John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akihutubia katika maadhimisho ya 'Siku ya Wanawake Duniani', Zanzibar, hivi ni baadhi ya kauli zake:
"Tunajua kwamba wanawake wengi wanajishughulisha na biashara ndogondogo ambazo hazipo kisheria na hazina kanuni, na sasa tunataka kwenda kurasimisha eneo hili ambayo ni sekta isiyo rasmi.
"Kama tulivyoagizwa na lengo namba nne katika malengo ya millenia kuhusu elimu, tumeendele kuhakikisha tunatoa fursa ya elimu ikiwemo kuwarudisha shuleni wale wote waliokatisha masomo.
"Tunakwenda kuweka mitaji kila mkoa, tumeshalifanyia kazi suala la mitaji na benki za CRDB na NMB zimekubali. Na huu mtaji sio mgao ni mkopo maalum kwa wanawake mbali na ile mikopo ya halmashauri.
"Wanawake walibeba mzigo mkubwa kipindi cha ugonjwa wa Uviko-19, kwani wengi waliambukizwa, waliuguza na hata wengine walipoteza uhai.
"Kama kweli suala la ukatili wa kijinsia linatukera sisi wanawake basi tutalifanyia kazi, Wanawake tutasimama imara kwa serikali zetu zote mbili zielewe kuq sulaa hili linatuudhi na tutaonesha njia.
"Tanzania na dunia kwa ujumla inakabaliwa na athari za mabadiliko ya tabia nchi, waathirika wakuu kabisa katika athari za mabadiliko ya tabia nchi ni wanawake.
"Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumefanya mabadiliko ya sera ya Mazingira mwaka jana na kuongeza suala la mabadiliko ya tabia nchi, mabadiliko ambayo hayakuwepo katika sera hiyo mwaka 2014.”
Source: DarMpya
"Tunajua kwamba wanawake wengi wanajishughulisha na biashara ndogondogo ambazo hazipo kisheria na hazina kanuni, na sasa tunataka kwenda kurasimisha eneo hili ambayo ni sekta isiyo rasmi.
"Kama tulivyoagizwa na lengo namba nne katika malengo ya millenia kuhusu elimu, tumeendele kuhakikisha tunatoa fursa ya elimu ikiwemo kuwarudisha shuleni wale wote waliokatisha masomo.
"Tunakwenda kuweka mitaji kila mkoa, tumeshalifanyia kazi suala la mitaji na benki za CRDB na NMB zimekubali. Na huu mtaji sio mgao ni mkopo maalum kwa wanawake mbali na ile mikopo ya halmashauri.
"Wanawake walibeba mzigo mkubwa kipindi cha ugonjwa wa Uviko-19, kwani wengi waliambukizwa, waliuguza na hata wengine walipoteza uhai.
"Kama kweli suala la ukatili wa kijinsia linatukera sisi wanawake basi tutalifanyia kazi, Wanawake tutasimama imara kwa serikali zetu zote mbili zielewe kuq sulaa hili linatuudhi na tutaonesha njia.
"Tanzania na dunia kwa ujumla inakabaliwa na athari za mabadiliko ya tabia nchi, waathirika wakuu kabisa katika athari za mabadiliko ya tabia nchi ni wanawake.
"Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumefanya mabadiliko ya sera ya Mazingira mwaka jana na kuongeza suala la mabadiliko ya tabia nchi, mabadiliko ambayo hayakuwepo katika sera hiyo mwaka 2014.”
Source: DarMpya