Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
- Thread starter
-
- #21
Wawaongozao ndio waliowapotosha, tuwaonee huruma tu.Hao uliowataja ndio waliongoza biadmshara ya kutumia peda za walipa kodi kununua wabunge na kurudia chaguzi kila mara.
Hakuna kitu kibaya katika utawala na uongozi kama anaeteuliwa kufanya kazi katika mazingira ya uncertainty, kama kesho atakuwapo au atakuwa ameshaondolewa. Hata ziara utaogopa kufanya, ukihofia usije kutumbuliwa ukiwa ziarani na kuishia kupanda basi kurudi nyumbani toka mikoani. Raisi Samia anapaswa kutambua hiloHadi sasa ndio anashikilia hiyo rekodi. Ana miaka 3 ila kila taasisi ina wakurugenzi 4 ama 5. Kila wizara una mawaziri 3 am 4, kila halmashauri ina wakuu wa wilaya 3 ama 3, wakurugenzi, ras ama das, rc na wote wanaoteuliwa.
Labda tumsifie kama ni kweli ameikabili pressure ya Makamba senior katika kumteua Makamba junior kwenye hizi nafasi. Binafsi nahisi kama baada ya muda mfupi tutasikia Makamba junior kapata uteuzi mwingine mzito. Kuna wakati tulisoma humu JF kwamba influence ya Makamba senior kwenye uteuzi wa Makamba junior ilikuwa kubwa hadi kwenye kusema ni wizara ipi Makamba junior apewe. Na akijua hili Makamba junior ali dictate hata nani anataka kufanya nae kazi, kutia ndani nani awe Mkurugenzi wa Tanesco, na ikabidi watu kama kina Prof. Tito Mwinuka waondolewe Tanesco ili Makamba junior aweke watu wake -kina Mahagarechande, nk! Kilichofuata kila mtu anakijua, very sad indeed, na inabidi tumlaumu Raisi Samia kwa kuruhusu hili. Hawezi kukwepa lawama hapa.Ni kama wanamshikia bunduki kwamba lazima awateue wao tu. Tangu ameingia madrakani ameteua na kutengua zaidi ya mara tano lkn cycle ni ile ile.
Mh Dr Samia please weka watu wapya hao hawana uwezo tena.
Nakumbuka Marehemu Mzee wetu Alhaji Mwinyi, alimteua mtu ambaye alimuharakisha kutoka katika Nyumba ya serikali alipojiuzulu uwaziri, lakini alipokuja kuwa Raisi, alimteua Mtu huyo kuwa Waziri.Huku kwetu sifa ya kwanza uwe chawa.
Yeye anafuata Katiba,kwamba ina mpa hayo mamlaka basi anayatumiaSSH ana shida hapendi watu wampite umaarafu, wachapakazi kama Lukuvi, Slaa, Kalemani, Majaliwa, Kabudi, Polepole, Bashiru hawa walikuwa watendaji wazuri angewatumia vizuri wangemsaidia sana na kuepuka matatizo mengi na mikataba mibovu
Raisi Samia anaweza ku anaona matatizo katika watu anaowateua na hivyo inabidi awatengue, lakini kwa jinsi anavyofanya hivyo kila wakati, eventually conclusion inakuwa kwamba yeye ndio mwenye tatizo, sio hao anaowateua na kuwatengua. Huwezi kuwa kiongozi mahili ikiwa unabadili mawazo kila baada ya miezi miwili au mitatu. Unasababisha instability katika uongozi wa nchi.Hadi sasa ndio anashikilia hiyo rekodi. Ana miaka 3 ila kila taasisi ina wakurugenzi 4 ama 5. Kila wizara una mawaziri 3 am 4, kila halmashauri ina wakuu wa wilaya 3 ama 3, wakurugenzi, ras ama das, rc na wote wanaoteuliwa.
Jackson Makweta alikuwa mmoja wapo wa viongozi wenye ujasiri wa kutokukubaliana na maoni ya Nyerere wakati wa vikao vya baraza la mawaziri. Nyerere hakumuondoa kwa kufanya hivyo. Alikuwa aki-argue na Makweta kwa hojaNakumbuka Marehemu Mzee wetu Alhaji Mwinyi, alimteua mtu ambaye alimuharakisha kutoka katika Nyumba ya serikali alipojiuzulu uwaziri, lakini alipokuja kuwa Raisi, alimteua Mtu huyo kuwa Waziri.
Kila mteule wa Samia sasa hawezi kua na utulivu kazini kwa sababu anajua any time anaondolewa, any time. Uboss serikalini sasa uko very uncertain. Hii ingekua wizarani kwa mawaziri haina shida ila tatizo hadi kwa watendaji wa chini.Raisi Samia anaweza ku anaona matatizo katika watu anaowateua na hivyo inabidi awatengue, lakini kwa jinsi anavyofanya hivyo kila wakati, eventually conclusion inakuwa kwamba yeye ndio mwenye tatizo, sio hao anaowateua na kuwatengua. Huwezi kuwa kiongozi mahili ikiwa unabadili mawazo kila baada ya miezi miwili au mitatu. Unasababisha instability katika uongozi wa nchi.
Instability and uncertainty in public administration is a recipe for failed governance, someone needs to tell President SamiaKila mteule wa Samia sasa hawezi kua na utulivu kazini kwa sababu anajua any time anaondolewa, any time. Uboss serikalini sasa uko very uncertain. Hii ingekua wizarani kwa mawaziri haina shida ila tatizo hadi kwa watendaji wa chini.
Hata Benjamin alivyokuwa Waziri mambo ya Nje , kuna jnr staff alimtolea maneno, lakini hakumuwekea kisasi au kumdhulumu nafasi au utu wake kwa mambo hayo, huo ndio ukomavu wa kuwa KiongoziJackson Makweta alikuwa mmoja wapo wa viongozi wenye ujasiri wa kutokukubaliana na maoni ya Nyerere wakati wa vikao vya baraza la mawaziri. Nyerere hakumuondoa kwa kufanya hivyo. Alikuwa aki-argue na Makweta kwa hoja
Nilijua hatimaye utaingiza udini,na yaelekea focus yako Kila teuzi una scrutinize dini za wateule kwanza which speaks volume on you.Sintashangaa kwamba katika maraisi wote wa Tanzania, Raisi Samia atakuwa anashikilia rekodi ya kuteua na kutumbua, na kama bado hashikilii hiyo rekodi, basi ataishikilia hivi punde, na huenda ikawa ni rekodi ya raisi aliyeteua na kutumbua kwa kiwango cha juu zaidi duniani!
Nataka nikueleze wazi Raisi Samia kwamba huwezi kutoa samaki mzuri katika kapu lenye kutoa harufu ya samaki waliovunda. Hawa waeule wako, utawajaribu kila mahali, na mwishowe bado utaona wanapwaya katika nafasi unazowapa.
Sasa ninavyoona hapa una matatizo makubwa mawili katika kuteua kwako; kwanza unateua watu wale wale waliopwaya katika nafasi fulani, ukiwa na matumaini kwamba wataweza katika nafasi nyingine. Hilo halitatokea kamwe. Maini yataendelea kuwa maini katika bucha zote.
Pili ni kwamba, nimeona katika uteuzi wako uko sensitive sana katika dini ya mtu unaemteua. Ni rahisi kuona mara nyingi unaanza na sifa ya udini, kwamba nafasi hii nataka ichukuliwe na mwislamu/mkristo, halafu ndio unatafuta mtu wa kuijaza. Unajaribu ku-balance udini katika wateule wako. That is a very wrong approach, lakini naelewa kwa nini unafanya hivyo.
Ushauri wangu kwako, na nakuhakikishia ukifuata ushauri huu utafanikiwa sana, kubali kuingiza watu wa upinzani au hata watu wasio na vyama vya siasa katika teuzi zako. Kumbuka hilo linafanyika sasa kule Zanzibar bila matatizo, lilifanyika Kenya likafanikiwa na sasa wanalifanya tena, na pia sasa linafanyika South Africa na kwingineko.
Achana na conservatives katika CCM wanaokuambia huwezi kuwaweka watu wa upinzani kwenye baraza lako la mawaziri, au teuzi zako za mabalozi nk. Na unapaswa kuteua watu hao bila kuwataka wajiunge na CCM. Wateue na waambie waendelee kuwa na vyama vyao kisiasa na kuwajibika kwako kikazi. Teua Watanzania wanaoweza kazi, sio vyama vyao vya siasa. Tanzania ni kubwa kuliko vyama vya siasa, kumbuka hilo.
Kwa mfano, umeona kwamba tuna matatizo makubwa katika utendaji wa jeshi la polisi, hadi wamefikia kiwango cha wao kuwa wahalifu sasa, kwa sababu wanaichukulia CCM for granted. Mimi ningekushauri kwamba wizara ambazo zinakuletea lawama sana kama raisi, kama Mambo ya Ndani na Maliasili na Utalii, wape watu wa Upinzani waziongoze. Mwaka 1994, Mandela wa ANC alipokuwa Raisi wa South Africa, alimpa Buthelezi wa Inkatha Freedom Party kuongoza wizara ya Mambo ya Ndani kwa sababu ilionekana kuwa wizara yenye matatizo sana, ambayo yalihusishwa na Inkatha Party ya Buthelezi. Sasa kama wananchi wana malalamiko sana na Polisi na Uhamiaji, wape Wapinzani waongoze Wizara hiyo. Mteue Mbowe, Tundu Lissu au Lema awe waziri wa mambo ya ndani, mwache yeye aliunde upya jeshi la polisi - si itakuwa kwa faida ya Watanzania, pamoja na CCM?
Pia, acha kufikiria dini kabla ya kutafuta mtu wa kujaza nafasi fulani. Kuna wakati Nyerere aliulizwa swali, hivi katika baraza lako la mawaziri kuna waislamu wangapi na Wakristo wangapi, akashangaa, na kusema hajui, na hajawahi hata kufikiria kama huyu ni mkristo au muislamu anapofanya uteuzi. Najua wewe ni tofauti na Nyerere, unafikiria suala la udini unapofanya uteuzi, na huenda hata unajua idadi ya mawaziri wakristo na waislamu katika baraza lako. Achana mtazamo huo kabisa. Sio tatizo kuwa na mawaziri wengi wakristo au waislamu - ili mradi ni watu makini, wachapa kazi na wazalendo wa kweli walioteuliwa.
Wewe huna utimamu wa akili. Mimi namshauri Samia asifikirie udini wewe unasema naingiza udini, uko sawa kichwani kweli?Nilijua hatimaye utaingiza udini,na yaelekea focus yako Kila teuzi una scrutinize dini za wateule kwanza which speaks volume on you.
Mengine uliyosema yapite ila yaonyesha vile ulivyopiga kimya teuzi za udini za Mwendakuzimu unaumizwa kuondoka kwa Ile monopoly.
Pole Kiboko ya Wachawi
Mjinga ni wewe unayejiona mjanja wengine tunajua kusoma between the lines. Unazeekea JF hukuwai kukemea kiatu kilipokuwa mguu mwingine.Wewe huna utimamu wa akili. Mimi namshauri Samia asifikirie udini wewe unasema naingiza udini, uko sawa kichwani kweli?
Mtu anaesema "Sio tatizo kuwa na mawaziri wengi wakristo au waislamu - ili mradi ni watu makini, wachapa kazi na wazalendo wa kweli walioteuliwa" ni mtu wa udini? Wewe ni mjinga unaehitaji kuelimishwa.
Kitu kimoja ninachojua ni kwamba naweza kuwa mjinga humu JF, lakini nakuzidi akili wewe.Mjinga ni wewe unayejiona mjanja wengine tunajua kusoma between the lines. Unazeekea JF hukuwai kukemea kiatu kilipokuwa mguu mwingine.
Usjione genius Kumbe ni hot foul air tuu.
Kama unaleta mitusi hapa umefika let's take the gloves off
Sorry Kiboko ya Wachawi kuingilia forum inayokupa emotional gratification
Mjinga mwenye akili ,unaumwa tena unaumwa sana psychologically (self inflation egoism syndrome) tafuta usaidizi wa afya ya akiliKitu kimoja ninachojua ni kwamba naweza kuwa mjinga humu JF, lakini nakuzidi akili wewe.
Lazima wewe ni wa dini ile na kutoka kule. Ndio mnaoongea namna hiiMjinga mwenye akili ,unaumwa tena unaumwa sana psychologically (self inflation egoism syndrome) tafuta usaidizi wa afya ya akili
Pungo jua, ni zaidi ya mjinga hasa mpumbavu anaekimbilia kutukana kwenye hoja isiyio hitaji tusi.
Tatizo la makuzi ya hovyo ya mzazi mmoja.
Naamini wewe upo nje ya mfumo kiasi cha kuweza kuongea hivi. Hao hao anaowapa vyeo wanafanya shughuli ya kishenzi ya kumgeuka na kusaliti ofisi wanazopewa.Raisi Samia anaweza ku anaona matatizo katika watu anaowateua na hivyo inabidi awatengue, lakini kwa jinsi anavyofanya hivyo kila wakati, eventually conclusion inakuwa kwamba yeye ndio mwenye tatizo, sio hao anaowateua na kuwatengua. Huwezi kuwa kiongozi mahili ikiwa unabadili mawazo kila baada ya miezi miwili au mitatu. Unasababisha instability katika uongozi wa nchi.
wewe - singularLazima wewe ni wa dini ile na kutoka kule. Ndio mnaoongea namna hii