Rais wa Ethiopia awasili Chato mkoani Geita. Rais Magufuli aahaidi kuwaachia wahamiaji haramu 1789 kutoka Ethiopia bila masharti

Lissu aliposema ule uwanja hauna activities zozote sasa mkuu anawalazimisha wageni wake watue angalau kule?
London ina Viwanja vitatu vya ndege vya kimataifa, Heathrow ndo kikubwa na busiest kuliko vyote siyo Uingereza tu bali Ulaya yote na kila dakika 5 kuna ndege ya abiria inapaa au inatua katika Uwanja huo. KIA, Kiwanja kikubwa kuliko vyote Tanzania kinapokea ndege moja au mbili za abiria kwa siku. Mh. Lissu alikuwa na maana hiyo!
 
Unaogopa mabadiriko wewe...maisha hayapo constant ki hivyo
Hakuna Mwanadamu makini duniani anayeogopa mabadiliko, ila hayo mabadiliko yawe kwa misingi ya Katiba na Sheria za nchi - Rais anafanya kazi zake zote kwa mujibu wa Katiba na sheria na si vinginevyo

Wananchi wanamtafuta Rais wao hawajui aliko - maana IKULU zote zinazotambulika kisheria hayupo - yupo wapi?? CCM mtujibu Rais wetu mmempekela wapi?
 
Samahani mkuu, KIA ndio kiwanja kikubwa Tanzania?
 
Chato kuna ikulu? Nijuavyo ikulu ndogo ni makao makuu ya mikoa sasa labda tuambiwe makao makuu ya Geita ni chato
Unaruhusiwa kusimamia unachokijua ila sio kila unachokijua wewe ndio kiko sahihi
Kwa hiyo leo rais akisema akafanyie kazi ikulu ya ndogo ya mkoa wa Kilimanjaro utakataa kwamba sio ikulu sababu haipo kwenye makao makuu ya mkoa
 
Hata Nyerere kazi nyingine alifanyia Msasani!
 
Tulisema tunahamia Dodoma ila gari imefeli breki!
 
Alipohamishia serikali Dodoma mlipinga, Anafanyia kazi ikulu ya chato mnapinga, Asipofanya kazi mnasema kajificha corona.... Akianza kufanyia kazi mkoa gani kwenu itakua sawa?

Mamlaka ya rais iheshimiwe tuu
Chato.....kuna IKULU kumbe....
 
Naomba kujuzwa wakuu...hivi
Ikulu ni mahala popote anapolala rais wa nchi kwa wakati fulani? au ni maala maalum palipotengwa kwa ajili ya shughuri za taasisi ya urais..??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…