Rais Samia: Wakuu wa Mashirika walikuwa wanakopa fedha Benki ili walipe Gawio Serikalini kulinda vibarua vyao

Rais Samia: Wakuu wa Mashirika walikuwa wanakopa fedha Benki ili walipe Gawio Serikalini kulinda vibarua vyao

Kitu pekee nachoweza kuamini Ni Magufuli alidanganya hivo hakukuwa na gawio alilopokea, lakini kusema mikopo ilichukuliwa Bank Ni uongo,
Yeye kama mkuu wa nchi alipokuwa anakopa bank kwa ajili ya hii miradi alikuwa anaweka dhamana gani?
 
Hapa nahisi ni chai

Mikopo yote ina records BOT. Sasa gavana wa BOT asimwambie Magufuli kweli?
Kama na yeye alikuwa anashiriki ili kuaminisha watu mambo yapo sawa na utawala wake umeleta ufanisi je?
 
Halafu Magufuli asijue kama wamechukuwa hela ktk central Bank ? Raisi yuko karibu na Gavana wa Benki anakuwa briefed kila kinachoendelea, asiambiwe kama shirika xyz limekopa ?
Wewe bhana kama tuliweza kudanganywa kuhusu ndege kuingiza faida hewa hata kwa hili hawashindwi
 
Kama na yeye alikuwa anashiriki ili kuaminisha watu mambo yapo sawa na utawala wake umeleta ufanisi je?
Umenena vyema mkuu, kwenye ndege tuliaminishwa haya haya kumbe kuna hasara kubwa
 
Siyo swala la kuabudu, ni logic ya kawaida tu, Central Bank hawafanyi kazi kienyeji kama ni kweli walikopa fedha kama hata hilo linawezekana sijui ni lazima raisi angejua!
Kwani huo mkopo analipa Magufuli ama shirika husika? Yeye alichojali ni hela ipatikane kwa njia yoyote bila kujali athari zake.
 
Halafu Magufuli asijue kama wamechukuwa hela ktk central Bank ? Raisi yuko karibu na Gavana wa Benki anakuwa briefed kila kinachoendelea, asiambiwe kama shirika xyz limekopa ?
Na kama yeye ndio alikuwa anawaambia hata kama hamna hela nendeni mkakope mradi ionekane mmetoa Gawio
Labda who knows
 
Mkuu labda hujaielewa vizuri mada
Kipindi Cha mwendazake mashiriks mengi yalirudisha gawio kwa SERIKALI ambalo Raisi ametolea tamko kuwa walirudisha gawio kwa kukopa Central Bank.
Ndo mana umeona nimejiuliza hayo MASWALI juu
 
Na wewe unaamini huu uongo ? ,CEO wa shirika la umma akope zaidi ya 1 billion aliweka Nini huko Bank Kama dhamana, na Jiwe asijue ? Na Kama kweli walikopa while shirika linapata loss pesa ya kulipa ilitoka wapi
Hawakulipa ndo maana ilikuwa vigumu kuwaondoa dhama ilikua ni serkali na ilikua lazima.
 
Records ziko wapi? Unaweza tu kukopa hela Central bank bila ya records zozote mahali na jinsi ya kuzirudisha? Na kama ni kweli kwamba walikuwa wanakopa ktk central Bank ili kumfurahisha Magufuli, je raisi Magufuli angeweza kutoligundua/kuambiwa hilo? I mean, huyo mtu sijui tu kwa kweli kwa maana dah!
Inasemekana kuna kijana alikuwa na nguvu kuliko katiba
 
Records ziko wapi? Unaweza tu kukopa hela Central bank bila ya records zozote mahali na jinsi ya kuzirudisha? Na kama ni kweli kwamba walikuwa wanakopa ktk central Bank ili kumfurahisha Magufuli, je raisi Magufuli angeweza kutoligundua/kuambiwa hilo? I mean, huyo mtu sijui tu kwa kweli kwa maana dah!
Na kwa nini mama alikaa kimya zaidi ya miaka 5 ANAKUJA sema Sasa? Kwa hiyo naye alikuwa ana Linda kibarua chake? Mama mambo mengine Kaa kimya kwani ulikuwa msaidizi wa kulia wa unaye 'mnanga'. Hebu mwacheni Magu apumzike. Au kivuli chake bado kinawatokea watu nini? Hata mahakama hufuta kesi ya mtuhumiwa ikijiridhisha kweli kafa. Au Magu hajafa nini?
 
Bora hata walikopa kutoa gawio ili mradi maisha kwa wananchi yalikuwa mazuri tofauti na awamu hii ya sita ambayo imeanzisha tozo lukuki na kusababisha mfumuko wa bei ambao haujawahi kutokea toka tupate uhuru
 
Mmh walikuwa wanakopa kwa kuweka dhamana vitu gani? BOT kama Regulator wa Industry hakuweza kulijua ilo na kubrief President kweli, Nakubali kuwa magufuli alipika data nyingi sana Kuhusu Dividend zilizokuwa zinatolewa na mashirika ya Umma ila hili la CEO kukopq ili watoe Gawio hapana kwa kweli
Halafu zinalipwaje? Report za CAG hazikuona hilo? Tena Assad!!
 
Back
Top Bottom