Rais wa Malawi akatiza ghafla ziara yake nchini Tanzania

Rais wa Malawi akatiza ghafla ziara yake nchini Tanzania

sasa huyo Rais wa nchi ambayo haina hata sungu sungu wenye ueledi hata asingekuja tungekosa nini
 
sasa Hugo rais wa nchi ambayo haina hata sungu sungu wenye ueledi hata asingekuja tungekosa nini

Yamekuwa hayo tena Mkuu !?.Jana si mlikuwa nae mnazindua Kituo cha Basi na manguo yenu ya kijani ?
,🙄🙄🙄😌 Duh!!.
 
Habari zinasema rais wa Malawi amekatiza ziara yake hapa nchini baada ya mazungumzo na Rais Magufuli na wafanya biashara wa Malawi.

Rais Chakwera alifika Tanzania Jumatano kwa ziara ya siku tatu ya kikazi, alitarajiwa kuondoka Ijumaa ila ameondoka alhamisi kutokana na dharura ya mambo ambayo yametokea nchini kwake...
Huyu Rais wa Malawi alitokea Upinzani na lazima aligundua mbinu chafu za mwenyeji wake za kutumia ujio wake kwenye kampeni za Uchaguzi ili abaki madarakani kuendeleza ubabe wake wa kuwabana Wapinzani.

Vimiradi, ambavyo havina maslahi kwa Malawi, alivyozungushwa kuona kweli vilikuwa hata vimefikia hadhi ya kukaribisha Rais wa nchi nyingine aje kuweka jiwe la msingi au kutembelea?

Rais wa Malawi asingegundua mapema angeshirikishwa kwenye Mkutano wa Mwenyeji wake wa kampeni Uwanja wa Mkapa leo kuanzia saa moja asubuhi kama ilivyokuwa imetangazwa maana angekuwa bado yupo nchini.

SGR ni Mradi ambao hauna faida yoyote kwa Malawi lakini hata hatua iliyofikiwa kweli inaweza kujustify kumkaribisha kiongozi wa nchi nyingine aje kuangalia ujenzi ambao katika miaka 5 haujafika popote?
 
Hapana alitumia English kudefend thesis yake hata hivyo alikuwa ni Mwalimu kwahiyo hatutegemei kiingereza kibovu kama kile kutoka kwake labda hiyo Phd iwe feki
Ndio maana nikauliza hiyo PHD ni ya kiingereza,maana hapo umepima elimu yake kwa kuangalia uwezo wake wa kuongea lugha ya kiingereza.

Kwa sababu mtu kushindwa kuongea vizuri lugha kuna sababu zake tofauti tofauti na hilo ni tatizo ambalo watanzania wengi tunalo ila hiyo haina maana kuwa hatukuwa tukielewa masomo yetu au hatukuwa tukitumia hicho kiingereza huko masomoni.
 
Janja ya Chakwera hataki kutumika....unajua Magufuli maji ya shingo sasa hivi anachomekea kila kitu kuokoa jahazi....Chakwera ni mpinzani ni mwanasiasa wa muda mrefu anajua hila za ccm ktk kukwamisha demokrasia. Hata hivyo alikuja tu kwa maslahi ya wana malawi tu.
Chakwera anatokana na chama cha MCP ambacho ndicho kilipigania uhuru wa Malawi. Hicho chama kiliondoshwa na Muluzi uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi na sasa kimerudi madarakani.
 
Katiba yetu ni moja kati ya katiba za ajabu kabisa duniani kipindi cha kampeni mgombea uraisi hapaswi kuwa na cheo cha uraisi kufanya hivyo ni kujifanyia kampeni.
Ni nchi gani duniani Rais wa nchi wakati wa kampeni za uchaguzi anaacha urais kwa muda?
 
Sasa Kama alikuja kuxindua stendi ya mabasi si ameona huo Ni upuuzi
 
Kiitifaki hili ni Jambo la kawaida tu na wala sidhani kama kuna haja ya kuanza sijui kutengeneza 'Hypotheses' juu yake. Mengine ni ya ndani mno.
 
Back
Top Bottom