Rais Samia, unda tume huru kuchunguza mauaji ya Hamza

Rais Samia, unda tume huru kuchunguza mauaji ya Hamza

Hamatan

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2020
Posts
3,197
Reaction score
7,677
Leo DCI ametoa taarifa aliyoiita kuwa ni matokeo ya uchunguzi.

Kwangu mimi, na nadhani kwa Watanzania walio wengi, Polisi hawakuwa taasisi sahihi ya kufanya uchunguzi wa mauaji yaliyofanywa na Hamza dhidi ya polisi na pia kifo chake yeye mwenyewe Hamza.

Kwa nini?

Katika tukio la mauaji ya polisi na Hamza, kulikuwa na maelezo kuwa mauaji ya Hamza yalikuwa ya kulipiza kisasi dhidi ya polisi ambao kabla ya shambulio, walikuwa wamempora mali yake. Hii tayari ilikuwa ni tuhuma dhidi ya Jeshi la Polisi, ambayo ilikuwa na uzito wa wazi kutokana na shambulio la Hamza kuwalenga polisi na siyo mauaji holela dhidi ya raia.

Hoja ya pili, kwetu tulio wengi, au hatuna imani au tuna imani ndogo kwa jeshi la polisi kutokana na historia ya jeshi hili. Miaka ya nyuma polisi waliwahi kupora pesa kutoka kwa wafanyabiashara wa madini, kisha wakawaua hao wafanyabiashara, tena wakaenda kuwaulia msituni.

Wakatengeneza kile walichokiita kamati ya uchunguzi, nayo ikaleta taarifa kuwa eti wale wafanyabiashara walikuwa majambazi, na walikufa kwa kupigwa risasi wakati wanakimbia kutoroka mkono wa dola.

Uchunguzi wa baadaye ulithibitisha kuwa polisi walifanya kazi kama genge la majambazi ambapo wapo waliowapora wafanyabiashara wale, wengine wakawaua, na wengine wakawalinda wahalifu wenzao kwa kutoa taarifa ya uwongo dhidi ya marehemu.

Tunataka kuujua ukweli, na ukweli hauwezi kutoka kwa mtuhumiwa. Polisi nao, kama wanataka kujisafisha na tuhuma hizi, nao wasisitize uchunguzi ufanywe na chombo kingine, kilicho huru.

Uchunguzi wa kitaalam, wa kina na ulio wa kweli ndio utakaolisababishia Taifa kuepuka matukio ya kutisha kama haya yaliyotokea hivi karibuni.

Mungu naomba uwajalie hekima watawala katika kufanya maamuzi yenye kulihakikishia amani ya kweli Taifa letu.
 
Mnavyo muamini huyo mama! Yaani utafikiri ni Malaika vile aliye shuka kutoka Mbinguni! Kumbe ni Kada tu wa chama kinacho ishi na kupumua kwa msaada wa polisi hao hao!!
 
Amiri jeshi mkuu Mwigulu Nchemba hawezi kuruhusu hilo.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]mkuu BAK you made my day kiongozi wangu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Hawawezi kuunda tume huru, wanataka kutulewesha na maneno yao ili tuwaamini, wanajua Tume huru inaweza kuja na maneno tofauti na tuliyoambiwa na DCI.
 
Ugaidi ni mbaya na hakuna anaefurahia
Na tukio liliotokea asilimia kubwa sana ingekemea na kulaani kwa nguvu moja kama hii tuhuma ya kuporwa mali yake isingejitokeza

Lisemwalo lipo ndio maana wengi tumeshindwa kuamini ukweli ni upi

Polisi nao ni binadamu kwa hiyo nao kufanya tofauti na kazi zao walizoapa kuzifanya huwa yanatokea sio kwetu tu bali duniani kote
Sio aibu bali ni kujua ukweli
 
Mtu kaua mchana kweupe alafu aundiwe tume!!

Mnachekesha sana
Wauaji wamekuwepo nyakati zote, lakini je, kila anayeua ni gaidi?

Kuna swali muhimu kuliko yote ambalo ni kwa nini Hamza alifanya mauaji yale tena ambayo yalilenga polisi tu?
 
Mtu kaua mchana kweupe alafu aundiwe tume!!

Mnachekesha sana
Hata wake wafanyabiashara wa madini waliuawa mchana kweupe na kina zombe na jk alifanya uchunguzi wakaja na majibu,unashangaa hii?
 
Wapinzani mnatiaga kinyaa.kwa nini mnapenda kushabikia matukio bila kutumia akili
 
Leo DCI ametoa taarifa aliyoiita kuwa ni matokeo ya uchunguzi.

Kwangu mimi, na nadhani kwa Watanzania walio wengi, Polisi hawakuwa taasisi sahihi ya kufanya uchunguzi wa mauaji yaliyofanywa na Hamza dhidi ya polisi na pia kifo chake yeye mwenyewe Hamza.

Kwa nini?

Katika tukio la mauaji ya polisi na Hamza, kulikuwa na maelezo kuwa mauaji ya Hamza yalikuwa ya kulipiza kisasi dhidi ya polisi ambao kabla ya shambulio, walikuwa wamempora mali yake. Hii tayari ilikuwa ni tuhuma dhidi ya Jeshi la Polisi, ambayo ilikuwa na uzito wa wazi kutokana na shambulio la Hamza kuwalenga polisi na siyo mauaji holela dhidi ya raia.

Hoja ya pili, kwetu tulio wengi, au hatuna imani au tuna imani ndogo kwa jeshi la polisi kutokana na historia ya jeshi hili. Miaka ya nyuma polisi waliwahi kupora pesa kutoka kwa wafanyabiashara wa madini, kisha wakawaua hao wafanyabiashara, tena wakaenda kuwaulia msituni.

Wakatengeneza kile walichokiita kamati ya uchunguzi, nayo ikaleta taarifa kuwa eti wale wafanyabiashara walikuwa majambazi, na walikufa kwa kupigwa risasi wakati wanakimbia kutoroka mkono wa dola.

Uchunguzi wa baadaye ulithibitisha kuwa polisi walifanya kazi kama genge la majambazi ambapo wapo waliowapora wafanyabiashara wale, wengine wakawaua, na wengine wakawalinda wahalifu wenzao kwa kutoa taarifa ya uwongo dhidi ya marehemu.

Tunataka kuujua ukweli, na ukweli hauwezi kutoka kwa mtuhumiwa. Polisi nao, kama wanataka kujisafisha na tuhuma hizi, nao wasisitize uchunguzi ufanywe na chombo kingine, kilicho huru.

Uchunguzi wa kitaalam, wa kina na ulio wa kweli ndio utakaolisababishia Taifa kuepuka matukio ya kutisha kama haya yaliyotokea hivi karibuni.

Mungu naomba uwajalie hekima watawala katika kufanya maamuzi yenye kulihakikishia amani ya kweli Taifa letu.

Hamza alidhulumu roho za watu wasio na hatia. halafu leo wajinga wanataka tuamini alionewa. Gaidi. Tena gaidi mwenye kitambi sababu ya kula mema ya nchi bila kutolea jasho.
Dini wote tuna dini. Tuache masikhara hapa kwamba mtu fulani ndio anahaki zaidi ya mwingine sababu ya dini au rangi au kabila au chochote kile kisicho na mashiko
 
Hamza alidhulumu roho za watu wasio na hatia. halafu leo wajinga wanataka tuamini alionewa. Gaidi. Tena gaidi mwenye kitambi sababu ya kula mema ya nchi bila kutolea jasho.
Dini wote tuna dini. Tuache masikhara hapa kwamba mtu fulani ndio anahaki zaidi ya mwingine sababu ya dini au rangi au kabila au chochote kile kisicho na mashiko
Kengelisim
 
Leo DCI ametoa taarifa aliyoiita kuwa ni matokeo ya uchunguzi.

Kwangu mimi, na nadhani kwa Watanzania walio wengi, Polisi hawakuwa taasisi sahihi ya kufanya uchunguzi wa mauaji yaliyofanywa na Hamza dhidi ya polisi na pia kifo chake yeye mwenyewe Hamza.

Kwa nini?

Katika tukio la mauaji ya polisi na Hamza, kulikuwa na maelezo kuwa mauaji ya Hamza yalikuwa ya kulipiza kisasi dhidi ya polisi ambao kabla ya shambulio, walikuwa wamempora mali yake. Hii tayari ilikuwa ni tuhuma dhidi ya Jeshi la Polisi, ambayo ilikuwa na uzito wa wazi kutokana na shambulio la Hamza kuwalenga polisi na siyo mauaji holela dhidi ya raia.

Hoja ya pili, kwetu tulio wengi, au hatuna imani au tuna imani ndogo kwa jeshi la polisi kutokana na historia ya jeshi hili. Miaka ya nyuma polisi waliwahi kupora pesa kutoka kwa wafanyabiashara wa madini, kisha wakawaua hao wafanyabiashara, tena wakaenda kuwaulia msituni.

Wakatengeneza kile walichokiita kamati ya uchunguzi, nayo ikaleta taarifa kuwa eti wale wafanyabiashara walikuwa majambazi, na walikufa kwa kupigwa risasi wakati wanakimbia kutoroka mkono wa dola.

Uchunguzi wa baadaye ulithibitisha kuwa polisi walifanya kazi kama genge la majambazi ambapo wapo waliowapora wafanyabiashara wale, wengine wakawaua, na wengine wakawalinda wahalifu wenzao kwa kutoa taarifa ya uwongo dhidi ya marehemu.

Tunataka kuujua ukweli, na ukweli hauwezi kutoka kwa mtuhumiwa. Polisi nao, kama wanataka kujisafisha na tuhuma hizi, nao wasisitize uchunguzi ufanywe na chombo kingine, kilicho huru.

Uchunguzi wa kitaalam, wa kina na ulio wa kweli ndio utakaolisababishia Taifa kuepuka matukio ya kutisha kama haya yaliyotokea hivi karibuni.

Mungu naomba uwajalie hekima watawala katika kufanya maamuzi yenye kulihakikishia amani ya kweli Taifa letu.
Wawaite FBI au Scotland Yard siku mbili tu watatoa majibu sahihi
 
Back
Top Bottom