Rais Samia: Wanaolipa kodi Tanzania ni milioni 2 tu

Rais Samia: Wanaolipa kodi Tanzania ni milioni 2 tu

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema wanaolipa kodi halisi Nchini ni Watu milioni mbili tu kati ya Watu milioni 65 ambapo amesema idadi hiyo ni ndogo sana hivyo amewataka Watanzania wengi zaidi walipe kodi ili kuchangia uchumi wa Taifa.

Rais Samia amesema hayo leo October 04,2024 Ikulu Jijini Dar es salaam wakati akiizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi.

“Kwa idadi yetu ya Watu, wanaolipa kodi halisi ni Watu wachache, ni Watu kama milioni mbili kati ya Watu milioni 65 sasa ukitoa Watoto na wengine ambao hawapaswi kukatwa kodi hatupungui labda milioni 37 ambao tunaweza kulipa kodi lakini wanaolipa kodi ni milioni mbili, sasa hii idadi ni ndogo, ni ndogo sana, ina maana Watu kidogo wanalipa kwa fursa ya kuwajenga Watu wengi hatuwezi kufika, lazima wote tuchangie kila Mtu kwa kiasi chake ili tuweze kufanya mengi.

Ubabe katika kukusanya Kodi
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema bado kuna malalamiko kutoka kwa Wafanyabiashara wanaolalamikia weledi kutozingatiwa wakati wa kukusanya kodi ikiwemo matumizi ya nguvu, lugha zisizo na staha na ubabe kwa baadhi ya Watumishi wa Serikali wanaohusika na utozaji kodi.

Akiongea leo October 04,2024 Ikulu Jijini Dar es salaam wakati akizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi, Rais Samia amesema “Baadhi ya Wafanyabiashara wanalalamikia wingi wa kodi na tozo lakini pia viwango vya kodi kutokuwa rafiki na hii ni kawaida, unajua Mtu ana hiyari kwenda kulipa faini bila kulazimishwa mwenyewe kwasababu faini ni kodi inayotokana na kosa, kwahiyo Mtu analipa ili asiende Jela lakini kodi tunayoizungumzia hapa ni kodi inayotokana na kitu kizuri”

“Sasa Mtu anaona nimefanya biashara nimepata pesa yangu kisha nikaipe Serikali bure lakini anasahau huduma inayotolewa na Serikali kwake na mazingira iliyomjengea kuweza kufanya biashara na kupata faida, kwahiyo ni maumbile ya Binadamu kuona kulipa kodi ni adhabu kumbe kulipa faini ni adhabu na Watu wanakwenda haraka, kwahiyo tuna tatizo ndani ya Nchi, Wafanyabiashara wanaamini hali hii inachangia mianya ya rushwa”

“Kuna malalamiko ya weledi kutozingatiwa wakati wa kukusanya kodi, mfano matumizi ya nguvu, lugha zisizo na staha na ubabe kwa baadhi ya Watumishi wa Serikali na baadhi ya biashara kutozwa kodi au tozo zinazoshabihiana na Taasisi zaidi ya moja kwahiyo hapa napo kuna mashakamashaka ambayo inatakiwa yakatazamwe”

PIA SOMA
- Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?
-Rais Samia: Uchumi wetu unakua lakini tunachokusanya, kingi kinaingia mifukoni kwa Wa
 
Nimeshindwa kumuelewa Rais anaposema nchi ina watu milioni 65 ila wanaolipa kodi ni watu milioni 2 tu!

Najiuliza sipati jibu!

Anataka WENDAWAZIMU, VICHAA, WASIO NA KAZI, WATOTO, VICHANGA walipe kodi!

Kwamba kila Mtanzania hata akizaliwa leo anatakiwa kulipa kodi1😅😅😅
 
... ilitakiwa under 18 wote, wanafunzi wote, wazee wote over 60 wawe excluded from the overall population kwanza. Ku-include hadi kids it doesn't depict the true tax base population.
 
Rais aseme ni kodi ipi hiyo wanayolipa watu Million mbili..Mimi navyo jua kila mtanzania analipa kodi nikinunua azam juice nimeshakatwa kodi.Swali dogo tu watumiaji wa simu tz ni million mbili tu ama ???Maana huko tuna limwa mi tozo na VAT au hizo sio kodi.
 
Usikute ile idadi nyingine makusanyo yake yanauelekeo mwingine kabisa. Hii nchi bana acha kabisa.

Kama kuna watu walikuwa wanaingiza 7m kwa dk/sec usishange walipakodi wengine milioni 2 zinachukuliwa na wajanja.
 
Nimeshindwa kumuelewa Rais anaposema nchi ina watu milioni 65 ila wanaolipa kodi ni watu milioni 2 tu!

Najiuliza sipati jibu!

Anataka WENDAWAZIMU, VICHAA, WASIO NA KAZI, WATOTO, VICHANGA walipe kodi!
Mi najiuliza Ile asilimia 18 ya vat kwenye bidhaa inaitwaje, au Ile mchanganuo tunaoona tukinunua vocha za simu au tukibet inaitwaje, au tukinunua fegi, au mahitaji mengine au tra wanatudanganya kwenye risiti za efd tunazopewa madukani kwamba kile kllichokatwa ni kitu Gani vile!! Yaan maswali ni mengi mno
 
Hiyo milioni mbili inahitaji mtu mwenye A8 kuielezea na akaeleweka kwa jamii vinginevyo ni siasa tu.
Kodi inalipwa na kila mtu kupitia manunuzi kuanzia vitu vidogo kama pipi, na kulipia huduma kama umeme, kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu, n.k.
Hiyo milioni 2 ingepanda kama rais, na wabunge wangelipa kodi pia.
 
Njia pekee ya kuongeza tax base kwa kiasi kikubwa ni kupiga marufuku umachinga rasmi, kila mjasiriamali (mkubwa au mdogo) awe na business license na tax ID number
 
Hapo kuna changa la macho. Huenda TRA na halmashauri wanapiga mzigo mkubwa sana halafu wanawasilisha kiduchu kwa kisingizio cha kwamba walipa kodi ni milioni mbili tu, au serikali inaleta kisingizio kwa kushindwa kwake kuleta huduma bora za kijamii kwa wananchi.
 
Wafanyakazi wote ambao wameajiliwa sehemu rasmi iwe serikalini au sekta binafsi wanalipa Kodi ya PAYE ( pay as you earn) Raia wote wengne wanalipa pia kupitia bidha wanazonunua indirectly ( Indirect tax) huyo mmama asidhani watanzania wote wajinga. Million mbili anaongelea wafanyabiashara na makampuni ambao wenyewe wanakamua kutoka kwa raia. Rubbish kabsa,
#No malice to anybody
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema wanaolipa kodi halisi Nchini ni Watu milioni mbili tu kati ya Watu milioni 65 ambapo amesema idadi hiyo ni ndogo sana hivyo amewataka Watanzania wengi zaidi walipe kodi ili kuchangia uchumi wa Taifa.

Rais Samia amesema hayo leo October 04,2024 Ikulu Jijini Dar es salaam wakati akiizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi.

“Kwa idadi yetu ya Watu, wanaolipa kodi halisi ni Watu wachache, ni Watu kama milioni mbili kati ya Watu milioni 65 sasa ukitoa Watoto na wengine ambao hawapaswi kukatwa kodi hatupungui labda milioni 37 ambao tunaweza kulipa kodi lakini wanaolipa kodi ni milioni mbili, sasa hii idadi ni ndogo, ni ndogo sana, ina maana Watu kidogo wanalipa kwa fursa ya kuwajenga Watu wengi hatuwezi kufika, lazima wote tuchangie kila Mtu kwa kiasi chake ili tuweze kufanya mengi.

Ubabe katika kukusanya Kodi
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema bado kuna malalamiko kutoka kwa Wafanyabiashara wanaolalamikia weledi kutozingatiwa wakati wa kukusanya kodi ikiwemo matumizi ya nguvu, lugha zisizo na staha na ubabe kwa baadhi ya Watumishi wa Serikali wanaohusika na utozaji kodi.

Akiongea leo October 04,2024 Ikulu Jijini Dar es salaam wakati akizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi, Rais Samia amesema “Baadhi ya Wafanyabiashara wanalalamikia wingi wa kodi na tozo lakini pia viwango vya kodi kutokuwa rafiki na hii ni kawaida, unajua Mtu ana hiyari kwenda kulipa faini bila kulazimishwa mwenyewe kwasababu faini ni kodi inayotokana na kosa, kwahiyo Mtu analipa ili asiende Jela lakini kodi tunayoizungumzia hapa ni kodi inayotokana na kitu kizuri”

“Sasa Mtu anaona nimefanya biashara nimepata pesa yangu kisha nikaipe Serikali bure lakini anasahau huduma inayotolewa na Serikali kwake na mazingira iliyomjengea kuweza kufanya biashara na kupata faida, kwahiyo ni maumbile ya Binadamu kuona kulipa kodi ni adhabu kumbe kulipa faini ni adhabu na Watu wanakwenda haraka, kwahiyo tuna tatizo ndani ya Nchi, Wafanyabiashara wanaamini hali hii inachangia mianya ya rushwa”

“Kuna malalamiko ya weledi kutozingatiwa wakati wa kukusanya kodi, mfano matumizi ya nguvu, lugha zisizo na staha na ubabe kwa baadhi ya Watumishi wa Serikali na baadhi ya biashara kutozwa kodi au tozo zinazoshabihiana na Taasisi zaidi ya moja kwahiyo hapa napo kuna mashakamashaka ambayo inatakiwa yakatazamwe”

PIA SOMA
- Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?
-Rais Samia: Uchumi wetu unakua lakini tunachokusanya, kingi kinaingia mifukoni kwa Wa
Aanze na wanasiasa wanaomzunguka. Pia Kila anayechukua form ya kugombea nafasi yoyote afanyiwe tax clearance.
Sababu nahisi wanasiasa ndio wanaongoza kukwepa Kodi.
Sijasoma habari zaidi ya heading
 
Kuna
1. Tax (Kodi)
2. Charges (Tozo)
3. Levy (Ushuru)

Watu hawalipi kodi kwasababu charges na levy ni nyingi sana sasa ukiongeza na kulipa kodi ni sawa hiyo kazi unaifanyia serikali na mwenye nyumba labda na maonesho kwamba unaamka asubuhi nawe una mahali unakwenda kushinda basi. Ndio maana watu wana opt wasilipe/wakwepe kodi.

Ushauri japo najua hauwezi fanyiwa kazi. Chagueni kufuta kodi zibaki charges and levy au zifutwe charges and levy ibaki kodi then boom 💥 muujiza makusanyo yataongezeka achana na maigizo ya sasa ya TRA.
 
Back
Top Bottom