Rais Samia, unadhani vyombo vyako vinaaminika mbele ya wananchi kwenye kuchunguza sakata hili la mauaji na utekaji nchini?

Rais Samia, unadhani vyombo vyako vinaaminika mbele ya wananchi kwenye kuchunguza sakata hili la mauaji na utekaji nchini?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Mheshimwa Rais.
Umesikika ukiagiza vyombo vyako kufanya uchunguzi wa masuala ya utekaji hata hivyo nasikitika kukwambia kuwa

1. Vyombo vyako haviaminiki tena
Tangu jeshi la polisi na mamlaka mbalimbali za uchunguzi kukataa/kushindwa kuchunguza tukio la Lissu kupigwa risasi, kupotea kwa Ben Saa nane na kupotea kwa Azory Gwanda, wananchi hawana imani na jeshi la polisi kuchunguza matukio utekaji yenye sura za kisiasa

2. Ubambikizwaji wa kesi ya uhaini kwa Akina Dr Slaa
Mheshimiwa rais juzi umesema umepewa taarifa za uwepo wa kikao huko Arusha chenye kula njama za kukuondoa madarakani kinguvu. Hata hivyo ni vyombo hivyohivyo kupitia jeshi la polisi viliatangaza uwepo wa jaribio la uhaini nchini lililopelekea akina Mwabukusi, Mdude Nyagali na Dr Slaa wakiwekwa ndani. Hata hivyo wakaja kuachiwa bila kesi kuunguruma mpaka mwisho. Hapa inaonyesha vyombo vyako vilichemsha

3. Wewe Rais serikali yako ilipeleka muswada bungeni wa kubadili sheria na kuifanya usalama wa Taifa iwe inakamata watu.
Mheshimwa Rais, kwa sheria hii uliyopeleka muswada wake bungeni na kisha kuisaini wewe mwenyewe wa kuwapa rungu watu hawa wa usalama wa Taifa kukamata watu, huku tukijua kuwa hawa hawana vituo vya kawaida vya kuhifadhi watuhumiwa, amabpo raia wanaweza kuwafuata, kuwajulia hali, wakawekwa kwenye reja za kawaida maana yake ni kuwa watu wa usalama wa Taifa wanafanya kazi gizani zaidi. Ni vigumu pia wananchi kuamini kuwa Idara hii pia katika masuala haya ya utekaji nchini.

4. Wapo wahanga wa utekaji na jeshi la polisi halijawahoji
Mtu kama SATIVA analalamika kutekwa, anatuma taarifa za watesi wake, alipigwa risasi akatupwa porini. Lakini jeshi la polisi halijaona umuhimu wa kumhoji ili kuchunguza tukio lake.

5. Wewe Mwenyewe umewahi kulituhumu jeshi la polisi kwa mauji
Uliagiza Waziri mkuu wakati fulani kuunda tume ya kulichunguza jeshi la polisi kwa mauji, ukasema jeshi la polisi lenyewe ni mtuhumiwa. Sasa kama wewe umewahi kudhani kuwa Si busara kwa jeshi la polisi kujichunguza kwa sababu ni mtuhumiwa, Je unadhani wananchi watakuwa na maoni tofauti katika matukio ya hivi karibuni ya mauaji ya mzee Ally Kibao na utekwaji wa watu mbalimbali hasa wananchama wa CHADEMA?

6. Juzi umesema ulisikia clip, Dr Slaa akizungumza tuhuma za utekaji hata hivyo vyombo vyako mpaka sasa vimezubaa havijamuita kumhoji kwa jambo hilo mpaka sasa
Mheshimiwa Rais, imagine wewe umepata clip ya Dr slaa akitoa kauli hiyo, tena miaka kadhaa iliyopita,lakini cha ajabu vyombo vyako eti havijaifanyia kazi clip hiyo kwa miaka yote hiyo. Sasa mheshimiwa rais kama vyombo vyako ni incompetent kiasi hiki, je unadhani raia wataamini kuwa vinao uwezo wa kuchunguza matukio kama hayo ambayo vimeshindwa kuchunguza kwa miaka kadhaa sasa?

SASA Mheshimiwa Rais:
Kama hilo jeshi lako la Polisi limeshindwa kufanya uchunguzi juu ya matukio lukuki ya utekwaji na mauaji nchini hasa yenye mrengo wa kisiasa unadhani wananchi watakuwa na imani na hilo unaloita "agizo" hivyo vyombo vichunguze?.
Mheshimiwa Rais nchi hii imewahi kuwaleta wachunguzi kutoka nje juu ya mauaji ya Padri huko Zanzibar, na sasa Wananchi wanataka wachunguzi huru waje wachunguze matendo ya kidhalimu kabisa ya mauaji ya watu wasi na hatia nchini.

BY THE WAY, TANGU LINI MTUHUMIWA AKAJICHUNGUZA MWENYEWE?
 
Sio hayajui hayo ila hajali kuhusu ninyi wananchi mnasema nini as long as ana nguvu kubwa, hakuna sisimizi anaeweza kumchallenge hapo alipo.
 
Inasikitisha ikiwa mmoja wa wanao fanya uchunguzi wa mauaji ni Ofisa ambaye ametajwa na Sativa kuwa ndiye aliyetoa Amri auwawe.
Hii tamthilia ya hovyo na kikatili sana.
 
Mheshimwa Rais.
Umesikika ukiagiza vyombo vyako kufanya uchunguzi wa masuala ya utekaji hata hivyo nasikitika kukwambia kuwa

1. Vyombo vyako haviaminiki tena
Tangu jeshi la polisi na mamlaka mbalimbali za uchunguzi kukataa/kushindwa kuchunguza tukio la Lissu kupigwa risasi, kupotea kwa Ben Saa nane na kupotea kwa Azory Gwanda, wananchi hawana imani na jeshi la polisi kuchunguza matukio utekaji yenye sura za kisiasa

2. Ubambikizwaji wa kesi ya uhaini kwa Akina Dr Slaa
Mheshimiwa rais juzi umesema umepewa taarifa za uwepo wa kikao huko Arusha chenye kula njama za kukuondoa madarakani kinguvu. Hata hivyo ni vyombo hivyohivyo kupitia jeshi la polisi viliatangaza uwepo wa jaribio la uhaini nchini lililopelekea akina Mwabukusi, Mdude Nyagali na Dr Slaa wakiwekwa ndani. Hata hivyo wakaja kuachiwa bila kesi kuunguruma mpaka mwisho. Hapa inaonyesha vyombo vyako vilichemsha

3. Wewe Rais serikali yako ilipeleka muswada bungeni wa kubadili sheria na kuifanya usalama wa Taifa iwe inakamata watu.
Mheshimwa Rais, kwa sheria hii uliyopeleka muswada wake bungeni na kisha kuisaini wewe mwenyewe wa kuwapa rungu watu hawa wa usalama wa Taifa kukamata watu, huku tukijua kuwa hawa hawana vituo vya kawaida vya kuhifadhi watuhumiwa, amabpo raia wanaweza kuwafuata, kuwajulia hali, wakawekwa kwenye reja za kawaida maana yake ni kuwa watu wa usalama wa Taifa wanafanya kazi gizani zaidi. Ni vigumu pia wananchi kuamini kuwa Idara hii pia katika masuala haya ya utekaji nchini.

4. Wapo wahanga wa utekaji na jeshi la polisi halijawahoji
Mtu kama SATIVA analalamika kutekwa, anatuma taarifa za watesi wake, alipigwa risasi akatupwa porini. Lakini jeshi la polisi halijaona umuhimu wa kumhoji ili kuchunguza tukio lake.

5. Wewe Mwenyewe umewahi kulituhumu jeshi la polisi kwa mauji
Uliagiza Waziri mkuu wakati fulani kuunda tume ya kulichunguza jeshi la polisi kwa mauji, ukasema jeshi la polisi lenyewe ni mtuhumiwa. Sasa kama wewe umewahi kudhani kuwa Si busara kwa jeshi la polisi kujichunguza kwa sababu ni mtuhumiwa, Je unadhani wananchi watakuwa na maoni tofauti katika matukio ya hivi karibuni ya mauaji ya mzee Ally Kibao na utekwaji wa watu mbalimbali hasa wananchama wa CHADEMA?

6. Juzi umesema ulisikia clip, Dr Slaa akizungumza tuhuma za utekaji hata hivyo vyombo vyako mpaka sasa vimezubaa havijamuita kumhoji kwa jambo hilo mpaka sasa
Mheshimiwa Rais, imagine wewe umepata clip ya Dr slaa akitoa kauli hiyo, tena miaka kadhaa iliyopita,lakini cha ajabu vyombo vyako eti havijaifanyia kazi clip hiyo kwa miaka yote hiyo. Sasa mheshimiwa rais kama vyombo vyako ni incompetent kiasi hiki, je unadhani raia wataamini kuwa vinao uwezo wa kuchunguza matukio kama hayo ambayo vimeshindwa kuchunguza kwa miaka kadhaa sasa?

SASA Mheshimiwa Rais:
Kama hilo jeshi lako la Polisi limeshindwa kufanya uchunguzi juu ya matukio lukuki ya utekwaji na mauaji nchini hasa yenye mrengo wa kisiasa unadhani wananchi watakuwa na imani na hilo unaloita "agizo" hivyo vyombo vichunguze?.
Mheshimiwa Rais nchi hii imewahi kuwaleta wachunguzi kutoka nje juu ya mauaji ya Padri huko Zanzibar, na sasa Wananchi wanataka wachunguzi huru waje wachunguze matendo ya kidhalimu kabisa ya mauaji ya watu wasi na hatia nchini.

BY THE WAY, TANGU LINI MTUHUMIWA AKAJICHUNGUZA MWENYEWE?
Amini Mungu gentleman na huko kwa nyumba za ibada..

Vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya kazi na majukumu yake kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi, na sio kwa imani au matimani ya mtu fulani...

polisi hawahubiri habari za dini, imani au kiroho. Zinalinda usalama wa watu,kazi na makazi yao upende usipende 🐒

hayo mengine ni porojo na stori za kawaida za kupoteza muda tu..
 
Yeye mwenyewe haaminiki, sembuse ya vyombo vyake vya usalama.
 
Saliva alipelekwa osterbay polisi.
Watakwambia hawana pa kuanzia
 
Mheshimwa Rais.
Umesikika ukiagiza vyombo vyako kufanya uchunguzi wa masuala ya utekaji hata hivyo nasikitika kukwambia kuwa

1. Vyombo vyako haviaminiki tena
Tangu jeshi la polisi na mamlaka mbalimbali za uchunguzi kukataa/kushindwa kuchunguza tukio la Lissu kupigwa risasi, kupotea kwa Ben Saa nane na kupotea kwa Azory Gwanda, wananchi hawana imani na jeshi la polisi kuchunguza matukio utekaji yenye sura za kisiasa

2. Ubambikizwaji wa kesi ya uhaini kwa Akina Dr Slaa
Mheshimiwa rais juzi umesema umepewa taarifa za uwepo wa kikao huko Arusha chenye kula njama za kukuondoa madarakani kinguvu. Hata hivyo ni vyombo hivyohivyo kupitia jeshi la polisi viliatangaza uwepo wa jaribio la uhaini nchini lililopelekea akina Mwabukusi, Mdude Nyagali na Dr Slaa wakiwekwa ndani. Hata hivyo wakaja kuachiwa bila kesi kuunguruma mpaka mwisho. Hapa inaonyesha vyombo vyako vilichemsha

3. Wewe Rais serikali yako ilipeleka muswada bungeni wa kubadili sheria na kuifanya usalama wa Taifa iwe inakamata watu.
Mheshimwa Rais, kwa sheria hii uliyopeleka muswada wake bungeni na kisha kuisaini wewe mwenyewe wa kuwapa rungu watu hawa wa usalama wa Taifa kukamata watu, huku tukijua kuwa hawa hawana vituo vya kawaida vya kuhifadhi watuhumiwa, amabpo raia wanaweza kuwafuata, kuwajulia hali, wakawekwa kwenye reja za kawaida maana yake ni kuwa watu wa usalama wa Taifa wanafanya kazi gizani zaidi. Ni vigumu pia wananchi kuamini kuwa Idara hii pia katika masuala haya ya utekaji nchini.

4. Wapo wahanga wa utekaji na jeshi la polisi halijawahoji
Mtu kama SATIVA analalamika kutekwa, anatuma taarifa za watesi wake, alipigwa risasi akatupwa porini. Lakini jeshi la polisi halijaona umuhimu wa kumhoji ili kuchunguza tukio lake.

5. Wewe Mwenyewe umewahi kulituhumu jeshi la polisi kwa mauji
Uliagiza Waziri mkuu wakati fulani kuunda tume ya kulichunguza jeshi la polisi kwa mauji, ukasema jeshi la polisi lenyewe ni mtuhumiwa. Sasa kama wewe umewahi kudhani kuwa Si busara kwa jeshi la polisi kujichunguza kwa sababu ni mtuhumiwa, Je unadhani wananchi watakuwa na maoni tofauti katika matukio ya hivi karibuni ya mauaji ya mzee Ally Kibao na utekwaji wa watu mbalimbali hasa wananchama wa CHADEMA?

6. Juzi umesema ulisikia clip, Dr Slaa akizungumza tuhuma za utekaji hata hivyo vyombo vyako mpaka sasa vimezubaa havijamuita kumhoji kwa jambo hilo mpaka sasa
Mheshimiwa Rais, imagine wewe umepata clip ya Dr slaa akitoa kauli hiyo, tena miaka kadhaa iliyopita,lakini cha ajabu vyombo vyako eti havijaifanyia kazi clip hiyo kwa miaka yote hiyo. Sasa mheshimiwa rais kama vyombo vyako ni incompetent kiasi hiki, je unadhani raia wataamini kuwa vinao uwezo wa kuchunguza matukio kama hayo ambayo vimeshindwa kuchunguza kwa miaka kadhaa sasa?

SASA Mheshimiwa Rais:
Kama hilo jeshi lako la Polisi limeshindwa kufanya uchunguzi juu ya matukio lukuki ya utekwaji na mauaji nchini hasa yenye mrengo wa kisiasa unadhani wananchi watakuwa na imani na hilo unaloita "agizo" hivyo vyombo vichunguze?.
Mheshimiwa Rais nchi hii imewahi kuwaleta wachunguzi kutoka nje juu ya mauaji ya Padri huko Zanzibar, na sasa Wananchi wanataka wachunguzi huru waje wachunguze matendo ya kidhalimu kabisa ya mauaji ya watu wasi na hatia nchini.

BY THE WAY, TANGU LINI MTUHUMIWA AKAJICHUNGUZA MWENYEWE?
Ni hatari kubwa sana hii.

Masuala haya ya kutekana hapa Tanzania jinsi yanavyofanyika ni kama vile ilivyokuwa nchini Zaire (DRC) enzi za Utawala wa Dikteta Mobutu Sese Seko, Watu walikuwa wanatekwa mchana kweupe kama hivi wanavyofanya hawa Watekaji. Nchini Zaire ilikuwa ukitekwa basi utapelekwa moja kwa moja nyumbani kwake Rais Mobutu Sese Seko kwenye makazi yake yaliyopo katika Kijiji Cha Gbadolite ili ukateswe na kisha kuuawa. Hali ilikuwa mbaya sana kupita kiasi nchini Zaire, naona hali kama hiyo hiyo sasa hivi ipo nchini Tanzania. Ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa Umma na nchi yote kabisa kwa ujumla wake.
Matukio ya namna hii yana madhara mabaya sana ambayo kamwe hayataweza kuja kurekebishika.

Nashangaa Sana kuona kwamba Serikali iliyopo ipo kimyaaa kabisa licha ya kwamba vilio vya Wananchi ni vikubwa sana katika kulaani matukio ya namna hii. Kulikoni hasa huko Serikalini?

Je, ukimya huu wa Serikali na vyombo vyake vyote vya Dola kuhusiana na matukio mabaya Kama haya ya Utekaji unamaanisha Nini hasa??
 
Back
Top Bottom