Pre GE2025 Rais wa Wanafunzi UDSM: Wanafunzi wa Vyuo tutamchagua Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
KUTOKA MAKTABA:

VIJANA NA MABADILIKO, WAKATI HUU 2024 / 2025 NI SAHIHI KUINGIA KTK NAFASI ZA MAAMUZI IKIWEMO URAIS


Duniani ni vijana wa vyuo vikuu ndiyo wanaoongoza kuchagiza mageuzi, Vijana ni taifa la leo, watoto ndiyo viongozi wa kesho. Kauli za kilaghai kuwa vijana ni kwa ajili ya taifa la kesho siyo sahihi.

Vijana msihofu msuguano na wazee waliopo mamlakani, kusubiri kupewa ni kukubali kuwa tumejumuishwa na watoto chipukizi. Ni wakati wa vijana kuchagiza kwa mbinyo wa hoja kuwa uongozi wa nchi ni kwa ajili ya vijana.

Historia inaonesha mara baada ya uhuru wa kwanza kupatikana ktk mtaifa mbalimbalii iwe kwa mtutu wa bunduki au maandamano ya kuondoa wakoloni, baadaye kulifuatia msuguano wa wananchi wenyewe kwa wenyewe kwa kutoridhishwa na wale waliochukua utawala toka kwa wakoloni.

Sababu mbalimbali zilizua msuguano ktk nchi huru kama udiktekta, tawala kamdamizi ya chama kimoja kongwe, utawala mbovu, ubaguzi wa kielimu mfano mtoto aliyesoma shule za kata / st. Kayumba anadanganywa kuwa akihitimu chuo kikuu atakuwa na nafasi sawa na mwenzake aliyesoma St. Mary's akamaliza elimu ya chuo kikuu pia anayekimanya kiingereza vizuri zaidi na wajomba wake wapo ktk nafasi za kiutawala n.k

Hapo ndipo Wanafunzi waliopo ktk nchi kama Sudan, Chile, Cuba, Afrika ya Kusini, Kenya walishiriki kudai mageuzi ili kuondokana na tawala zilizomgoa mkoloni.

Tanzania vijana hawajishughulishi kuhoji mambo yasiyowaridhisha wananchi kama bandari kuchukuliwa kuwa vituo vya nchi ngeni, matumizi mabaya ya kodi za wananchi, tozo zilizokifu wananchi, demokrasia kubinywa, katiba kandamizi n.k

Huko Chile marekani ya kusini nchi iliyo viongozi wa vyama vya wanafunzi wenye kushiriki kikamilifu katika siasa pia maandamano imewezesha kiongozi kijana wa wanafunzi Gabriel Boric ambaye ndiye rais kijana kabisa wa kuchaguliwa amezaliwa 11 February 1986 ambaye alichukua madaraka ya urais tarehe 11 March 2022 baada ya kushinda uchaguzi mkuu nchini Chile tarehe 19 December 2021 kwa kupata asilimia 60% ktk uchaguzi wa urais.

Gabriel Boric on the Chilean student movement 14 June 2017
Mwanafunzi wa chuo kikuu Tanzania toka familia masikini anazama ktk mkondo wa madeni ya fedha za mkopo wa elimu ya juu huku akiwa anaimani na matumaini potofu ya Ilani ya CCM imeandika ahadi ya mambo ya uongo ya kupata ajira, mazingira ruhani kuwa wataweza kupata vyeo vya ulaji vya kisiasa UVCCM, kuwa MNEC Halmashauri Kuu ya CCM, mbunge wa CCM n.k au kuwepo mazingira (hewa) ya kujiajiri.

VIJANA NI WAKATI WA KUACHA KUTEGEMEA CHAMA DOLA KONGWE

Picha maktaba : Vijana chawa wa Vyuo vya elimu ya juu Tanzania.

Vijana vyuo vikuu na mijini pia vijijini badala ya kumezwa na ukiritimba wa UVCCM na ahadi kuwa ni viongozi wa kesho huku watoto wa vigogo wa CCM wanapewa nafasi sasa na siyo kesho wanatakiwa kuunda chombo chao kipya cha kutambulika kama mdau muhimu anayehitaji kuonekana katika majukwaa ya siasa pia ktk vituo vya redio, televisheni na mitandao ya kijamii kuchagiza mabadiliko na mageuzi ikiwemo pia kupewa nafasi nje ya mfumo wa vyama ili wagombee nafasi za kuchaguliwa na wananchi.

VIJANA KULE CHILE BARA LA LATINO AMERIKA WAMEWEZA

Gabriel Boric - The 100 Most Influential People of 2022 - TIME

time.com › collection › gabriel-boric


23 May 2022 · He is making Chile the social, economic, and political laboratory of the world once again. Stiglitz is a Nobel Prize–winning economist
 
Hao sio wanafunzi ila wanachuo/vyuo. Wanafunzi wako primary na secondary.
 
Kaongeza Bajeti ,but it's nothing.
Bajeti siyo ya Kisomi.
Bajeti Kubwa jina hakuna lolote..
Imagine Ada 1.7M ,Mwanafunzi anapangiwa Mkopo, analipiwa 230k kama ada (115k per semester), halafu anapata boom 600k,
Nyumbani kwa Mwanafunzi Wazazi wanajua Mtoto wao Kapata Mkopo wa Serikali.
Wazazi wanajivua Majukumu ya kusomesha baada kujua Serikali imempa kijana wao Mkopo.
Kazi inabaki Kwa Mwanafunzi aliyepata Mkopo 230k kama ada na 600k boom,
Ada Kwa huyu Mwanafunzi atalipa vipi?
Akili kumkichwa.
Ila Wengi Ambao hawana sapoti nyingine tofauti na bodi hawaendelei na masomo
Masomo Kwisha Habari
 
acha upotoshaji gentleman,

kwenye uchaguzi huu,
hata chekechea waliofikisha umri wa miaka 18 wamejiandikisha kupiga kura uchaguzi wa serikali za mitaa, wakiongizwa na kaka zao hawa wasomi makini na wenye maono ya mbali sana, wa elimu ya Juu🐒
Ukitaka kujua CCM inanyofoa ubongo wa vijana na kuwaachia mafuvu msikilize huyu kijana!
 
Imekaa kinaa sana..
Heading: Waafrika na Waarabu
Hotuba imezungumzia waafrika kwa Maneno Mengi.
Trump alikuwa anahutubia wapi Maneno haya?
Source Tafadhali.
 

CHAWA MTOTO ..... Mbona Kafanana na Mwigulu. Au ni Macho yangu tu!!?
 
safi kabisa kiongizi wa wanafunzi chuo kikuuu mama mitano tena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…