DOKEZO Rais Samia, Watumishi Wastaafu wa Jeshi tunaomba utusaidie kupata stahiki zetu, tunateseka

DOKEZO Rais Samia, Watumishi Wastaafu wa Jeshi tunaomba utusaidie kupata stahiki zetu, tunateseka

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kitaeleweka tu,baadhi ya watu wanajuaga mwanajeshi hasumbuliwi na kikokotoo... Kitaeleweka tu,mtaani kugumu sana,wajiwekezage.Hakuna vita siku hizi,vyakusema yawezekana nikafa muda wowote kwahiyo ninywe pombe na niwatumie wanawake tu,maana muda wowote naweza nikafa... hakuna hicho siku hizi,mtafanya kazi,mtastaafu,mje huku tuliko mkione cha moto.Jiwekezeni.
 
Kuna baadhi ya wastaafu wa kada za askari ukiona maisha wanayoishi utawahurumia , ni kama vile kazi waliyokuwa wanafanya iko na laana
 
Ni huzuni kwa kweli, watu wa vyeo vya chini wanatumika kukandamiza haki za wananchi na CCM, halafu wakistaafu wanaachwa kama takataka!
 
Kitaeleweka tu,baadhi ya watu wanajuaga mwanajeshi hasumbuliwi na kikokotoo... Kitaeleweka tu,mtaani kugumu sana,wajiwekezage.Hakuna vita siku hizi,vyakusema yawezekana nikafa muda wowote kwahiyo ninywe pombe na niwatumie wanawake tu,maana muda wowote naweza nikafa... hakuna hicho siku hizi,mtafanya kazi,mtastaafu,mje huku tuliko mkione cha moto.Jiwekezeni.
Wajiwekeze vip na wanadai haki yao..

Kwamba kutumikia taifa sio kujiwekeza?

Sasa mtu kafanya kazi miaka 30 anaambiwa alikuwa kibarua, wewe inakuingia akilini?

Unadhani Mwanajeshi wa kawaida anaweza jiwekeza kwenye nini cha kumpa fedha uzeeni?
Embu jaribu ku feel hiyo gap.
 
Madhara ya kuibeba CCM ndiyo haya,wananchi wakitakakufanya mabadiliko mnakuwa wa kwanza kujaza kura fake kwenye maboksi ya kupigia kura na kuwapiga wananchi kwa mabomu,matokeo yake wananchi wanalia na wabeba CCM nao wanaomboleza kivyao.
 
pindueni meza... hamtaki mnajiona nyie ndo mnafaidi mema ya nchi! angalia sasa mmetelekezwa!
 
Ni aibu kwa askari kuilalamikia serikali ambayo pasipo ninyi haiwezi kuwa hapo.

Sisi raia tumedhuliwa sana, tuna hela zetu LAPF na NSSF na hatuwezi kuzitoa
 
Acha mlie tu na Saa 100 asiwasaidie lolote. Miaka yote mmewalinda watesi wetu, wadhulumu wetu, wezi wa kura ili wabaki madarakani. Sasa yamewatokea puani mnalalamika. Mliapa kulinda katiba ya JMT, mmewahi kusimamia hilo?
Baba zetu walikua watumishi pia na wamestaaf na hela kiduchu kutokana na sera mbovu za CCM ambayo nyie masikini wenzetu mlikua mkiwalinda na kututisha.
Au mmesahau Mkapa alivyowapeleka wajeda kule Unguja na Pemba?
Mmesahau.
 
➤ Sisi ni Watumishi wa Umma Wastaafu tuliokuwa tunafanyia kazi vikosi mbalimbali vya Jeshi, tuliajiriwa kila mtu na CV namba yake na kila mtu alipewa barua ya kuajiriwa pia kila Mwajiriwa alikuwa na C/NO yake ya kupatia Mshahara kutoka Hazina (Pay Slip tunazo).

➤ Tukiwa katika ajira tulikuwa tunapandishwa Vyeo na pia tukapewa barua za kuthibitishwa kazini.

➤ Pamoja na hayo tulifanya kazi katika mazingira magumu, miaka ya mwanzo tulipoanza kazi tulikuwa tunapewa ‘unform’, Viatu na Pesa na Likizo.

➤ Kuanzia Miaka ya 1998 mambo yakabadilika tukawa hatupewi tena, ikawa inapita hadi miaka mitatu au minne ndio mnapewa tena ya mwaka mmoja.

➤ Kabla ya kustaafu tuliandika barua kuomba tupatiwe haki hizo lakini mpaka leo (Agosti 11, 2023) hatujajibiwa.

Baadhi yetu tulikuwa katika Mifuko ya NPF, tukahamishiwa NSSF baadaye tukahamishiwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

➤ Mfano kuna Mtumishi ambaye ametumikia miezi 495 lakini kwenye malipo akapewa miezi 272, kisha miezi 223 iliyosalia haijulikani malipo yake yamepotelea wapi, hata alipouliza hakupata majibu ya kueleweka zaidi ya kuambiwa amuulize Mwajiri wake.

➤ Muda wa Kustaafu ulipofika tukawekwa kwenye kikokotoo, pesa tulizojiwekea kwenye Mifuko ya Hifadhi tukakuta zimekatwa, tukapewa nusu ya kile kilichokuwa tumechangia.

➤ Tulipohoji mbona pesa zetu zimekatwa tukajibiwa kuwa ‘ndizo mtakazo kuwa mnalipwa kwa mwezi’. Yote tumevumilia lakini maisha yanazidi kuwa magumu.

➤ Wakati tumelipwa malipo pungufu kutoka katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pia malipo ya Kiinua Mgongo hatujapata kabisa, tulipouliza tukaambiwa hatutapewa, tulipohoji tukaambiwa ni maelekezo kutoka juu, kwamba hatutakiwi kulipwa na Hazina.

➤ Tumeenda kwa Afisa Utumishi ili atuandalie malipo ya Kiinua Mgongo tukaambiwa hatupaswi kulipwa kiinua mgongo kwa kuwa sisi ni vibarua.

➤ Tunapatwa na mshangao wa majibu hayo, tukamuuliza Afisa Utumishi wetu kuwa ‘mbona tulikuwa tunapanda vyeo na Pay Slip tunazo’, akatujibu ‘tusihangaike hii ndio amri imetolewa’.

➤ Cha kushangaza waliopewa barua za kutokulipwa ni wachache zinazoonyesha hawastahili kulipwa Kiinua Mgongo, tukahoji mbona wengine hawajapewa hizo barua, wala hatujajulishwa, tulijibiwa tufuate barua walizotumiwa wenzetu.

➤ Tumebaki na mshangao wala hatujui hatima yetu.

➤ Tumefanya jitihada nyingi za kukutana na Waziri wa Ulinzi kupitia wasaidizi wake lakini imeshindikana.

➤ Tulipotaka kulalamika kwenye Vyombo vya Habari, wakasema masuala yetu hayatolewi kwenye Vyombo vya Habari.

➤ Aprili 2023 tulikutana na Mbunge mmoja, akaahidi kutusaidia kutukutanisha na Waziri wa Ulinzi lakini tangu wakati huo mchakato haujafanikiwa, tukijulishwa kuwa ratiba za Waziri zinambana.

➤ Wastaafu tuko wengi kuanzia wa Mwaka 2019.

➤ Wastaafu wenzetu wa miaka ya nyuma walilipwa vizuri kwenye Mifuko ya Hifadhi na kiinua mgongo wakapewa, leo sisi tunaambiwa vibarua Je? Kibarua anapata mshahara wa Hazina na anapandishwa cheo na kuthibitishwa kazini?

➤ Tunapewa majibu ya mdomo, kinachoumiza zaidi ni kuwa wakati wa kuajiriwa tulipewa barua, leo tunajibiwa mdomoni tu kwamba sisi ni vibarua, ukiuliza zaidi wanasema kuna wenzetu wachache wametumiwa barua, hivyo wengine wote tufuate kile kilichoandikwa katika barua za wenzetu wachache, hii si sawa.

➤ Tunaomba huruma yako kuna Watumishi wa Umma waliumwa maradhi mbalimbali wakiwa kazini mfano, TB, HIV na Corona hawakulipwa chochote na muda wa kustaafu umefika walivumilia yote hayo walijua watafika mwisho wa ajira yao watalipwa, leo wanaambiwa hawapaswi kulipwa kiinua mgongo je, hii ni haki?

➤ Mheshimiwa Rais, kwa nafasi yako tunaomba utusaidie; maisha yetu sasa yamekuwa magumu kwa mtihani huu tulioupata.
Hivi hawa wazee walipata stahiki zao?
 
➤ Sisi ni Watumishi wa Umma Wastaafu tuliokuwa tunafanyia kazi vikosi mbalimbali vya Jeshi, tuliajiriwa kila mtu na CV namba yake na kila mtu alipewa barua ya kuajiriwa pia kila Mwajiriwa alikuwa na C/NO yake ya kupatia Mshahara kutoka Hazina (Pay Slip tunazo).

➤ Tukiwa katika ajira tulikuwa tunapandishwa Vyeo na pia tukapewa barua za kuthibitishwa kazini.

➤ Pamoja na hayo tulifanya kazi katika mazingira magumu, miaka ya mwanzo tulipoanza kazi tulikuwa tunapewa ‘unform’, Viatu na Pesa na Likizo.

➤ Kuanzia Miaka ya 1998 mambo yakabadilika tukawa hatupewi tena, ikawa inapita hadi miaka mitatu au minne ndio mnapewa tena ya mwaka mmoja.

➤ Kabla ya kustaafu tuliandika barua kuomba tupatiwe haki hizo lakini mpaka leo (Agosti 11, 2023) hatujajibiwa.

Baadhi yetu tulikuwa katika Mifuko ya NPF, tukahamishiwa NSSF baadaye tukahamishiwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

➤ Mfano kuna Mtumishi ambaye ametumikia miezi 495 lakini kwenye malipo akapewa miezi 272, kisha miezi 223 iliyosalia haijulikani malipo yake yamepotelea wapi, hata alipouliza hakupata majibu ya kueleweka zaidi ya kuambiwa amuulize Mwajiri wake.

➤ Muda wa Kustaafu ulipofika tukawekwa kwenye kikokotoo, pesa tulizojiwekea kwenye Mifuko ya Hifadhi tukakuta zimekatwa, tukapewa nusu ya kile kilichokuwa tumechangia.

➤ Tulipohoji mbona pesa zetu zimekatwa tukajibiwa kuwa ‘ndizo mtakazo kuwa mnalipwa kwa mwezi’. Yote tumevumilia lakini maisha yanazidi kuwa magumu.

➤ Wakati tumelipwa malipo pungufu kutoka katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pia malipo ya Kiinua Mgongo hatujapata kabisa, tulipouliza tukaambiwa hatutapewa, tulipohoji tukaambiwa ni maelekezo kutoka juu, kwamba hatutakiwi kulipwa na Hazina.

➤ Tumeenda kwa Afisa Utumishi ili atuandalie malipo ya Kiinua Mgongo tukaambiwa hatupaswi kulipwa kiinua mgongo kwa kuwa sisi ni vibarua.

➤ Tunapatwa na mshangao wa majibu hayo, tukamuuliza Afisa Utumishi wetu kuwa ‘mbona tulikuwa tunapanda vyeo na Pay Slip tunazo’, akatujibu ‘tusihangaike hii ndio amri imetolewa’.

➤ Cha kushangaza waliopewa barua za kutokulipwa ni wachache zinazoonyesha hawastahili kulipwa Kiinua Mgongo, tukahoji mbona wengine hawajapewa hizo barua, wala hatujajulishwa, tulijibiwa tufuate barua walizotumiwa wenzetu.

➤ Tumebaki na mshangao wala hatujui hatima yetu.

➤ Tumefanya jitihada nyingi za kukutana na Waziri wa Ulinzi kupitia wasaidizi wake lakini imeshindikana.

➤ Tulipotaka kulalamika kwenye Vyombo vya Habari, wakasema masuala yetu hayatolewi kwenye Vyombo vya Habari.

➤ Aprili 2023 tulikutana na Mbunge mmoja, akaahidi kutusaidia kutukutanisha na Waziri wa Ulinzi lakini tangu wakati huo mchakato haujafanikiwa, tukijulishwa kuwa ratiba za Waziri zinambana.

➤ Wastaafu tuko wengi kuanzia wa Mwaka 2019.

➤ Wastaafu wenzetu wa miaka ya nyuma walilipwa vizuri kwenye Mifuko ya Hifadhi na kiinua mgongo wakapewa, leo sisi tunaambiwa vibarua Je? Kibarua anapata mshahara wa Hazina na anapandishwa cheo na kuthibitishwa kazini?

➤ Tunapewa majibu ya mdomo, kinachoumiza zaidi ni kuwa wakati wa kuajiriwa tulipewa barua, leo tunajibiwa mdomoni tu kwamba sisi ni vibarua, ukiuliza zaidi wanasema kuna wenzetu wachache wametumiwa barua, hivyo wengine wote tufuate kile kilichoandikwa katika barua za wenzetu wachache, hii si sawa.

➤ Tunaomba huruma yako kuna Watumishi wa Umma waliumwa maradhi mbalimbali wakiwa kazini mfano, TB, HIV na Corona hawakulipwa chochote na muda wa kustaafu umefika walivumilia yote hayo walijua watafika mwisho wa ajira yao watalipwa, leo wanaambiwa hawapaswi kulipwa kiinua mgongo je, hii ni haki?

➤ Mheshimiwa Rais, kwa nafasi yako tunaomba utusaidie; maisha yetu sasa yamekuwa magumu kwa mtihani huu tulioupata.
f4ab6b0ba6f3b27a65a2e9723d496945.png

Yaani mimi ndiyo JK WA JAMII FORUMS - "Moderator weka mambo hapo" 😂
 
Nakaaga najiuliza Waalimu na wanausalama wao ndio hua msaada mkubwa sana kipindi cha uchaguzi ila cha ajabu wao ndio wanasahaulika😂😂😂 au ndio yale yasemwayo malipo ni hapa hapa duniani. Imagine mtu anaomba hakinyake aliyowekeza kwa muda wote aliofanya kazi na anapangiwa apateje stahiki yake. Muda mwingine afe hajapata na watoto zake wasiipate. Wanajeshi mkiona hamsikilizwi kuomba ni unyonge nadhani mnajua nn cha kufanya.
 
➤ Sisi ni Watumishi wa Umma Wastaafu tuliokuwa tunafanyia kazi vikosi mbalimbali vya Jeshi, tuliajiriwa kila mtu na CV namba yake na kila mtu alipewa barua ya kuajiriwa pia kila Mwajiriwa alikuwa na C/NO yake ya kupatia Mshahara kutoka Hazina (Pay Slip tunazo).

➤ Tukiwa katika ajira tulikuwa tunapandishwa Vyeo na pia tukapewa barua za kuthibitishwa kazini.

➤ Pamoja na hayo tulifanya kazi katika mazingira magumu, miaka ya mwanzo tulipoanza kazi tulikuwa tunapewa ‘unform’, Viatu na Pesa na Likizo.

➤ Kuanzia Miaka ya 1998 mambo yakabadilika tukawa hatupewi tena, ikawa inapita hadi miaka mitatu au minne ndio mnapewa tena ya mwaka mmoja.

➤ Kabla ya kustaafu tuliandika barua kuomba tupatiwe haki hizo lakini mpaka leo (Agosti 11, 2023) hatujajibiwa.

Baadhi yetu tulikuwa katika Mifuko ya NPF, tukahamishiwa NSSF baadaye tukahamishiwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

➤ Mfano kuna Mtumishi ambaye ametumikia miezi 495 lakini kwenye malipo akapewa miezi 272, kisha miezi 223 iliyosalia haijulikani malipo yake yamepotelea wapi, hata alipouliza hakupata majibu ya kueleweka zaidi ya kuambiwa amuulize Mwajiri wake.

➤ Muda wa Kustaafu ulipofika tukawekwa kwenye kikokotoo, pesa tulizojiwekea kwenye Mifuko ya Hifadhi tukakuta zimekatwa, tukapewa nusu ya kile kilichokuwa tumechangia.

➤ Tulipohoji mbona pesa zetu zimekatwa tukajibiwa kuwa ‘ndizo mtakazo kuwa mnalipwa kwa mwezi’. Yote tumevumilia lakini maisha yanazidi kuwa magumu.

➤ Wakati tumelipwa malipo pungufu kutoka katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pia malipo ya Kiinua Mgongo hatujapata kabisa, tulipouliza tukaambiwa hatutapewa, tulipohoji tukaambiwa ni maelekezo kutoka juu, kwamba hatutakiwi kulipwa na Hazina.

➤ Tumeenda kwa Afisa Utumishi ili atuandalie malipo ya Kiinua Mgongo tukaambiwa hatupaswi kulipwa kiinua mgongo kwa kuwa sisi ni vibarua.

➤ Tunapatwa na mshangao wa majibu hayo, tukamuuliza Afisa Utumishi wetu kuwa ‘mbona tulikuwa tunapanda vyeo na Pay Slip tunazo’, akatujibu ‘tusihangaike hii ndio amri imetolewa’.

➤ Cha kushangaza waliopewa barua za kutokulipwa ni wachache zinazoonyesha hawastahili kulipwa Kiinua Mgongo, tukahoji mbona wengine hawajapewa hizo barua, wala hatujajulishwa, tulijibiwa tufuate barua walizotumiwa wenzetu.

➤ Tumebaki na mshangao wala hatujui hatima yetu.

➤ Tumefanya jitihada nyingi za kukutana na Waziri wa Ulinzi kupitia wasaidizi wake lakini imeshindikana.

➤ Tulipotaka kulalamika kwenye Vyombo vya Habari, wakasema masuala yetu hayatolewi kwenye Vyombo vya Habari.

➤ Aprili 2023 tulikutana na Mbunge mmoja, akaahidi kutusaidia kutukutanisha na Waziri wa Ulinzi lakini tangu wakati huo mchakato haujafanikiwa, tukijulishwa kuwa ratiba za Waziri zinambana.

➤ Wastaafu tuko wengi kuanzia wa Mwaka 2019.

➤ Wastaafu wenzetu wa miaka ya nyuma walilipwa vizuri kwenye Mifuko ya Hifadhi na kiinua mgongo wakapewa, leo sisi tunaambiwa vibarua Je? Kibarua anapata mshahara wa Hazina na anapandishwa cheo na kuthibitishwa kazini?

➤ Tunapewa majibu ya mdomo, kinachoumiza zaidi ni kuwa wakati wa kuajiriwa tulipewa barua, leo tunajibiwa mdomoni tu kwamba sisi ni vibarua, ukiuliza zaidi wanasema kuna wenzetu wachache wametumiwa barua, hivyo wengine wote tufuate kile kilichoandikwa katika barua za wenzetu wachache, hii si sawa.

➤ Tunaomba huruma yako kuna Watumishi wa Umma waliumwa maradhi mbalimbali wakiwa kazini mfano, TB, HIV na Corona hawakulipwa chochote na muda wa kustaafu umefika walivumilia yote hayo walijua watafika mwisho wa ajira yao watalipwa, leo wanaambiwa hawapaswi kulipwa kiinua mgongo je, hii ni haki?

➤ Mheshimiwa Rais, kwa nafasi yako tunaomba utusaidie; maisha yetu sasa yamekuwa magumu kwa mtihani huu tulioupata.
Wasaidiwe
 
Wanatakiwa kuchukua hatua nao tuko nao tunalalamika?

Kwisha habari yetu. Nyie Makamanda wastaafu hata sitawapa pole kuleni za uso tu
 
Back
Top Bottom