Rais Samia: Wanaolipa kodi Tanzania ni milioni 2 tu

Rais Samia: Wanaolipa kodi Tanzania ni milioni 2 tu

Kukatwa Kodi haimaanishi wewe ni mlipa Kodi.Kama huna TIN wewe sio mlipakodi.
"...kukatwa Kodi haimanishi wewe ni mlipa kodi...". Inamaanisha nini? Au ndo na yy anavofikiri?! Kwani hajui unaponunua chchte unakua umelipa kodi!? Kwamba hata watt wakinunua pp wanalipa? Tozo? Ushuru? VAT? PAYE? TAX ...nk. Wamekadiria kkukusanya 28tri/-. Kwa msingi huo, kila 1 wa hao 2 mil. wanaolipa, anatarajiwa alipe 14tri/-!? Matango pori ...duh!
 
Waandika hotuba za Rais watakuwa wanamdanganya mchana kweupe. Kwani ulipaji Kodi unahusu nini? Maana Nchi kila kitu utakachofanya cha halali lazima ulipe Kodi. Ina maana wanajishughulisha Nchi hii ni milioni 2? Mbona ni suala rahisi kula, kuvaa na usafiri si unalipa Kodi. Wanaofanya hivyo Tanzania ni milioni 2? Ya kuambiwa......
 
Kuna
1. Tax (Kodi)
2. Charges (Tozo)
3. Levy (Ushuru)

Watu hawalipi kodi kwasababu charges na levy ni nyingi sana sasa ukiongeza na kulipa kodi ni sawa hiyo kazi unaifanyia serikali na mwenye nyumba labda na maonesho kwamba unaamka asubuhi nawe una mahali unakwenda kushinda basi. Ndio maana watu wana opt wasilipe/wakwepe kodi.

Ushauri japo najua hauwezi fanyiwa kazi. Chagueni kufuta kodi zibaki charges and levy au zifutwe charges and levy ibaki kodi then boom 💥 muujiza makusanyo yataongezeka achana na maigizo ya sasa ya TRA.
Chukulia mfano tu mafuta ya dizel na petrol makato ni lukuki. Inamaana watumiaji milioni 2? Come on! Watanzania mbona tunafanyiana mzaha kana kwamba watu hawaelewi wakati ni suala simple tu.
 
Mh. Rais hapo umedanganywa. Waliokupa hiyo taarifa wafafanue vizuri vinginevyo Watanzania hatukuelewi. Watanzania karibu wote tunalipa 18% ya thamani ya bid haai tunazonunua zitokanazo na viwanda. Je idadi hiyo ni milioni mbili au ni milioni 37 kama ulivyoeleza katika hotuba yako?
Wafanyakazi wote katika Serikali na Sekta binafsi wanalipa PAYE. Je jumla yao kwa Tanzania wapo wangapi, waliokuabdalia taarifa wakupe takwimu.
Wafanyabiasha(kampuni na watu) binafsi wenye TIN namba ni idadi gani kati yao ni wangapi wanalipa kodi?
Licha ya kodi hizo kuna too nyingi kwenye miahamala kwenye simu na mabenki.
Itakuwa sahihi ukitumbia kodi tunazolipa zinaingia mifuko binafsi kama ulivyosema na sio kuwa watanzania milioni 2 tu ndiyo tunalipa kodi ndiyo change cha sisi kuwa tunaomba misaada toka nje.
Ukiwa kiongozi mkuu wa Nchi na umeelezwa kuwa kudi zinzokusanywa zinaingia mifuko binafsi umechukua hatua gani? Waliokipa taarifa wataje hiyo mifuko binfsi kodi zetu zinapoenda.

Kweli hii inatuumiza sana Watanzania.
 
IMG_4266.jpeg

WATANZANIA MNAJUA KUA RAIS ALIONDOLEWA KWENYE MFUMO WA KULIPA KODI ?

Sasa naona na yeye anashangaa kua idadi ya walipa kodi ni ndogo.
 
Na wabunge wote hawalipi Kodi ..... Na Anatoka anashangaaa ..... Na wananchi wamamshangaa huyu vipi.....
 
Ukiongea kitu ambacho hukijui vizuri au kwa kuambiwa tu matokeo yake ni kama hayo.
Za kuambiwa changanya na zako (j. Kikwete)
 
Ye mwenyewe halipi kodi, halafu sie wachache tulipe kodi atumie pesa zetu kununulia mabao ya mama na kuhonga wasanii?!.
 
Tumechoka kusikia hizi blah blah
ukinunua hata pipi ya mtoto au nepi za mtoto umesha changia kodi humo !
Hao wafanya biashara ni wakusanyaji tu wa kodi wanao fahamika 😳 !

Bidhaa zao wanazozalisha na wanazoziuza na hata huduma wanazozitoa zote wanaweka na gharama za kodi zao na mpaka faida watakayoipata itatoka kwa hao hao walaji wa hizo bidhaa na huduma wanazozitoa kwa hao walaji wa mwisho !
Maajabu ya tafsiri ya walipa kodi iliyowekwa na wanaoitwa wataalamu wa masuala ya kodi ni kwamba Eti yule mfanyabiashara anayekusanya mauzo kutoka kwa walaji ambayo yameshawekwa na kodi zote kwenye hizo bidhaa na kwenye huduma zote anahesabika yeye ndiye mlipa kodi 😂😂😅 !
Haya kwangu ni maajabu 😱 !
 
ukinunua hata pipi ya mtoto au nepi za mtoto umesha changia kodi humo !
Hao wafanya biashara ni wakusanyaji tu wa kodi wanao fahamika 😳 !

Bidhaa zao wanazozalisha na wanazoziuza na hata huduma wanazozitoa zote wanaweka na gharama za kodi zao na mpaka faida watakayoipata itatoka kwa hao hao walaji wa hizo bidhaa na huduma wanazozitoa kwa hao walaji wa mwisho !
Maajabu ya tafsiri ya walipa kodi iliyowekwa na wanaoitwa wataalamu wa masuala ya kodi ni kwamba Eti yule mfanyabiashara anayekusanya mauzo kutoka kwa walaji ambayo yameshawekwa na kodi zote kwenye hizo bidhaa na kwenye huduma zote anahesabika yeye ndiye mlipa kodi 😂😂😅 !
Haya kwangu ni maajabu 😱 !
Ndio walivyokaririshwa shule na ndio wanawashauri hivyo viongozi wetu. Aibu sana
 
Sio kweli direct tax & indirect tax inamgusa kwa asilimia kubwa kila mtanzania.Labda kama anazungumzia Direct tax tu
 
Sio kodi pekee hata wanaopiga kura na kura zao kuibiwa pia ni wengi.
 
Back
Top Bottom