Rais wa nchi kuiita pesa ya nchi yake pesa ya madafu, kiongozi kweli huyo?

Rais wa nchi kuiita pesa ya nchi yake pesa ya madafu, kiongozi kweli huyo?

Mkuu mtoa mada hili jambo liliniuma sana nikalipost facebook straight ili liwalo na liwe. Wachangiaji wasioona tatizo ni washabiki ambao upeo wao wa masuala ya uchumi na fedha ni mdogo sana. Na hawajui thamani ya fedha inaakisi nini, pili hata Kikwete mwenyewe hajui kwanini hela yetu inashuka thamani kila uchwao. Kweli shule ni tatizo

Uwezo wa Rais wetu unatia mashaka. Lugha za mitaani na sokoni Kariakoo huwezi kuziweka katika hotuba ya kitaifa kama ile ambayo unajua nchi nzima na mashirika wahisani wanasubiri kusikia utasema nini.
Kama kiongozi wa nchi anajua wazi kuwa utawala wake umeshindwa kuimarisha uchumi na pesa yetu inadondoka kwa kasi na wananchi kwa hasira waaiita pesa hiyo ya MADAFU. Hakupaswa naye kama Rais kulibariki jina hilo la kejeli la pesa yetu hadharani. Hii nisawa na mwenye mke ambaye anashindwa kumtunza kiasi anaonekana mchafu na mtaani ana jina la utani " Masulupwete".
Sasa mume awe ana address kikao cha mtaani kisha anamtambulisha mkewe kama Masulupwete huo sii utakuwa ujinga?
 
kama raisi anajukumu la kusimamia ukuaji wa uchumi na thamani ya fedha ya nchi yake,kinyum cha hapo ni umasikini uliotopea kwa wananchi wake
 
Mimi sijaona tatizo lolote, kukosa hoja za msingi za kujadili mambo muhimu
tunakaa kushupalia neno 'pesa ya madafu'. Labda hili linaweza kuwa tatizo
kwa watu wa shamba na si mjini. Neno hilo halina athari yoyote iwe kisiasa
kiuchumi nk. Tutafute kukosoa hotuba yake katika mambo mengine
kujadili hili ni upuuzi zaidi.
Kuwa mzalendo ww!! Kushuka kwa thaman ya tsh kwa dola kumeifanya wanasiasa kama chenge, na jk kuita pesa yetu kwa maneno ya kejeri na dharau. Kuwa na rais mswahl ndo tabu yake hyo
 
Uwezo wa Rais wetu unatia mashaka. Lugha za mitaani na sokoni Kariakoo huwezi kuziweka katika hotuba ya kitaifa kama ile ambayo unajua nchi nzima na mashirika wahisani wanasubiri kusikia utasema nini.
Kama kiongozi wa nchi anajua wazi kuwa utawala wake umeshindwa kuimarisha uchumi na pesa yetu inadondoka kwa kasi na wananchi kwa hasira waaiita pesa hiyo ya MADAFU. Hakupaswa naye kama Rais kulibariki jina hilo la kejeli la pesa yetu hadharani. Hii nisawa na mwenye mke ambaye anashindwa kumtunza kiasi anaonekana mchafu na mtaani ana jina la utani " Masulupwete".
Sasa mume awe ana address kikao cha mtaani kisha anamtambulisha mkewe kama Masulupwete huo sii utakuwa ujinga?

100% na watu wazima humu JF eti hawaoni tatizo? Yule ni mkuu wa nchi na alikuwa anaongelea hatima ya maisha yetu. Wengi wetu sasa tunashindwa hata kupanga bajeti kwasababu ya mfumuko wa bei. Mada yenyewe aliyokuwa anaongelea sio ya utani kwani wafadhili wamezuia hela na watu wanakufa kwa kukosa dawa
 
Nimemsikiliza rais Jakaya Kikwete (JK) jana na hotuba yake ya kujibaraguza mbele ya Watanzania. Sikutegemea jipya kwenye story zake za jana na wale Wazee wa vijiwe vya CCM ila hili la yeye kama rais wa nchi kudharau sarafu ya nchi yake mwenyewe hadharani limenisikitisha sana.

Ni ajabu sana kwa rais wa nchi kwenda mbele ya vyombo vya habari kukiwa na halaiki ya watu na kuiita bila haya wala aibu sarafu ya nchi kwa jina la kebehi kuwa eti ni "hela ya madafu" halafu anaachwa tu hakuna kitakachompata. Hii ni fedheha na dharau ya hali ya juu kwa sisi ambao hela hiyo ya 'madafu' ndio mshahara wetu na fedha yetu ya kufanya biashara kila siku.

Tunajua mmeiba sana na tena mkishaiba chap chap mnazibadilisha kuwa dollar hivyo haya "madafu" hata yawe sawa na toilet paper (karatasi za kuchambia) kwenu sio issue. Itakuwa ajabu sana kama nikimsikia tena waziri wa fedha na uchumi akisisitiza wafanyabiashara hasa Wahindi ambao wanajua sana umuhimu wa dhamani ya fedha wasiuze bidhaa zao kwa dollar maana hela wanayoambiwa watumie hata mkuu wa nchi anaiona haina maana yoyote zaidi ya kuwaweza kununulia tunda la bei duni la aina ya madafu.

Rais anatakiwa aelewe kuwa kauli zake za namna hii tena anazozitoa hadharani zina madhara ya moja kwa moja kwa uchumi wetu na achunge sana kauli zake anapozungumza masuala muhimu ya nchi hadharani. Kama ni kutudharau kesha fanya hivo sana lakini atuache basi na hii sarafu yetu ambayo kila kukicha anafanya mbinu za kuishusha dhamani. Kudharau sarafu ya nchi hadharani tena mchana kweupe na mtoa dharau akiwa ndie rais wa nchi inatakiwa liwe kosa la uhujumu uchumi na JK anapaswa kushitakiwa kwa hili.

Tumekuvumilia kwa mengi JK lakini kwa kuifananisha sarafu yetu na madafu umevuka mipaka. Bora ungeiita hivyo ukiwa chumbani kwako au ukisha acha nafasi yako ya urais. Ni kwa sababu unaongoza nchi yenye mifumo mibovu ya sheria inayokulinda laiti ingelikuwa nchi nyingine kauli yako hiyo ingetosha wewe kujiuzulu ukachunge mbuzi wako kule Msoga.

Mwana JF hebu piga picha nini kitampata rais Baraka Obama wa Marekani kama siku atakwenda hadharani kukiwa na vyomba vya habari na kutamka maneno ya dhihaka kwa dollar kama alivyofanya rais Jakaya Kikwete jana pale ukumbi wa Diamond Jubilee. Jibu nadhani unalo mwenyewe mwana Jf.

Wasalaam,
Kinyungu.

Nilipata ukakasi
 
Mimi sijaona tatizo lolote, kukosa hoja za msingi za kujadili mambo muhimu
tunakaa kushupalia neno 'pesa ya madafu'. Labda hili linaweza kuwa tatizo
kwa watu wa shamba na si mjini. Neno hilo halina athari yoyote iwe kisiasa
kiuchumi nk. Tutafute kukosoa hotuba yake katika mambo mengine
kujadili hili ni upuuzi zaidi.

Maneno yanabeba maana kubwa. Ni kielelezo tosha jinsi mtu anavyoelewa au kulichukulia au kulipa uzito jambo. AMECHEMKA!
 
Mimi sijaona tatizo lolote, kukosa hoja za msingi za kujadili mambo muhimu
tunakaa kushupalia neno 'pesa ya madafu'. Labda hili linaweza kuwa tatizo
kwa watu wa shamba na si mjini. Neno hilo halina athari yoyote iwe kisiasa
kiuchumi nk. Tutafute kukosoa hotuba yake katika mambo mengine
kujadili hili ni upuuzi zaidi.

Sawa mtoto wa mtaani
 
Kwa hiyo wewe huoni 'udhaifu' uliopo katika kutamka maneno kama hayo. Yeye ni kiongozi wa nchi mkuu, anatetea maslahi ya Tanzania duniani kote. Kuitaja sarafu ya nchi anayoongoza kwa miaka tisa na ushee kuwa ni madafu ni kujidhalilisha mwenyewe. Kama hulitambui hilo angalau fikiri kidogo.
Mkuu,
Hujajibu swali langu lililoko ndani ya hoja yangu.

Kwani pesa ya madafu ni nini au ina maana gani?

Je, hiyo maana inaondoa ukweli wake?

Nadhani hoja yako ina harufu ya political correctness!
 
Kwani hela ya ''madafu'' ina maana gani kwa sababu inawezekana tunalaumu kitu ambacho kinabeba uharisia wa maneno.

Kwani kusema hela ya ''madafu'' ina madhara gani ya moja kwa moja katika uchumi wa nchi?

Naomba unieleweshe kwa sababu sifahamu msingi wa hoja yako.

Mkuu msingi wa kuiita fedha yetu madafu wakati ule ilikuwa ni kumaanisha kuwa ina thamani ndogo kiasi cha kununua madafu hata kama ni noti kubwa.

Anachimaanisha mleta thread ni kuwa kwa mkuu wa Nchi kutumia kejeli hiyo ni dharau kwa fedha yetu.
 
Moja kwa moja akiachia madaraka ni mahakamani, sasa hivi nahitaji msaada wa kisheria maana hata shilingi ni tunu ya taifa.
 
Mimi sijaona tatizo lolote, kukosa hoja za msingi za kujadili mambo muhimu
tunakaa kushupalia neno 'pesa ya madafu'. Labda hili linaweza kuwa tatizo
kwa watu wa shamba na si mjini. Neno hilo halina athari yoyote iwe kisiasa
kiuchumi nk. Tutafute kukosoa hotuba yake katika mambo mengine
kujadili hili ni upuuzi zaidi.

unajiita "dos santos", ningeshangaa kama ungekuwa na mawazo tofauti na haya
 
Mtoto kama ni mbumbumbu kiasi gani hauwezi kumchana laiv vile2 tena mbele ya wanafunzi ama watoto wenzie kua hana akili, mpumbavuu au la mchafuuu!!!
Especially ukiwa kama mwalimu au mzazi au mlezi!!
JK hana elimu ya kisaikolojia, naamini hata IQ yke ya kuforce sana coz ana uwezo mdogo sana ktk kufikiri!!!!
 
Mkuu msingi wa kuiita fedha yetu madafu wakati ule ilikuwa ni kumaanisha kuwa ina thamani ndogo kiasi cha kununua madafu hata kama ni noti kubwa.

Anachimaanisha mleta thread ni kuwa kwa mkuu wa Nchi kutumia kejeli hiyo ni dharau kwa fedha yetu.
Mimi sioni tatizo lolote kwa sababu haliondoi ukweli na halileti athari yoyote katika uchumi.

Mbona maneno ya utani au wakati hata UK wanaita utawasikia wanaita pesa yao majina kama quid, nicker, bin lid, vile vile hata Wamarekani wanaita pesa yao majina kama bucks.
 
Nimemsikiliza rais Jakaya Kikwete (JK) jana na hotuba yake ya kujibaraguza mbele ya Watanzania. Sikutegemea jipya kwenye story zake za jana na wale Wazee wa vijiwe vya CCM ila hili la yeye kama rais wa nchi kudharau sarafu ya nchi yake mwenyewe hadharani limenisikitisha sana.

Ni ajabu sana kwa rais wa nchi kwenda mbele ya vyombo vya habari kukiwa na halaiki ya watu na kuiita bila haya wala aibu sarafu ya nchi kwa jina la kebehi kuwa eti ni "hela ya madafu" halafu anaachwa tu hakuna kitakachompata. Hii ni fedheha na dharau ya hali ya juu kwa sisi ambao hela hiyo ya 'madafu' ndio mshahara wetu na fedha yetu ya kufanya biashara kila siku.

Tunajua mmeiba sana na tena mkishaiba chap chap mnazibadilisha kuwa dollar hivyo haya "madafu" hata yawe sawa na toilet paper (karatasi za kuchambia) kwenu sio issue. Itakuwa ajabu sana kama nikimsikia tena waziri wa fedha na uchumi akisisitiza wafanyabiashara hasa Wahindi ambao wanajua sana umuhimu wa dhamani ya fedha wasiuze bidhaa zao kwa dollar maana hela wanayoambiwa watumie hata mkuu wa nchi anaiona haina maana yoyote zaidi ya kuwaweza kununulia tunda la bei duni la aina ya madafu.

Rais anatakiwa aelewe kuwa kauli zake za namna hii tena anazozitoa hadharani zina madhara ya moja kwa moja kwa uchumi wetu na achunge sana kauli zake anapozungumza masuala muhimu ya nchi hadharani. Kama ni kutudharau kesha fanya hivo sana lakini atuache basi na hii sarafu yetu ambayo kila kukicha anafanya mbinu za kuishusha dhamani. Kudharau sarafu ya nchi hadharani tena mchana kweupe na mtoa dharau akiwa ndie rais wa nchi inatakiwa liwe kosa la uhujumu uchumi na JK anapaswa kushitakiwa kwa hili.

Tumekuvumilia kwa mengi JK lakini kwa kuifananisha sarafu yetu na madafu umevuka mipaka. Bora ungeiita hivyo ukiwa chumbani kwako au ukisha acha nafasi yako ya urais. Ni kwa sababu unaongoza nchi yenye mifumo mibovu ya sheria inayokulinda laiti ingelikuwa nchi nyingine kauli yako hiyo ingetosha wewe kujiuzulu ukachunge mbuzi wako kule Msoga.

Mwana JF hebu piga picha nini kitampata rais Baraka Obama wa Marekani kama siku atakwenda hadharani kukiwa na vyomba vya habari na kutamka maneno ya dhihaka kwa dollar kama alivyofanya rais Jakaya Kikwete jana pale ukumbi wa Diamond Jubilee. Jibu nadhani unalo mwenyewe mwana Jf.

Wasalaam,
Kinyungu.

Hiv kwann wengi wetu huonekana tunapenda ukweli lakin ukweli unapowekwa waz kwa baadhi ya mambo tunaanza kukosoa ,tatizo nchi yetu saiz kila mtu anajua , anataka kuonekana anajua zaid ya wengine ( muchknow), sasa ndugu kwann unakataa ukweli alioungea rais kuwa ni fedha za madafu? Hebu nenda kaulize elf 1 ya tanzania ni sawa na dola ngapi za kimarekan hapo ni mwanzo mzuri wa kujua kuwa rais hajakosa kusema alichosema, tatizo ukweli unauma sana lakin ndo ukweli hata ukisema utukane au umshambulie rais , ukweli utabaki palepale na hauwezi kufunikwa na kauli mbiu za kujifariji
 
Aliikuta Tsh 600 kwa USD 1;Sasa ni Tsh 1800 kwa USD 1:anahaki ya kuidharau naamini Ana nia ya dhati kuiua nchi hii.
 
Sasa wewe ulitaka iitwe pesa gani kama si ya madafu, ina thamani gani? mtu anaongea lugha ambae yule msikilizaje ataelewa pia ndiyo jina tulioipa sarafu yetu na tunalitumia katika maongezi yetu ya kila siku.
 
Back
Top Bottom