo inatarajiwa kuzingatia njia mpya za kukusanya kodi ambazo zitasaidia kuongeza mapato ya serikali bila kuweka mzigo mzito kwa wananchi. Hii inaweza kujumuisha matumizi ya teknolojia ya kisasa katika ukusanyaji wa kodi, kama vile mifumo ya kielektroniki inayorahisisha malipo ya kodi na kuondoa urasimu usio wa lazima.

Aidha, Rais Samia amesisitiza katika ushirikiano na sekta binafsi ili kuboresha mfumo wa kikodi. Ushirikiano huu unaweza kuleta mawazo mapya na mbinu za kisasa katika ukusanyaji wa kodi na pia kutoa fursa kwa sekta binafsi kushiriki katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

Kwa kufanya hivi, Rais Samia atasaidia kukuza mazingira ya biashara yanayovutia wawekezaji na kuimarisha uchumi wa nchi. Hii ni muhimu katika kipindi ambacho uchumi wa dunia unakabiliwa na changamoto, na Tanzania inahitaji kuongeza mapato yake ya ndani ili kufikia malengo yake ya maendeleo.

Hapa Mh ZK ni kama ameshikwa na hasira ya kile anachosikiliza na anatamani anyanyuke aondoke ila Tumbo nalo linamtaka andelee kubakia Royal hata kama hakubaliani na hizo " Hadithi za Bibi"
 
Nguvu anayotumia kuteka na kuua watu aihamishie kwenye kukusanya na kusimamia mapato ya serikali.
 
NDUGU ............ MENEJA WA TRA MKOA WA KODI KINONDONI ANAKUHIMIZA KULIPA KIASI CHA SH. 93,418,445.29 AMBAYO NI MALIPO YA VAT YA MWEZI AGOSTI 2024. LIPA KODI HII KABLA YA TAREHE YA LEO 30/09/2024. RIBA NA ADHABU ZITAJUMUISHWA KWA KUSHINDWA KULIPA KWA WAKATI.
"PAMOJA TUNAJENGA TAIFA LETU"

Waaaambie silipi hata kwa fimbo, waniue! Hii ni Kodi au ni laana?
Huyu bibi haishi kulalamika kama vile hajui jukumu lake la kuwa Rais!
Hata muunde tume ngapi na kuleta mapendekezo lukuki ya kuongeza makusanyo, hamuwezi kufanikiwa kwasababu , viongozi wa serikali ndio wao wanawalinda wafanya biashara wakubwa kwani wanakula nao!! Mkazo wao mkubwa ni kuwakamua watu wa chini kwa kuongeza tozo za kila aina.
Huyu bibi hajui shida za nchi kwani anatilia mkazo mapato tu badala ya kuangalia jinsi serikali yake inavyotumia kodi za wananchi ; Huyu bibi anawagawia chawa wake shs. 40,000,000 kila mmoja kutokana na kodi za wananchi ili wamsaidie propaganda za kumuwezesha kupata urais!
If she was serious the so called commission would not only be tasked with looking at the revenue side but also the expenditure side in order to balance the equation.
 
Back
Top Bottom