Rais umewasikiliza wanaotaka katiba mpya! Je, sisi tusiotaka katiba mpya utatusikiliza lini? Tuna hoja!

Rais umewasikiliza wanaotaka katiba mpya! Je, sisi tusiotaka katiba mpya utatusikiliza lini? Tuna hoja!

Asalaam ndugu zangu ..nianze Kumpongeza rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya .. wamesikilizwa na ninasikia mchakato karibia utaanza ni jambo jema ... Lakini tupo sisi ambao hatukubaliani na mchakato huo .. hatuhitaji katiba mpya na tuna hoja na sababu za msingi ..nchi yetu imekuwa na amani kwa miaka zaidi ya 50 kwa katiba hii .. nchi yetu imekuwa na uchumi unaokuwa vizuri kwa katiba hii ... Kwa sisi tusiotaka katiba utatusikiliza lini ? Na sisi tuna haki ya kusikilizwa kama ulivyowasikiliza hao wanaotaka katiba mpya !! Mimi na wenzangu wengi TU tusiotaka katiba mpya tutasikilizwa lini ? Hatutaki kabisa katiba mpya !! Tumeona nchi jirani zilizokimbilia katiba mpya kwa minajiri ya ustawi kisiasa na maisha ya watu wetu lakini imekuwa kinyume chake! Kenya vurugu tupu! Afrika kusini vurugu tupu !! Nchi zote zilizothubutu kubadilisha katiba ziliingia kwenye migogoro isiyoisha .. please rais hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu ..asanteni
..
 
Rais haleti katiba mpya, anawezesha tu mchakato wa maamuzi wa hiyo katiba.

Kwa hiyo katiba mpya itapendekezwa, kura zitapigwa. Nyie msioitaka hiyo mpya mtapiga kura za maoni na wale wanaoitaka hiyo mpya watapiga kura zao. Upande utakaopata kura nyingi ndio utakuwa mshindi.

Kwa hiyo kwa sasa hata nyie msioitaka katiba mpya, mnatakiwa pia muungane kudai wananchi kupewa uwezo wa kujiamulia aina ya katiba wanayoitaka karne hii.
Asalaam ndugu zangu ..nianze Kumpongeza rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya .. wamesikilizwa na ninasikia mchakato karibia utaanza ni jambo jema ... Lakini tupo sisi ambao hatukubaliani na mchakato huo .. hatuhitaji katiba mpya na tuna hoja na sababu za msingi ..nchi yetu imekuwa na amani kwa miaka zaidi ya 50 kwa katiba hii .. nchi yetu imekuwa na uchumi unaokuwa vizuri kwa katiba hii ... Kwa sisi tusiotaka katiba utatusikiliza lini ? Na sisi tuna haki ya kusikilizwa kama ulivyowasikiliza hao wanaotaka katiba mpya !! Mimi na wenzangu wengi TU tusiotaka katiba mpya tutasikilizwa lini ? Hatutaki kabisa katiba mpya !! Tumeona nchi jirani zilizokimbilia katiba mpya kwa minajiri ya ustawi kisiasa na maisha ya watu wetu lakini imekuwa kinyume chake! Kenya vurugu tupu! Afrika kusini vurugu tupu !! Nchi zote zilizothubutu kubadilisha katiba ziliingia kwenye migogoro isiyoisha .. please rais hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu ..asanteni
..
 
Kwa nini utake kuzuia mchakato wa watu kujiamulia mfumo wao wa kujiendesha??
Ni sawa wewe kutotaka katiba mpya, ila ni wendawazimu kutaka kuzuia mchakato wa kidemokrasia wa raia wengi kuamua wajitawalaje.
Niko tayari kukosolewa na nimejiandaa kwenda kuzuia huu mchakato mahakamani
 
Kama unafahamu uhuru wa maoni kwa nini unataka kuzuia huo huru wa wananchi wengi kufikia hatua ya kupiga kura ya maoni kujiamulia mfumo wao wa uendeshaji nchi yao?? Kuna nati zitakuwa hazijakaza vizuri kichwani kwako.
Juha ni wewe usiejua maana ya uhuru wa maoni wewe ni mpumbavu
 
Hayo ya sasa hivi Kenya ni maandamano tu yanayoruhusiwa na Katiba, mwaka 2007 wakati wanachinjana katika vurugu baada ya uchaguzi wakiwa na katiba chakavu ya zamani itakuwa bado ulikuwa unanyonya na kutawazwa.
Walisifia nchi jirani wakati wa uchaguzi eti katiba mpya sasa kinachotokea huko siyo katiba mpya bali kitabu kipya
 
Duh...!. Mkuu Mganguzi , kwanza nikupongeze kwa bandiko hili na kuheshimu uhuru wa maoni na uhuru wa kijieleza, yaani freedom of expression and freedom of speech.

Dunia ilipoumbwa, hakuna aliyejua dunia ni duara, watu wote kwa kutokujua kwao wakajua umbo la dunia ni umbo bapa.

Galileo Galilee alipogundua telescope na kuliona umbo la dunia kupitia kivuli cha kwenye mwezi, alipotangaza kuwa dunia ni duara, Galileo Galilee aliuwawa kwa kosa la kumkufuru Mungu kwa kitendo chake cha kusema dunia ni duara!.

Ukiwa hujaonja embe dodo ukiambiwa tunda tamu kuliko yote ni pera utaamini mpaka utakapoonja embe dodo ndio utagundua kumbe tunda tamu ni embe dodo.

Ukionja zabibu unagundua ni zabibu, ukionja nanasi unagundua ni nanasi, ukionja tende unagundua ni tende, ukionja asali ndipo utagundua asali ndio funga kazi ya utamu!.

Wewe ni mmoja wa Watanzania wasiojua katiba wala Umuhimu wa katiba mpya, hivyo wameridhika sana na hii katiba pera iliyopo, bila kuonjeshwa katiba embe, katiba nanasi, katiba tende na katiba asali, kamwe hauwezi kujua Umuhimu wa katiba mpya.

Hili la Watanzania kutujua katiba, hata Rais Samia amelisema

Hivyo watu kama akina sisi tuliobahatika kajiuwezo ka kusoma sheria na kuijua katiba, tumejitolea kuwaelimisha wengine Umuhimu wa katiba mpya kwanza kwa kuwaelimisha Watanzania wenzetu elimu ya katiba ili waifahamu katiba.

Angalia bandiko hili elimishi kuhusu kuijua katiba ni la lini na limechangiwa na watu wangapi ili kupata picha ya Watanzania wanavyotaka kuijua katiba Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio ila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?
Just imagine mtu unajitolea kuelimisha umma kuhusu katiba halafu responses ndio hii!, utaendelea kweli?.

Hivyo watu kama nyinyi mnapojitokeza kusema hamuhitaji katiba mpya, hatuwashangai bali tunawahurumia!.

Laiti ungelijua tungekuwa na katiba bora, Tanzania tungekuwa wapi, ndipo ungeweza kujua tofauti ya utamu wa pera na asali!.

Kama una muda karibu pande hizi
P

We nani aweza kukuamini na huu upotoshaji wako. Galileo hakuuawa alifungwa na kanisa. Halafu we umeonja wapi hiyo katiba mpya ambayo haipo. Umeandika porojo tupu
 
Asalaam ndugu zangu ..nianze Kumpongeza rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya .. wamesikilizwa na ninasikia mchakato karibia utaanza ni jambo jema ... Lakini tupo sisi ambao hatukubaliani na mchakato huo .. hatuhitaji katiba mpya na tuna hoja na sababu za msingi ..nchi yetu imekuwa na amani kwa miaka zaidi ya 50 kwa katiba hii .. nchi yetu imekuwa na uchumi unaokuwa vizuri kwa katiba hii ... Kwa sisi tusiotaka katiba utatusikiliza lini ? Na sisi tuna haki ya kusikilizwa kama ulivyowasikiliza hao wanaotaka katiba mpya !! Mimi na wenzangu wengi TU tusiotaka katiba mpya tutasikilizwa lini ? Hatutaki kabisa katiba mpya !! Tumeona nchi jirani zilizokimbilia katiba mpya kwa minajiri ya ustawi kisiasa na maisha ya watu wetu lakini imekuwa kinyume chake! Kenya vurugu tupu! Afrika kusini vurugu tupu !! Nchi zote zilizothubutu kubadilisha katiba ziliingia kwenye migogoro isiyoisha .. please rais hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu ..asanteni
..
Naunga mkono Hoja kwa asilimia 100 .Watanzania hatuna haja ya Katiba Mpya .Katiba ya Mwaka 1977 ni Msingi Imara wa Taifa letu. Mambo yote ambayo tumeyafanikisha kama Taifa au Watu binafsi yametokana na Katiba hii.

Wanatokea baadhi ya Watanzania wenzetu kwa maslai ambayo hayako wazi , ovu,potofu na hatarishi wanataka Katiba hii ibadishwe.Kumbukeni mkibadirisha Katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 huo ndio utakuwa Mwisho wa utambulisho wa Mtanzania.

Acheni kufanya majaribio kwenye eneo lisilohitaji majaribio hata kidogo.

Matatizo mlio nayo au matatizo tuliyonayo kama Nchi kisiasa,kiuchumi,kiteknojia,kibailojia, kiutamaduni,kitibabu etc hayawezi kutatuliwa kwa kubadilisha Katiba.

Mkifanikisha hili mtakuja na hoja ya kubadilisha VITABU VYA DINI ili kuendana na matakwa yenu.

Yangu Maoni ni hayo kwa ajili ya rejea mbeleni.

ARTICLE.
 
Subiria kura ya maoni ndio tutajua wangapi wanataka na wangapi hawataki katiba mpya.
Hata wakati wa kurudisha vyama vingi inasemakana wengi karibia 80% walijifanya hawataki vyama vingi kupitia Tume ya Nyalali ila mwaka 1995 kwenye uchaguzi wa vyama vingi Mrema alipata 40% ya kura. Hiyo janja janja yenu itaamuliwa kwa kura.

Kuhusu vitabu vyako vya dini hakuna anayejali , hayo ni mambo yenu na waumini wenzako huko kwenye nyumba zenu za ibada. Mkiamua kuvibadilisha, kuvichoma au kuachana navyo kabisa ni juu yenu. Hili taifa halina dini, haliwezi kuingilia mambo yenu kama hamvunji amani ya nchi.
Naunga mkono Hoja kwa asilimia 100 .Watanzania hatuna haja ya Katiba Mpya .Katiba ya Mwaka 1977 ni Msingi Imara wa Taifa letu. Mambo yote ambayo tumeyafanikisha kama Taifa au Watu binafsi yametokana na Katiba hii.

Wanatokea baadhi ya Watanzania wenzetu kwa maslai ambayo hayako wazi , ovu,potofu na hatarishi wanataka Katiba hii ibadishwe.Kumbukeni mkibadirisha Katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 huo ndio utakuwa Mwisho wa utambulisho wa Mtanzania.

Acheni kufanya majaribio kwenye eneo lisilohitaji majaribio hata kidogo.

Matatizo mlio nayo au matatizo tuliyonayo kama Nchi kisiasa,kiuchumi,kiteknojia,kibailojia, kiutamaduni,kitibabu etc hayawezi kutatuliwa kwa kubadilisha Katiba.

Mkifanikisha hili mtakuja na hoja ya kubadilisha VITABU VYA DINI ili kuendana na matakwa yenu.

Yangu Maoni ni hayo kwa ajili ya rejea mbeleni.

ARTICLE.
 
Subiria kura ya maoni ndio tutajua wangapi wanataka na wangapi hawataki katiba mpya.
Hata wakati wa kurudisha vyama vingi inasemakana wengi karibaia 80% walijifanya hawataki kupitia Tume ya Nyalali ila mwaka 1995 kwenye uchaguzi wa vyama vingi Mrema alipata 40% ya kura. Hiyo janja janja yenu itaamuliwa kwa kura.

Kuhusu vitabu vyako vya dini hakuna anayejali , hayo ni mambo yenu na waumini wenzako huko kwenye nyumba zenu za ibada. Mkiamua kuvibadilisha, kuvichoma au kuachana navyo kabisa ni juu yenu. Hili taifa halina dini, haliwezi kuingilia mambo yenu kama hamvunji amani ya nchi.
Katiba ndio Dini yetu Kama Taifa.Unaposema wewe ni Mtanzania rejea ya utanzania inakuwa inaanzia kwenye Katiba na si penginepo popote.
 
Kama hiyo katiba mpya haitawekwa sheria ya kunyonga mafisadi hata Mimi pia sitaki maana itakuwa hakuna jipya
 
Tatizo la wanasiasa haswa vyama vya upinzani wanadhani kuwepo kwa katiba mpya kutawawezesha washike dola!!!!!
Mimi nasema fikra hizo ni za kipuuzi!

Mfano angalia nchi JIRANI ya Kenya pamoja na kuwa na katiba mpya nzuri lakini kila Uchaguzi Raila analia hakubali matokeo na hakubali maamuzi ya mahakama!!!!

Kwa maana hiyo ni wazi kuwa katiba mpya sio "mwarobaini"

Kwa mtizamo wangu, maadili/uadilifu ndio jambo la msingi ambao hauletwi na katiba mpya bali unajengwa kwa kizazi na kizazi.

Uadilifu na maadili mazuri ya viongozi wetu wote walio pita kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa awamu ya sita ni kutokana na uadilifu wa viongozi wetu, wamejengwa na kulelewa kwenye misingi ya maadili na uadilifu.
 
Back
Top Bottom