Rais Samia: Wameanza kuandika kwenye vigazeti kwamba sitasimama 2025, nani kawaambia?

Rais Samia: Wameanza kuandika kwenye vigazeti kwamba sitasimama 2025, nani kawaambia?

Kama kauli hii kaitoa rais SSH tayari ameshapoteza mwelekeo hakuna atakayemchagua Mbeya, Mwanza, Arusha na Dar Es Salaam

Utajitangazaje utagombea urais wakati una miezi sita tu tangu ushike madaraka ya ngekewa

Kauli gani gani yenye ukakasi kama hii?

Kwa hiyo JPM aliangamizwa na nini ili wadai ni kudra ya menyezi Mungu wachukue nafasi ya urais?

Kwa hiyo hata madai yanayodaiwa kwamba JPM alihujumiwa ni kweli na yeye anajua?

Wanawake anaojifariji watampigia kura ndio hawamtaki kabisa kumsikia lakini wanamg'ong'a

*She will never be voted by anybody nor win the general election race come 2025.

"Kufika hapa, kama isingekuwa kudra ya Mungu ingekuwa ngumu sana, sasa ndugu zangu Rais mwanamke tutamuweka 2025. Mwaka 2025 tukifanya vitu vyetu vizuri, tukishikamana, tukimuweka Rais wetu, tutakutana hapa kwa furaha kubwa sana
Wameanza kutuchokoza kuandika kwenye vigazeti kwamba Samia hatasimama, nani kawaambia? Wanawake oyee. Fadhila za mwenyezi Mungu zikija mikononi mwako usiziachie.
Wanawake wamefanya kazi kubwa kuleta uhuru wa nchi hii, Wanawake tumefanya kazi kubwa kujenga siasa za nchi hii, tumebeba sana wanaume katika siasa za nchi hii, leo Mungu ametupa baraka mikononi, tukiiachia Mungu atatulaani"


Hii kauli amewadhalilisha sana wanaume kwa kujiona anauwezo na nguvu cha kufanya chochote kwa raia wa nchi-NO
Kumbe jpm was kudra?? So it's possible and confirmed?? Saw bhana..
 
CCM imuweke SAMIA kugombea?

Najua mara zote huwa inafanya dhuluma lakini sifa za mgombea aliyepo huwafanya angalau wapate hata 50% za ukweli alafu ndo waibe nyingine hata 20% Ili kujazia.

Kumuweka SAMIA itawaladhimu kuiba zaidi ya asilimia 60% ya kura Ili apite,kitu ambacho kitawaladhimu kutumia nguvu kibwa sana kuliko zile waliowahi kutumia huko nyuma na hapo ndipo tunaweza kuliingiza Taifa katika phase nyingine kabisa (maana kuna muda unapigwa tukio hata kuiba inabaki kuwa aibu) waangalizi ZAMBIA kama mfano, au ile nchi aliyowahi kuirithi Joyce banda.

Akisimama SAMIA 2025, kushinda kwa upinzani kutakuwa si kigumu tena, itategemeana tu na watakae msimamisha(asiwe LISSU), maana kuliuhalisia tangu 2015 CCM ilishachokwa watu walichagua mtu (Magufuli) na sio kwa mapenzi ya chama.

Nakumbuka uke muda JK anataka kutoka, iliafika muda hata mtu akivaa tu nguo ya CCM alikuwa anazomewa mitaani, Magufuli aliweza kuirudisha ila hadhi japo kwa uchache, na aliweza kwa kuwashika majority kwa ujenzi wake wa miundombinu huku akiwafinya minority.

SAMIA hafit, anyways huwezi jua labda mwisho wa CCM ndo unafika kwa style hii.
Miezi sita waliobaki wanamsifia ni wasanii, wapiga deal na wanasiasa.

Wengine wote hawana hamu nae kutwa anasafiri na kufanya kazi ya kukutana watu au makundi ya watu; shida za wananchi hazijui.

Huko kwenye halmashauri michezo michafu imerudi kwa kasi ya 4G.
 
Aisee huyu ni sawa na mama yangu

USSR
Kumbe huwa tunapigizana kelele na watoto tu humu? Na wengine unakuta mnatukana tu watu hovyohovyo humu.

Kwahiyo mtu wa miaka 60 anaweza kukuzaa ? Sawa.
 
Kaongea na nani haya masuala? Kwani mzanzibari bado ataendelea kuongoza bara? Zanzibar watakubali mbara akienda kuongoza kwao?

Akija mwinyi mama akaenda znz yote sawa. Wote wako vizuli. Mwenyezi Mungu awabaliki.
 
Mbona kama 2025 mbali sana! Anyway, wanasiasa hao...tusiwaamini sana!
 
Hawa watu ndio maana wanakufaga kibudu. Unahudhuria maadhimisho ya demokrasia gani unayo practice kama sio unafki mkubwa!!!

Huyo hata ma ccm wenzake wahawezi kukubali arudi madarakani.
Hawana ubavu, yeye ana nguvu zote.
 
“Rais mwanamke tutamuweka mwaka 2025, tukifanya vitu vyetu vizuri, tukishikamana tutakutana hapa kwa furaha kubwa sana, wameanza kutuchokoza kuandika kwenye vigazeti Samia hatasimama nani kawaambia? - Rais Samia Suluhu Hassan

#UnokoNiUzalendo

View attachment 1938721

Uyu mama tunampenda sana. Mungu ampe afya na umri mrefu mama etu. Anahekima, busara na huluma.
 
Miezi sita waliobaki wanamsifia ni wasanii, wapiga deal na wanasiasa.

Wengine wote hawana hamu nae kutwa anasafiri na kufanya kazi ya kukutana watu au makundi ya watu; shida za wananchi hazijui.

Huko kwenye halmashauri michezo michafu imerudi kwa kasi ya 4G.
Kuna watu watabisha tu hapa, ila kiuhalisia anachukiwa mpaka na baadhi ya wanawake wenzake.

Watakaomsifia hawawezi kukosekana, ila wengi wao wameegemea zaidi katika malengo wa Feminism, Dini, uzanzibar na wengine ni wale wanaonufaika na uwepo wake pale.

Tofauti na hapo, SAMIA hii nchi imeshamshinda mapema sana.Si kwasababu ni mpole ni kwasababu haelewi afanye nini licha ya kuwa ikulu kwa zaidi ya miaka sita.
 
Miezi sita waliobaki wanamsifia ni wasanii, wapiga deal na wanasiasa.

Wengine wote hawana hamu nae kutwa anasafiri na kufanya kazi ya kukutana watu au makundi ya watu; shida za wananchi hazijui.

Huko kwenye halmashauri michezo michafu imerudi kwa kasi ya 4G.
Lini halimshauri zilitulia , watanzania ni wezi na wavivu

USSR
 
Rais Samia Suluhu Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Demokrasia Duniani Mkoani Dar amesema wanawake bado hawajamuweka Rais mwanamke bali aliyekuwepo amepatikana kwa kudra ya Mungu na matakwa ya katiba. Amesema walichofanikiwa wanawake ni kusukuma mpaka kumpata makamu wa Rais mwanamke.

"Kufika hapa, kama isingekuwa kudra ya Mungu ingekuwa ngumu sana, sasa ndugu zangu Rais mwanamke tutamuweka 2025. Mwaka 2025 tukifanya vitu vyetu vizuri, tukishikamana, tukimuweka Rais wetu, tutakutana hapa kwa furaha kubwa sana

Wameanza kutuchokoza kuandika kwenye vigazeti kwamba Samia hatasimama, nani kawaambia? Wanawake oyee. Fadhila za mwenyezi Mungu zikija mikononi mwako usiziachie.

Wanawake wamefanya kazi kubwa kuleta uhuru wa nchi hii, Wanawake tumefanya kazi kubwa kujenga siasa za nchi hii, tumebeba sana wanaume katika siasa za nchi hii, leo Mungu ametupa baraka mikononi, tukiiachia Mungu atatulaani.


Alisema Rais Samia Suluhu


Mengineyo, Rais Samia amesema ataendeleza mema yote katika awamu zote na watajitahidi kuongeza mema mengine.

Kuhusu usawa wa jinsia amesema hawajafika lakini wanawake wataendelea kuongezeka kwani asipofanya yeye hakuna ambae atafanya.
Raisi kuwa mwanamke au mwanaume si issue. Tunataka raisi atakyeheshimu katiba hata hii iliyopo yenye matatizo.
aAkija mwinyi mama akaenda znz yote sawa. Wote wako vizuli. Mwenyezi Mungu awabaliki.
Afadhali Mwinyi ana ubara kidogo na yuko vizuri. Mama tozo, petroli inapanda kila kukicha, mafuta ya kula yanapanda nk. Yaani haangalii vitu vianvyomgusa mwananchi wa kawaida!!!! Tumelalamika wanapunguza only 30%. Tumegoma kutumia miamala ya simu tukaanza kutumia simbanking akaingia huko nako!!!! Ili mradi tu tukome ubishi!!!
 
Back
Top Bottom