TANZIA Rais wa Namibia, Hage Geingob afariki Dunia

Pamoja Na mambo mengine umri wake ulikuwa umeenda saana

Miaka 82 ni aged sana kuendelea kuwa madarakani, Kuna muda inatakiwa kupumzika..mbona Sisi wafanyakazi tuna stafu age YA 60 bila extension of another year

Sasa chukua miaka YA kustaff ongeza miaka 22 upo oficene

RiP Rai's Wa Namibia..bado Paul Bia Wa Cameroon, Mseven ,Kagame..file muda wastafi
 
Huyu ndio alimkaripia yule balozi wa ujerumani aliposema mbovu kuhusu uwepo wa wachina Namibia.
 
duuu... wiki iliyopita alikimbilia nje kutibiwa, Mungu akamfuma Marekani huko akamwambia .... weee, usintanie...
rudi kafie mbele huko wanakofia wenzio....

===================
CNN World / Africa
Geingob was receiving treatment at the hospital after revealing in January he had been diagnosed with cancer. He had returned last Wednesday from a trip to the United States, where he was undergoing a two-day treatment as part of a medical trial, according to his office.
 
Poleni ndugu, jamaa na marafiki wa Mr President.
 
Safiri salamaa..tupo nyuma wasafiri wenzio
 
Huo ndio ukomavu, pamoja na umri wake wa miaka 82 wameweza kuweka wazi ugonjwa wake. Afrika ina la kujifunza kupitia Namibia,
Mwendo ameumaliza, mengine tumuachie Mungu ndio anajua ya kumfanya huko aliko.
 
Umri mzuri wa kufa.
Alifariki katika Hospitali ya Lady Pohamba Windhoek.

Kuna GT member mwenzetu humu Pohamba
 



Rais wa Namibia Hage Geingob amefariki dunia asubuhi hii akiwa na umri wa miaka 82, Ofisi yake imesema, wiki tatu baada ya kutangazwa kuwa angefanyiwa matibabu ya saratani.

Geingob alifariki katika Hospitali ya Lady Pohamba huko mji mkuu Windhoek akiwa na mkewe na watoto wake, Makamu wa Rais Nangolo Mbumba alisema katika taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa rasmi wa Facebook wa Geingob.

"Taifa la Namibia limepoteza mtumishi bora wa watu, shujaa wa mapigano ya ukombozi, muasisi mkuu wa katiba yetu na nguzo ya nyumba ya Namibia," alisema Mbumba.

"Wakati huu wa huzuni kubwa, nawasihi wananchi waendelee kuwa watulivu wakati serikali inashughulikia mipango ya mazishi ya kitaifa, maandalizi na itifaki nyingine muhimu. Taarifa zaidi kuhusu hili zitatolewa."

Ofisi ya Geingob ilitangaza mwezi uliopita kuwa alikuwa ameanza matibabu baada ya kugunduliwa "seli za saratani" wakati wa upasuaji wa kawaida wa utumbo mdogo na utumbo mkubwa.

Tangazo hilo halikutoa maelezo ya uchunguzi wa kiongozi huyo wa lakini lilisema kuwa atakuwa anaendelea na majukumu yake ya urais.

Ofisi ya Geingob baadaye ilitangaza kwamba atakwenda Marekani kwa matibabu na atarejea Namibia tarehe 2 Februari.

Geingob, ambaye aliwahi pia kuwa waziri mkuu kwa miaka 12, alikuwa na historia ya matatizo ya afya kabla ya kuchaguliwa kuwa rais wa tatu wa Namibia mwaka 2014.

Mwaka 2013, mwanaharakati huyo wa kupinga ubaguzi wa rangi aliyegeuka kuwa mwanasiasa alifanyiwa upasuaji wa ubongo, na mwaka uliofuata alisema kuwa alikuwa amepona saratani ya tezi dume.

Mwaka jana, Geingob alitangaza kuwa alikuwa amefanyiwa upasuaji wa aorta jimboni Afrika Kusini.

Namibia, koloni la zamani la Kijerumani ambalo lilipata uhuru kutoka Afrika Kusini mwaka 1990, inatarajiwa kufanya uchaguzi wa rais na bunge mwezi Novemba.

Geingob hakuweza kugombea uchaguzi tena kwa sababu katiba ya Namibia inazuia rais kuhudumu kwa vipindi viwili tu.

Mgombea urais kutoka chama tawala cha SWAPO, Nandi-Ndaitwah, atakuwa rais wa kwanza mwanamke wa nchi hiyo endapo atachaguliwa.
 
Kweli mimi nipo nyuma ya current affairs kabisa!

Leo ningepewa mtihani wa swali tu dogo: ...'taja Rais wa Namibia'...
Waalah ningeliangukia pua!

Baada ya Samu Nujoma sijawahi tena kujishuhulisha kujua viongozi wa nchi hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…