Raisi Samia, utatembelea bucha zote lakini maini ni yale yale!

Raisi Samia, utatembelea bucha zote lakini maini ni yale yale!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Sintashangaa kwamba katika maraisi wote wa Tanzania, Raisi Samia atakuwa anashikilia rekodi ya kuteua na kutumbua, na kama bado hashikilii hiyo rekodi, basi ataishikilia hivi punde, na huenda ikawa ni rekodi ya raisi aliyeteua na kutumbua kwa kiwango cha juu zaidi duniani!

Nataka nikueleze wazi Raisi Samia kwamba huwezi kutoa samaki mzuri katika kapu lenye kutoa harufu ya samaki waliovunda. Hawa waeule wako, utawajaribu kila mahali, na mwishowe bado utaona wanapwaya katika nafasi unazowapa.

Sasa ninavyoona hapa una matatizo makubwa mawili katika kuteua kwako; kwanza unateua watu wale wale waliopwaya katika nafasi fulani, ukiwa na matumaini kwamba wataweza katika nafasi nyingine. Hilo halitatokea kamwe. Maini yataendelea kuwa maini katika bucha zote.

Pili ni kwamba, nimeona katika uteuzi wako uko sensitive sana katika dini ya mtu unaemteua. Ni rahisi kuona mara nyingi unaanza na sifa ya udini, kwamba nafasi hii nataka ichukuliwe na mwislamu/mkristo, halafu ndio unatafuta mtu wa kuijaza. Unajaribu ku-balance udini katika wateule wako. That is a very wrong approach, lakini naelewa kwa nini unafanya hivyo.

Ushauri wangu kwako, na nakuhakikishia ukifuata ushauri huu utafanikiwa sana, kubali kuingiza watu wa upinzani au hata watu wasio na vyama vya siasa katika teuzi zako. Kumbuka hilo linafanyika sasa kule Zanzibar bila matatizo, lilifanyika Kenya likafanikiwa na sasa wanalifanya tena, na pia sasa linafanyika South Africa na kwingineko.

Achana na conservatives katika CCM wanaokuambia huwezi kuwaweka watu wa upinzani kwenye baraza lako la mawaziri, au teuzi zako za mawaziri, mabalozi nk. Na unapaswa kuteua watu hao bila kuwataka wajiunge na CCM. Wateue na waambie waendelee kuwa na vyama vyao kisiasa na kuwajibika kwako kikazi. Teua Watanzania wanaoweza kazi, sio vyama vyao vya siasa. Tanzania ni kubwa kuliko vyama vya siasa, kumbuka hilo.

Kwa mfano, umeona kwamba tuna matatizo makubwa katika utendaji wa jeshi la polisi, hadi wamefikia kiwango cha wao kuwa wahalifu sasa, kwa sababu wanaichukulia CCM for granted. Mimi ningekushauri kwamba wizara ambazo zinakuletea lawama sana kama raisi, kama Mambo ya Ndani na Maliasili na Utalii, wape watu wa Upinzani waziongoze. Mwaka 1994, Mandela wa ANC alipokuwa Raisi wa South Africa, alimpa Buthelezi wa Inkatha Freedom Party kuongoza wizara ya Mambo ya Ndani kwa sababu ilionekana kuwa wizara yenye matatizo sana, ambayo yalihusishwa na Inkatha Party ya Buthelezi. Sasa kama wananchi wana malalamiko sana na Polisi na Uhamiaji, wape Wapinzani waongoze Wizara hiyo. Mteue Mbowe, Tundu Lissu au Lema awe waziri wa mambo ya ndani, mwache yeye aliunde upya jeshi la polisi - si itakuwa kwa faida ya Watanzania, pamoja na CCM?

Pia, acha kufikiria dini kabla ya kutafuta mtu wa kujaza nafasi fulani. Kuna wakati Nyerere aliulizwa swali, hivi katika baraza lako la mawaziri kuna waislamu wangapi na Wakristo wangapi, akashangaa, na kusema hajui, na hajawahi hata kufikiria kama huyu ni mkristo au muislamu anapofanya uteuzi. Najua wewe ni tofauti na Nyerere, unafikiria suala la udini unapofanya uteuzi, na huenda hata unajua idadi ya mawaziri wakristo na waislamu katika baraza lako. Achana mtazamo huo kabisa. Sio tatizo kuwa na mawaziri wengi wakristo au waislamu - ili mradi ni watu makini, wachapa kazi na wazalendo wa kweli walioteuliwa.
 

Chief Mangosuthu Buthelezi: The man who divided South Africa​


During apartheid, he was the chief minister of the KwaZulu Bantustan: a semi-independent territory allocated to the Zulu people by the country's white supremacist government.

His administration was widely seen as a puppet regime: dependent on the South African state for power, intolerant of political opposition and dominated by Inkatha - the party he founded in 1975.

Buthelezi eventually joined Mandela's government of national unity in 1994. Despite continuing tensions, he served as minister for home affairs for a decade.

"South Africa is one country," he declared. "It has one destiny. Those who are attempting to divide the land of our birth are attempting to stem the tide of history."

As a result, Buthelezi was appointed Minister of Home Affairs. From time to time, he even acted up as president when Nelson Mandela was abroad.

Kwa hiyo isiwe ajabu kwa Samia kumteua Mbowe akiwa Chadema kwenye baraza la mawaziri, na hata kumfanya amwakilishe raisi katika matukio fulani
 
Hadi sasa ndio anashikilia hiyo rekodi. Ana miaka 3 ila kila taasisi ina wakurugenzi 4 ama 5. Kila wizara una mawaziri 3 am 4, kila halmashauri ina wakuu wa wilaya 3 ama 3, wakurugenzi, ras ama das, rc na wote wanaoteuliwa.
 
Tatizo lake kubwa ni yeye SSH, hana uwezo, kipaji cha uongozi. Suluhisho la kudumu ni yeye SSH kujiuzulu.
Watu wengi wanafikiria Mandela alikuwa na kipaji kikubwa cha uongozi wa serikali. Si kweli. Mandela alikuwa na busara ya kuweka amani katika nchi, lakini kwenye serikali alitumia watu makini sana, bila kujali wanatoka wapi
 
Watu wengi wanafikiria Mandela alikuwa na kipaji kikubwa cha uongozi wa serikali. Si kweli. Mandela alikuwa na busara ya kuweka amani katika nchi, lakini kwenye serikali alitumia watu makini sana, bila kujali wanatoka wapi
Samia uwe uwezo, hiyo busara hana, aliwatimua wote wenye uwezo alipoingia madarakani akawaweka wahuni.
 
Sasa ninavyoona hapa una matatizo makubwa mawili katika kuteua kwako; kwanza unateua watu wale wale waliopwaya katika nafasi fulani, ukiwa na matumaini kwamba wataweza katika nafasi nyingine. Hilo halitatokea kamwe. Maini yataendelea kuwa maini katika bucha zote.
Ni kama wanamshikia bunduki kwamba lazima awateue wao tu. Tangu ameingia madrakani ameteua na kutengua zaidi ya mara tano lkn cycle ni ile ile.

Mh Dr Samia please weka watu wapya hao hawana uwezo tena.
 
Samia uwe uwezo, hiyo busara hana, aliwatimua wote wenye uwezo alipoingia madarakani akawaweka wahuni.
Sasa anaanza kuwatafuta baadhi ya aliowaondoa. Kuna watu nawajua walimshauri watu kama kina Prof. Kabudi wana ambition za kuwa raisi, na huenda ni jambo aliliona toka kwa Magufuli. Hivi Samia hafikirii kuwa Mwigulu ana nia ya kuwa raisi kuliko hata hao kina Kabudi?
 
Sintashangaa kwamba katika maraisi wote wa Tanzania, Raisi Samia atakuwa anashikilia rekodi ya kuteua na kutumbua, na kama bado hashikilii hiyo rekodi, basi ataishikilia hivi punde, na huenda ikawa ni rekodi ya raisi aliyeteua na kutumbua kwa kiwango cha juu zaidi duniani!

Nataka nikueleze wazi Raisi Samia kwamba huwezi kutoa samaki mzuri katika kapu lenye kutoa harufu ya samaki waliovunda. Hawa waeule wako, utawajaribu kila mahali, na mwishowe bado utaona wanapwaya katika nafasi unazowapa.

Sasa ninavyoona hapa una matatizo makubwa mawili katika kuteua kwako; kwanza unateua watu wale wale waliopwaya katika nafasi fulani, ukiwa na matumaini kwamba wataweza katika nafasi nyingine. Hilo halitatokea kamwe. Maini yataendelea kuwa maini katika bucha zote.

Pili ni kwamba, nimeona katika uteuzi wako uko sensitive sana katika dini ya mtu unaemteua. Ni rahisi kuona mara nyingi unaanza na sifa ya udini, kwamba nafasi hii nataka ichukuliwe na mwislamu/mkristo, halafu ndio unatafuta mtu wa kuijaza. Unajaribu ku-balance udini katika wateule wako. That is a very wrong approach, lakini naelewa kwa nini unafanya hivyo.

Ushauri wangu kwako, na nakuhakikishia ukifuata ushauri huu utafanikiwa sana, kubali kuingiza watu wa upinzani au hata watu wasio na vyama vya siasa katika teuzi zako. Kumbuka hilo linafanyika sasa kule Zanzibar bila matatizo, lilifanyika Kenya likafanikiwa na sasa wanalifanya tena, na pia sasa linafanyika South Africa na kwingineko.

Achana na conservatives katika CCM wanaokuambia huwezi kuwaweka watu wa upinzani kwenye baraza lako la mawaziri, au teuzi zako za mabalozi nk. Na unapaswa kuteua watu hao bila kuwataka wajiunge na CCM. Wateue na waambie waendelee kuwa na vyama vyao kisiasa na kuwajibika kwako kikazi. Teua Watanzania wanaoweza kazi, sio vyama vyao vya siasa. Tanzania ni kubwa kuliko vyama vya siasa, kumbuka hilo.

Kwa mfano, umeona kwamba tuna matatizo makubwa katika utendaji wa jeshi la polisi, hadi wamefikia kiwango cha wao kuwa wahalifu sasa, kwa sababu wanaichukulia CCM for granted. Mimi ningekushauri kwamba wizara ambazo zinakuletea lawama sana kama raisi, kama Mambo ya Ndani na Maliasili na Utalii, wape watu wa Upinzani waziongoze. Mwaka 1994, Mandela wa ANC alipokuwa Raisi wa South Africa, alimpa Buthelezi wa Inkatha Freedom Party kuongoza wizara ya Mambo ya Ndani kwa sababu ilionekana kuwa wizara yenye matatizo sana, ambayo yalihusishwa na Inkatha Party ya Buthelezi. Sasa kama wananchi wana malalamiko sana na Polisi na Uhamiaji, wape Wapinzani waongoze Wizara hiyo. Mteue Mbowe, Tundu Lissu au Lema awe waziri wa mambo ya ndani, mwache yeye aliunde upya jeshi la polisi - si itakuwa kwa faida ya Watanzania, pamoja na CCM?

Pia, acha kufikiria dini kabla ya kutafuta mtu wa kujaza nafasi fulani. Kuna wakati Nyerere aliulizwa swali, hivi katika baraza lako la mawaziri kuna waislamu wangapi na Wakristo wangapi, akashangaa, na kusema hajui, na hajawahi hata kufikiria kama huyu ni mkristo au muislamu anapofanya uteuzi. Najua wewe ni tofauti na Nyerere, unafikiria suala la udini unapofanya uteuzi, na huenda hata unajua idadi ya mawaziri wakristo na waislamu katika baraza lako. Achana mtazamo huo kabisa. Sio tatizo kuwa na mawaziri wengi wakristo au waislamu - ili mradi ni watu makini, wachapa kazi na wazalendo wa kweli walioteuliwa.
Mkapa alitupa hotuba za kika mwezi.

Samia anatupa teuzi za kila mwezi.

Ridiculous.
 
Achana na conservatives katika CCM wanaokuambia huwezi kuwaweka watu wa upinzani kwenye baraza lako la mawaziri, au teuzi zako za mabalozi nk. Na unapaswa kuteua watu hao bila kuwataka wajiunge na CCM. Wateue na waambie waendelee kuwa na vyama vyao kisiasa na kuwajibika kwako kikazi. Teua Watanzania wanaoweza kazi, sio vyama vyao vya siasa. Tanzania ni kubwa kuliko vyama vya siasa, kumbuka hilo.
Etwege hata kubali hii😆😆
 
Kuna wakati Nyerere aliulizwa swali, hivi katika baraza lako la mawaziri kuna waislamu wangapi na Wakristo wangapi, akashangaa, na kusema hajui, na hajawahi hata kufikiria kama huyu ni mkristo au muislamu anapofanya uteuzi
Akaja kujua baadaye kuwa walikuwa wakatoliki wawili yeye na Kahama japokuwa Kahama alishakuwa na bibi mbili
 
Kwa mfano, umeona kwamba tuna matatizo makubwa katika utendaji wa jeshi la polisi, hadi wamefikia kiwango cha wao kuwa wahalifu sasa, kwa sababu wanaichukulia CCM for granted. Mimi ningekushauri kwamba wizara ambazo zinakuletea lawama sana kama raisi, kama Mambo ya Ndani na Maliasili na Utalii, wape watu wa Upinzani waziongoze.
Huu uzi ni Mkali sana una nondo nzito.
 
Sasa anaanza kuwatafuta baadhi ya aliowaondoa. Kuna watu nawajua walimshauri watu kama kina Prof. Kabudi wana ambition za kuwa raisi, na huenda ni jambo aliliona toka kwa Magufuli. Hivi Samia hafikirii kuwa Mwigulu ana nia ya kuwa raisi kuliko hata hao kina Kabudi?
SSH ana shida hapendi watu wampite umaarafu, wachapakazi kama Lukuvi, Slaa, Kalemani, Majaliwa, Kabudi, Polepole, Bashiru hawa walikuwa watendaji wazuri angewatumia vizuri wangemsaidia sana na kuepuka matatizo mengi na mikataba mibovu
 
SSH ana shida hapendi watu wampite umaarafu, wachapakazi kama Lukuvi, Slaa, Kalemani, Majaliwa, Kabudi, Polepole, Bashiru hawa walikuwa watendaji wazuri angewatumia vizuri wangemsaidia sana na kuepuka matatizo mengi na mikataba mibovu
Hao uliowataja ndio waliongoza biadmshara ya kutumia peda za walipa kodi kununua wabunge na kurudia chaguzi kila mara.
 
Back
Top Bottom