Rais Samia: Wanaolipa kodi Tanzania ni milioni 2 tu

Rais Samia: Wanaolipa kodi Tanzania ni milioni 2 tu

Atuonyeshe mfano, kodi inalipwaje, yeye na ccm wenzie.
 
Apunguze matumizi serikalini!
SGR ipo, watumishi serikalini waitumie vyema tena waende na Economy class. Masafari yasioeleweka futa kule. Yeye naye ajimulike msafara wake ni kufuru!
Bado mianja ya udokozi ipo! Hela zinapigwa bila huruma!
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema wanaolipa kodi halisi Nchini ni Watu milioni mbili tu kati ya Watu milioni 65 ambapo amesema idadi hiyo ni ndogo sana hivyo amewataka Watanzania wengi zaidi walipe kodi ili kuchangia uchumi wa Taifa.

Rais Samia amesema hayo leo October 04,2024 Ikulu Jijini Dar es salaam wakati akiizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi.

“Kwa idadi yetu ya Watu, wanaolipa kodi halisi ni Watu wachache, ni Watu kama milioni mbili kati ya Watu milioni 65 sasa ukitoa Watoto na wengine ambao hawapaswi kukatwa kodi hatupungui labda milioni 37 ambao tunaweza kulipa kodi lakini wanaolipa kodi ni milioni mbili, sasa hii idadi ni ndogo, ni ndogo sana, ina maana Watu kidogo wanalipa kwa fursa ya kuwajenga Watu wengi hatuwezi kufika, lazima wote tuchangie kila Mtu kwa kiasi chake ili tuweze kufanya mengi.

Ubabe katika kukusanya Kodi
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema bado kuna malalamiko kutoka kwa Wafanyabiashara wanaolalamikia weledi kutozingatiwa wakati wa kukusanya kodi ikiwemo matumizi ya nguvu, lugha zisizo na staha na ubabe kwa baadhi ya Watumishi wa Serikali wanaohusika na utozaji kodi.

Akiongea leo October 04,2024 Ikulu Jijini Dar es salaam wakati akizindua Tume ya Rais ya Marekebisho ya Kodi, Rais Samia amesema “Baadhi ya Wafanyabiashara wanalalamikia wingi wa kodi na tozo lakini pia viwango vya kodi kutokuwa rafiki na hii ni kawaida, unajua Mtu ana hiyari kwenda kulipa faini bila kulazimishwa mwenyewe kwasababu faini ni kodi inayotokana na kosa, kwahiyo Mtu analipa ili asiende Jela lakini kodi tunayoizungumzia hapa ni kodi inayotokana na kitu kizuri”

“Sasa Mtu anaona nimefanya biashara nimepata pesa yangu kisha nikaipe Serikali bure lakini anasahau huduma inayotolewa na Serikali kwake na mazingira iliyomjengea kuweza kufanya biashara na kupata faida, kwahiyo ni maumbile ya Binadamu kuona kulipa kodi ni adhabu kumbe kulipa faini ni adhabu na Watu wanakwenda haraka, kwahiyo tuna tatizo ndani ya Nchi, Wafanyabiashara wanaamini hali hii inachangia mianya ya rushwa”

“Kuna malalamiko ya weledi kutozingatiwa wakati wa kukusanya kodi, mfano matumizi ya nguvu, lugha zisizo na staha na ubabe kwa baadhi ya Watumishi wa Serikali na baadhi ya biashara kutozwa kodi au tozo zinazoshabihiana na Taasisi zaidi ya moja kwahiyo hapa napo kuna mashakamashaka ambayo inatakiwa yakatazamwe”

PIA SOMA
- Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?
-Rais Samia: Uchumi wetu unakua lakini tunachokusanya, kingi kinaingia mifukoni kwa Wa
Mbona kuna ubabe kuzuia maandamano si atumie Jeshi la Polisi kufuatilia kodi.
 
Kila mtanzania anaelipia huduma analipa kodi lakini inaonekana haitoshi kwa sababu ya matumizi ya hovyo na anasa za waliopewa nafasi pamoja na wizi uliokithili ndio maana tra kila siku wanasema wamevunja rekodi ya ukusanyaji lakini kasi ya kukopa haipungui tuu
 
Njia pekee ya kuongeza tax base kwa kiasi kikubwa ni kupiga marufuku umachinga rasmi, kila mjasiriamali (mkubwa au mdogo) awe na business license na tax ID number
Magufuli ndo aliweka utaratibu wwnye akili af tukaona hafai tukamwondoa haraka
 
Huko tra kuna mambo ya kipuuzi Sana sometimes. Niliwahi fungua biashara na niliamua kua muaminifu kwa kulipa Kodi lakini Kodi niliyokadiliwa ni kubwa na inalingana na wafanyabiashara wenye mitaji mikubwa Sana Wakati Mimi nina mtaji wa milioni mbili tu.

Biashara ikafirisika nikaamua kufunga. Sasa ole wako ununue ardhi kwa mtu halafu unataka kufanya transfer nenda huko tra ukalipe kodi wanavyosumbua utadhani hawataki hiyo kodi
 
Nimeshindwa kumuelewa Rais anaposema nchi ina watu milioni 65 ila wanaolipa kodi ni watu milioni 2 tu!

Najiuliza sipati jibu!

Anataka WENDAWAZIMU, VICHAA, WASIO NA KAZI, WATOTO, VICHANGA walipe kodi!

Kwamba kila Mtanzania hata akizaliwa leo anatakiwa kulipa kodi1😅😅😅
Sijui anamaanisha kitu gani anaposema ni “Watu milioni 2 tu ndo wanaolipa kodi”

Je kwenye hao watu ni makampuni pamoja na biashara zote ambazo zimesajiliwa? Je ni pamoja na individual taxes?

Kauli hiyo iko vague kidogo kueleweka na wananchi wa kawaida.

Kwasababu kodi zenyewe ziko tofauti. Kuna “direct and indirect taxes” nk

Biashara zote zinatakiwa kuwa na leseni. Sasa wanashindwaje kujuwa kama siyo mfumo ambao umeweka mianya inayoleta udhaifu?

Hao anaowataka walipe kodi ni watu ambao wana biashara halafu hawalipi kodi?

Maana hii kauli yake kama ndo anavyoongea na Mwigulu Nchemba, siwezi kushangaa tozo zikaongezeka ili kuweza kupata “watu wengi zaidi wanaolipa kodi”

🤦🏾‍♂️
 
Kuna
1. Tax (Kodi)
2. Charges (Tozo)
3. Levy (Ushuru)

Watu hawalipi kodi kwasababu charges na levy ni nyingi sana sasa ukiongeza na kulipa kodi ni sawa hiyo kazi unaifanyia serikali na mwenye nyumba labda na maonesho kwamba unaamka asubuhi nawe una mahali unakwenda kushinda basi. Ndio maana watu wana opt wasilipe/wakwepe kodi.

Ushauri japo najua hauwezi fanyiwa kazi. Chagueni kufuta kodi zibaki charges and levy au zifutwe charges and levy ibaki kodi then boom 💥 muujiza makusanyo yataongezeka achana na maigizo ya sasa ya TRA.
Kodi ni nyingi mno. Binafsi kila mwezi nailipa serikali mamilioni mengi tu kutokana na huo utitiri wa kodi. Ndo maana sishangai kama mtu akitafuta upenyo wa kukwepa kodi.

Mfano hiyo service levy ni mauwaji.
 
Shida siyo kulipa kodi.shida ni kwamba hakuna uezeshwaji Kwa walipa Kodi Ili wakupe Kodi directly.asilimia kubwa ya wafanyabiasha hawalipi kodi au kulipisha kodi.watu wengi hawaoni umuhimu wa kulipa Kodi kwa sababu haoni faida ya kulipa Kodi kwa sababu haoni kama Serikali inamsaidiaje kukuza kipato Cha mlipa Kodi.
 
Nani anamwandikia Rais hizi Hotuba? Kweli anasema nchi nzima walipa kodi ni Milion 2 tu? Kweli? Au anamaanisha kuna watu wanaenda kwenye kadirisha flani wanalipa kodi wanapewa receipt wanarudi kwao?

Screenshot_2024-10-05-18-26-33-579_com.twitter.android~2.jpg
 
Registered tax payers, Walikuwa ml 4, wamepungua Hadi ml 2.

Hapo hapo TRA imekusanya Trillion 3 ndani ya miezi 3 ikidai imevunja rekodi zote za makusanyo.

Hili Giza nchini petu soon litapita na KUTAPAMBAZUKA!!

Naipenda sana Nchi yangu nzuri, tajiri TANZANIA 🇹🇿

Amen.
 
Nani anamwandikia Rais hizi Hotuba? Kweli anasema nchi nzima walipa kodi ni Milion 2 tu? Kweli? Au anamaanisha kuna watu wanaenda kwenye kadirisha flani wanalipa kodi wanapewa receipt wanarudi kwao?

View attachment 3116429
Rais ameongea utafiti, so inabidi akosolewe kwa tafiti sio kwa threads za JF. Leta utafiti wako wenye orodha ya walipa kodi zaidi ya milioni mbili.

Ova
 
Mbona yapo mazingira ambayo hayapo katika mfumo wa biashara lakini yametengenezwa system ya kodi?

Kwa hiyo zile buku jero za kila mwisho wa mwezi tunazokatwa kwenye Luku sio sehemu ya kodi?
 
Back
Top Bottom