mzeewaSHY
JF-Expert Member
- Aug 31, 2021
- 8,916
- 8,630
Hata wa upande wa pili nao ni vivyo hivyo wanataka vyeo ndio maana wako kwenye siasa !!Watu wanataka wapate vyeo kwa sababu ajira Yao ni siasa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata wa upande wa pili nao ni vivyo hivyo wanataka vyeo ndio maana wako kwenye siasa !!Watu wanataka wapate vyeo kwa sababu ajira Yao ni siasa
Hoja nzito kabisa hiiMi niko na wewe. Sijaona shida ya katiba iliyopo zaidi ya shida ya wananchi wenyewe. Ni kupitia Katiba hii mimi wa Nakapanya naweza kwenda Ngara na kuoa, na kupewa Shamba bure na kulima na kufanya maisha na mtoto wangu akaamua kwenda kuishi chakechake peacefully. Nadhani kama nchi tatizo letu sio katiba bali malezi kuanzia ngazi ya familia, unless niambiwe katiba mpya itasaidiaje kuwafanya wahadzabe wasiishi naporini.
Ni kweli kabisa na hii ni kwa sababu walioloshika buyu la Asali hawataki kuwaachia na wenzao nao walambe japo nao ni Watanzania wenzao !! Hiyo ndio shida kuu !!Ndio lengo lao
Hata wewe inaonekana unahitaji elimu ya kujua kwamba katiba sio chanzo Cha umaskini wetu Bali uvivuWazo lako ni sawa na wakulima wanataka kuwekewa mfumo wa Kunywesha mashamba yao wanakataa kwa kusema wasikilizwe kwani Mvua ya Mungu inatosha...
Ninachotaka kusema ni kuwa, rudi darasani au fanya utafiti kujua kwa nini watu wanataka katiba mpya; ukishapata hojazao; utanielewa ninachokisema!
Asante sana mkuu elimu hii inatakiwa tuitoe wananchi wanapelekwa pelekwa TUTatizo la wanasiasa haswa vyama vya upinzani wanadhani kuwepo kwa katiba mpya kutawawezesha washike dola!!!!!
Mimi nasema fikra hizo ni za kipuuzi!
Mfano angalia nchi JIRANI ya Kenya pamoja na kuwa na katiba mpya nzuri lakini kila Uchaguzi Raila analia hakubali matokeo na hakubali maamuzi ya mahakama!!!!
Kwa maana hiyo ni wazi kuwa katiba mpya sio "mwarobaini"
Kwa mtizamo wangu, maadili/uadilifu ndio jambo la msingi ambao hauletwi na katiba mpya bali unajengwa kwa kizazi na kizazi.
Uadilifu na maadili mazuri ya viongozi wetu wote walio pita kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa awamu ya sita ni kutokana na uadilifu wa viongozi wetu, wamejengwa na kulelewa kwenye misingi ya maadili na uadilifu.
Mkuu naungana na ww wanaopigania katiba walio wengi ni wanasiasa na wafuasi wao,Katiba ina mambo Mengi sana inayazungumzia...ila watu kama chadema kwenye itaji lao la katiba mpya wanataka kipengele tu cha TUME HURU YA UCHAGUZI.Hakuna kinachopiganiwa hapo zaidi ya maslahi ya wanasiasa
Hata wa upande wa pili wanaing’ang’ania hii katiba ili waendelee kushika dola !!! Ukweli hutuweka huru wajameni 😂🙏Tatizo la wanasiasa haswa vyama vya upinzani wanadhani kuwepo kwa katiba mpya kutawawezesha washike dola!!!!!
Mimi nasema fikra hizo ni za kipuuzi!
Mfano angalia nchi JIRANI ya Kenya pamoja na kuwa na katiba mpya nzuri lakini kila Uchaguzi Raila analia hakubali matokeo na hakubali maamuzi ya mahakama!!!!
Kwa maana hiyo ni wazi kuwa katiba mpya sio "mwarobaini"
Kwa mtizamo wangu, maadili/uadilifu ndio jambo la msingi ambao hauletwi na katiba mpya bali unajengwa kwa kizazi na kizazi.
Uadilifu na maadili mazuri ya viongozi wetu wote walio pita kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa awamu ya sita ni kutokana na uadilifu wa viongozi wetu, wamejengwa na kulelewa kwenye misingi ya maadili na uadilifu.
Duh...!. Mkuu Mganguzi , kwanza nikupongeze kwa bandiko hili na kuheshimu uhuru wa maoni na uhuru wa kijieleza, yaani freedom of expression and freedom of speech.
Dunia ilipoumbwa, hakuna aliyejua dunia ni duara, watu wote kwa kutokujua kwao wakajua umbo la dunia ni umbo bapa.
Galileo Galilee alipogundua telescope na kuliona umbo la dunia kupitia kivuli cha kwenye mwezi, alipotangaza kuwa dunia ni duara, Galileo Galilee aliuwawa kwa kosa la kumkufuru Mungu kwa kitendo chake cha kusema dunia ni duara!.
Ukiwa hujaonja embe dodo ukiambiwa tunda tamu kuliko yote ni pera utaamini mpaka utakapoonja embe dodo ndio utagundua kumbe tunda tamu ni embe dodo.
Ukionja zabibu unagundua ni zabibu, ukionja nanasi unagundua ni nanasi, ukionja tende unagundua ni tende, ukionja asali ndipo utagundua asali ndio funga kazi ya utamu!.
Wewe ni mmoja wa Watanzania wasiojua katiba wala Umuhimu wa katiba mpya, hivyo wameridhika sana na hii katiba pera iliyopo, bila kuonjeshwa katiba embe, katiba nanasi, katiba tende na katiba asali, kamwe hauwezi kujua Umuhimu wa katiba mpya.
Hili la Watanzania kutujua katiba, hata Rais Samia amelisema
Hivyo watu kama akina sisi tuliobahatika kajiuwezo ka kusoma sheria na kuijua katiba, tumejitolea kuwaelimisha wengine Umuhimu wa katiba mpya kwanza kwa kuwaelimisha Watanzania wenzetu elimu ya katiba ili waifahamu katiba.
Angalia bandiko hili elimishi kuhusu kuijua katiba ni la lini na limechangiwa na watu wangapi ili kupata picha ya Watanzania wanavyotaka kuijua katiba Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio ila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?
Just imagine mtu unajitolea kuelimisha umma kuhusu katiba halafu responses ndio hii!, utaendelea kweli?.
Hivyo watu kama nyinyi mnapojitokeza kusema hamuhitaji katiba mpya, hatuwashangai bali tunawahurumia!.
Laiti ungelijua tungekuwa na katiba bora, Tanzania tungekuwa wapi, ndipo ungeweza kujua tofauti ya utamu wa pera na asali!.
Kama una muda karibu pande hizi
P
- Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?
- Mchakato huu wa Katiba ni umasikini wetu. Tujikubali, tuukubali, tuupigie kura ya ndio
- Je Wajua Kuwa Kura ya "Hapana" Kwa Katiba Mpya! Ni Kura ya "Ndiyo!" Kwa Katiba Hii Iliyopo?
- Bora Katiba tuikubali, tusiichukie CCM kwa sababu CCM itahukumiwa na Karma kwa Uovu wake
- Pascal Mayalla: CHADEMA watengeneze kwanza Katiba mpya ya chama chao kabla ya kukimbilia katiba ya nchi, wawatendee haki wabunge 19
- Mungu asingemchukua yule Mwamba, ilikuwa atuachie katiba mpya Trends, Visions: Watanzania msitatizwe na kauli zake kuhusu Katiba, baada ya Nyerere, ni Magufuli ndiye ataacha legacy kubwa ikiwemo Katiba Mpya!.
- Sasa Mama atatuletea katiba mpya ila ni 2025 -2030, ila sisi washauri wa bure tumemshauri Hongera Sana Rais Samia kwa Miaka Miwili Madarakani. Japo Umefanya Mengi, Makubwa, Mazuri, Lakini Bado! Linalowezekana Leo, Lisingoje Kesho!
Ndio tumeanza Sasa tunaratibu Mikutano tutatembea nchi kuwaambia wananchi katiba mpya haifai
Katiba iliyopo mpaka hatujaona madhara yake Bali amani yetu imekuwa tunu katiba hii Ingekuwa mbaya tusingefika hapa
Anaogopa kutumbuliwa na kushitakiwa kwa sababu ya ufisadi waliofanya yeye na Magufuri.Vurugu ipi? Mbona umekazania vurugu unaogopa Nini?
Kuhusu Muundo wa Serikali ya Muungano,Kinga za Viongozi wa Serikali,Ajira,Elimu na mambo mengine.Tupo wengi sana. Hata kwa wanaotaka wengi wao ni kufuata mkumbo tu lakini hakuna hoja za msingi za kutaka katiba mpya zaidi ya madaraka ya Rais ambayo yanaweza kurekebishwa bila kuandika katiba mpya.
Wewe bila shaka ni Mwigulu NchembaNaunga mkono Hoja kwa asilimia 100 .Watanzania hatuna haja ya Katiba Mpya .Katiba ya Mwaka 1977 ni Msingi Imara wa Taifa letu. Mambo yote ambayo tumeyafanikisha kama Taifa au Watu binafsi yametokana na Katiba hii.
Wanatokea baadhi ya Watanzania wenzetu kwa maslai ambayo hayako wazi , ovu,potofu na hatarishi wanataka Katiba hii ibadishwe.Kumbukeni mkibadirisha Katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 huo ndio utakuwa Mwisho wa utambulisho wa Mtanzania.
Acheni kufanya majaribio kwenye eneo lisilohitaji majaribio hata kidogo.
Matatizo mlio nayo au matatizo tuliyonayo kama Nchi kisiasa,kiuchumi,kiteknojia,kibailojia, kiutamaduni,kitibabu etc hayawezi kutatuliwa kwa kubadilisha Katiba.
Mkifanikisha hili mtakuja na hoja ya kubadilisha VITABU VYA DINI ili kuendana na matakwa yenu.
Yangu Maoni ni hayo kwa ajili ya rejea mbeleni.
ARTICLE.
Poor governance na uwajibikaji hafifu wewe unakuja kuongelea mambo ya usalama?!!Nchi Iko sehemu salama kabisa chini ya katiba hii iliyopo
Ohoo. !!Wewe bila shaka ni Mwigulu Nchemba