Rais Uhuru atoa amri kila aliyetajwa kwenye ufisadi ang'atuke madarakani

Rais Uhuru atoa amri kila aliyetajwa kwenye ufisadi ang'atuke madarakani

naiona serikali nzuri inayowajibika kwa raia wake huko kenya. ewe Mungu tusaidie na sisi tuwe na serikali inayowajibika kwetu.
 
Habari za jamvini wanajamvi?

Kwa wale waliofatilia habari mbalimbali mitandaoni nadhani wameona habari kuhusu rais wa Kenya Mh. Uhuru Kenyatta kusimamisha kazi watumishi wa umma wapatao 175 kwa tuhuma za ufisadi na kati ya hao wamo Mawaziri 5, makatibu 6 wa kudumu na Magavana 10 wametajwa.

Lakini mh. Kenyatta alisema ''Ufisadi umevuka mipaka na lazima nasi tujifunge kibwebwe na kukabiliana nao''.''Natarajia kuwa wale waliotajwa katika ripoti hii watanga'tuka mamlakani hadi pale uchunguzi utakapokamilishwa ndipo warejee afisini.'' alisema Kenyatta.

Kenyatta aliongezea kusema kuwa ''Ninamtaka kiongozi wa mashtaka ya umma kuanzisha uchunguzi mara moja kuhusiana visa vyote vilivyotajwa humu katika kipindi cha siku 60 zijazo''.

Pia alisikitishwa na uwepo wa kamati ya bunge inayoshughulikia ufisadi kuwepo katika ripoti hiyo kama wahusika wa ufisadi.

MY TAKE
Kama kaka nae angeweza kua na ujasiri wa mdogo wake jirani basi kina vijisenti na vihela vya mboga wasingeshamiri.

Wewe sio mtanzania , tunakufaham unaishi kibera slum , kama unabisha sema tukuumbue wewe mkikuyu
 
Kazaneni maana hawandio wahujum uchumi na maendeleo
 
Ili kuweza kuthubutu kuwapiga chini watumishi 175 kwa mpigo wakiwemo mawaziri na magavana, inabidi uwe na "moral authority" ya kufanya hivyo. Kama wewe sio msafi huwezi kuwa na ubavu wa kukemea ufisadi. Huyu wa kwetu anakosa moral authority ya kukemea ufisadi kwani na yeye ni sehemu ya huo mchezo. Nani asiyejua kwamba jamaa yetu aliingia magogoni kwa pesa za wizi kutoka benki kuu EPA? Sasa katika mazingira kama haya anapata wapi ubavu wa kukemea mafisadi?

Sikumbuki hata siku moja kumsikia anakemea ufisadi achilia mbali kufukuza watumishi wa umma kazi kwa tuhuma za ufisadi.

Hongera Uhuru Kenyatta kwa kuthubutu.

Tiba
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wewe sio mtanzania , tunakufaham unaishi kibera slum , kama unabisha sema tukuumbue wewe mkikuyu

Angalia mantiki ya Uzi sio mleta mada! Awe anaishi kibera au awe mkamba, ukweli upo pale pale, UK kafanya la maana na JK Hana ubavu huo!
 
Mimi nilisoma sehemu ,kasema wakar pembeni,uchunguzi ufanyike.
mbona wale wa chicken gate sijui nini amegoma kuwaadhibu,wakati ushahidi upo from UK,na waliotoa rushwa washafungwa?
wapo wale wa tume ya uchaguzi nao bado wanadunda mtaani mbona hata hatua stahiki hazijachukuliwa?
juzi juzi hapa nilisoma sehem ODINGA aliwashauri bure kwamba wakitaka serikali yao ifike 2017 basi wa deal na mambo ya rushwa.
kesho yake Ruto akamjibu utumbo baba wa watu,Leo Uhuru anawambia wakae pembeni uchunguzi ufanyike,hahaha kumbe Yale maneno ya odinga yalikuwa ya kweli eeeehh!!!??
hapo Uhuru Ana fight corruption kupitia makaratasi,cheap PR lakin hatua hazita chukuliwa,bora huyu wetu yeye alishaziba masikio yake na pamba na kuruhusu watu wapige wawezavyo.
 
I agree...no doubts...Mwigulu anaweza hili...!!

Ila USIMSAHAU LOWASSA ndio kazi zake...harembi...ukila cha UMMA...anazaa na ww...!!

Lowassa hacheki na wezi ya mali ya umma...!!

wao walizaa nae kwenye Richmond na mpaka sasa bado analea!
 
Hatimaye Rais Kenyatta akunjua makucha yake, safi sana. Hongera zao... huku kwetu wimbo ni sio za umma
 
JK; my president; take a leaf from UK's work book, your legacy is at stake!!
====================


Source:nation

There is nothing positive to learn there. Some of the accused are within his constitutional power to handle. Why not simply fire them? Why ask them to step aside instead of firing them?
I can only understand the case of County Governors. He can not fire them. It seems Uhuru Kenyatta has the same weakness as Jakaya Kikwete.
 
  • Thanks
Reactions: MTK
yani kuna mijitu mijinga saana maana wanaboa.mimi nimezungumzia jinsi nilivyopokea habari cha kushangaza mtu anaongelea habari za kibera... kwani mkenya kwenye jf ni shida?kama mwanadamu na mpenzi wa sera za usawa na maisha bora swala hili hata angefanya Piere Nkurunzinza still ngempongeza.Kwahiyo wewe Baro learn to respect people's ideas and if you are good on criticizing then pose a hot and sensible standing fact within the thread.mijitu kama hii ndo inakurupukaga kwa usahili ikikosa inalalamika wamemnyima kazi...
 
Huyo UK ni CRIMINAL hana nguvu ya kumuwajibisha yeyote serikalini kwa mujibu wa katiba ya Kenya hana mamlaka ya kumfukuza Gavana, Mbunge labda Mawaziri (tena baada ya Bunge kuridhia). Si rahisi hao 175 officials kama anavyodai NI NGUMU.
 
Council of Govenors wamepinga kwa sababu wao wamechaguliwa kikatiba na wanatakiwa waondoke kikatiba.
 
Kwetu itaondoka serikali nzima

in reality so should all the MPs, the senators and some of the cabinet secretaries in the kenyan govt.

a few of the cabinet secretaries are clean because they came straight from the private sector to the public sector but some are knee deep in corruption scandals
 
Ningeishi kama inavyoishi serikali yangu.....ningekuwa jela kitambo sana
 
Back
Top Bottom