Ramadhan Special Thread

Ramadhan Special Thread

Asalaam aleyqum ndugu katika imaani, napenda kuuliza vip mwezi umeandama?
 
*بسم الله الرحمن الرحيم*

*MADA YA ISHIRINI NA TISA*

*ADABU ZA IDDI*

Katika Uislamu kuna Iddi mbili, Iddi el Fitri na Idd el Hajj na Waislamu hufurahi katika Iddi hizo furaha anayoiridhia Allah na pia hufurahi kwa Allah kuwawafikisha Waisalamu kukamilisha ibada ya Funga na ibada ya Hijja, na kutaraji kupata malipo makubwa.

Iddi ina hukmu zake na adabu zake ambazo kati ya hizo:

1. Ni haramu kufunga siku ya Iddi. Kwani Mtume SAWW amekataza kama ilivopokewa na Imam Bukhari kutoka kwa Abi Said Alkhudriy,

2. Imesuniwa kwa kutiliwa mkazo Wanaume na Wanawake kwenda kusali sala ya Iddi, hata wenye hedhi wende kunakosaliwa ila wao hawatosali. Kwa ushahidi wa hadithi iliyopokewa na Imam Bukhari na kusimuliwa na Ummu Attiya.

3. Sala ya Iddi huwa kabla ya khutba mbili.

4. Kukoga josho kabla ya kwenda kusali Idd na kujitia mafuta mazuri kwa wanaume.

5. Katika Iddi el Fitri ni sunna kula tende na ziwe idadi ya witri kabla ya kwenda kusali Iddi.

6. Kuleta takbira kwa wengi, njiani, sokoni na vikaoni.

7. Kupongezana kwa kuombeana dua Allah azitakabali amali zetu.

8. Kujipamba kwa kuvaa nguo mpya na nzuri kwa mujibu wa sharia.

9. Kuwasaidia mayatima, masikini na wasiojiweza, na unapotoa utoe kwa nia ya sadaka na sio pokea skukuu yako au mkono wa Iddi.

Tunamuomba Allah atujalie nasi tuwe katika waja wake anao waacha huru na moto na kuwatakabalia dua zao na amali zao njema na anaowasamehe madhambi yao. Aamiyn
 
*KCWW RAM/XXV‎ 1438*

Darsa ya Maswali ya Ramadhani, Jumamosi tarehe 29 Ramadhani 1438, ‎sawa na 24 Juni 2017

SWAUMU YA SITA NA DENI LA RAMADHANI

Nimeulizwa kuhusu kufunga Sita, NANUKUU:‎

Naomba kuuliza, Habib Abdulqadir. Je, inajuzu kwa mtu mwenye deni la ‎Ramadhani kufunga Sita kabla ya kulipa deni lake?‎

JIBU

BISMILLAH

Naam inajuzu iwapo kuna muda wa kutosha wa kufanya yote hayo mawili, ‎kabla ya kumalizika mwezi wa Shawwal. Hivyo, iwapo mtu anadaiwa siku ‎kadhaa za Ramadhani, tuseme siku 7, na umeingia mwezi wa Shawwali, basi ‎anaweza kulipa deni lake la siku 7 za Ramadhani, na kisha akaendelea ‎kufunga siku Sita, ndani ya Shawwal, na kwa kufanya hivyo, atakuwa ‎amepata thawabu kamili za Hadithi isemayo: ‎
‏( مَنْ صَامَ رَمَضَانَ ثُمَّ أَتْبَعَهُ سِتًّا مِنْ شَوَّالٍ كَانَ كَصِيَامِ الدَّهْرِ) ، رواه مسلم‏‎ ‎
“Mwenye kufunga Ramadhani, kisha akafuatiliza kwa siku za Sita katika ‎Shawwali, atapata thawabu za mtu aliyefunga milele.” Riwaya nyengine, ‎‎“ …thawabu za kufunga mwaka mzima”–maana atakuwa amekamilisha ‎KWANZA kufunga Ramadhani, kisha akafuatiliza kwa swaumu ya siku sita, ‎ndani ya Shawwal. Kwa vile kuna sharti la kukamilisha Ramadhani ‎kwanza, kisha kufuatiliza kwa swaumu ya Sita, basi atakuwa amekamilisha ‎kufunga Ramadhani, kwanza, na kisha kufunga sita ndani ya Shawwal.‎

Ama ikiwa hakuna muda wa kutosha kufunga Sita, kutokana na wingi wa ‎deni lake halali la Ramadhani, kama kuumwa kwa muda wa siku 25 katika ‎Ramadhani, basi kuna khilafu ndogo. Wapo wanaosema kuwa anatakiwa kulipa kwanza deni lake la Ramadhani, ‎na kisha afuatilize kufunga siku Sita, hata kama itapindukia kuingia mwezi ‎wa mfungo pili–ilimradi ameanza funga ya Sita ndani ya Shawwal, na funga ‎ya Sita iwe ni kawaida yake kuifunga kila mwaka. Venginevyo–yaani kama ‎SI kawaida yake kufunga Sita kila mwaka–basi itakuwa Sita imempita, na ‎asubiri mwakani, in shaa’Allah. Huu ndio msimamo wa wanazuoni wengi ‎sana wenye kuonelea dharura ya kulipa deni la Faradhi haraka ‎iwezekanavyo– wanaona kuwa faradhi haiwezi kucheleweshwa nje ‎ya wakati wake, kwa kufanya kwanza ibada ya kujitolea.

Wanazuoni wengine–na hawa ndio wengi zaidi–wanaona hakuna ‎ulazima wa kulipa deni la Ramadhani mara tu baada ya kumalizika ‎Ramadhani, hivyo, deni la Ramadhani linaweza kulipwa wakati wowote ‎ule, kabla ya kuingia Ramadhani nyengine. Hivyo, hakuna junaha kuanza ‎kufunga Sita, baada ya kumalizika Ramadhani na kuswali Idi, ili aweze ‎kuipata Sita–siyo tu, katika muda wake ndani ya mwezi wa Shawwal–bali ‎pia kwa kuifuatiliza baada ya Ramadhani. Ilimradi udhuru wa deni lake ni ‎udhuru wa kisheria.‎

Mwenyezi Mungu amesema: ‎
‏ومن كان مريضاً أو على سفر فعدّة من أيام أخر
(البقرة:185)
_‎“Na atakayekuwa mgonjwa, au yumo safarini, basi aweke idadi siku ‎nyengine.”_

Mwenyezi Mungu Hakusema: “aweke idadi mara moja”, bali _“siku nyengine”_. Siku ‎nyengine ni siku nyengine yoyote isiyokuwa siku ya Ramadhani. Hivyo, ‎hakuna ulazima wa kulipa mara moja. Huu ndio msimamo unaoungwa ‎mkono na wanazuoni wengi sana. ‎

Hata hivyo, kuna msimamo wa kati na kati, wenye kuunganisha misimamo ‎hiyo miwili: i) Ulipaji wa haraka na ii) Kujaribu kupata fadhila za Sita, bila ya ‎kupoteza fadhila moja dhidi ya nyengine. ‎

Msimamo huo ni ule wa wanazuoni wanaoona kuwa mtu anaweza ‎kukusanya yote mawili hayo, kwa wakati mmoja, kwa kutia nia ya kulipa ‎Ramadhani kwanza, na kisha kuongezea nia ya kufunga sita wakati mmoja. ‎Yaani nia mbili kwa swaumu moja–ilimradi nia ya kulipa faradhi itangulie ili ‎iweze kuibeba nia ya Sunna ya kujitolea. Hakuna khilafu kuhusu kujuzu nia ‎zaidi ya moja, kwa Ibada moja–ilimradi Faradhi ndiyo iwe yenye kubeba ‎Sunna ya kujitolea na SI kinyume chake. Huwezi kutia nia ya kufunga Sita, ‎na kuongezea nia ya kulipa deni la Ramadhani. Haiwezekani. Nyepesi ‎haiwezi kubeba nzito: Faradhi haiwezi kubebwa na Sunna, ila Faradhi ‎inaweza kubeba Sunna. ‎

Ndiyo maana, ukiingia msikitini ukakuta watu wanaswali jamaa swala ya ‎Faradhi, basi huwezi kuanza kuswali Sunna ya Qabliyya ya faradhi hiyo, ‎wala huwezi kuswali Tahiyyatul-Masjid, ukaacha kujiunga na swala ya faradhi ‎inayoswaliwa jamaa. ‎

Mtume ‎ﷺ‎ amesema, Ikikimiwa Swala ya jamaa hakuna swala nyengine ‎kuswaliwa.” Hivyo, ni budi ujiunge na Swala hiyo ya Jamaa. Ila ukipenda, ‎unaweza kuongezea nia ya Tahiyyatul-Masjid, na vile vile nia ya Qabliyya ya ‎swala hiyo, baada ya nia kuswali faradhi hiyo jamaa; na hapo utakuwa ‎umepiga ndege watatu kwa jiwe moja. Umeswali Faradhi, umeongezea nia ya ‎Tahiyyatul-Masjid, na nia ya Qabliyya ya faradhi hiyo. Hakuna khilafu ‎katika hilo. Vivyo hivyo basi, kuhusu Swaumu ya faradhi na swaumu ya ‎kujitolea. Deni la Ramadhani linaweza kubeba Sunna ya kujitolea ya Sita, ‎pamoja na Sunna ya kujitolea ya Siku nyeupe–endapo utataka kulipa deni la ‎Ramadhani, katika masiku meupe, ndani ya Shawwal. Hakuna junaha.‎

والله أعلم وبالله التوفيق‎ ‎
الحقير إلى الله تعالى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم

**********
‎2. Naomba kuuliza Sharif wangu. Mimi nina kawaida ya kufunga kila ‎Jumatatu na Alhamisi. Je, naweza kufunga Sita ndani ya funga yangu ya ‎Jumatatu na Alhamisi, na nikapata fadhila zote mbili: Fadhila za kufunga ‎Jumatatu na Alhamisi, na fadhila za kuzifunga siku hizo ndani ya Shawwal? ‎Shukran.”‎

JIBU
BISMILLAH

Naam unaweza. Hakuna junaha. Zote hizo ni Sunna za kujitolea. Moja ni ‎Sunna ya majira–Sita katika Shawwal, na nyengine ni Sunna ya masiku–Jumatatu na Alhamisi: Zinabebana. Lau kama una kawaida vile vile ya kufunga ‎masiku meupe–tarehe 13, 14 na 15 za kila mfungo, na swaumu zako ‎zinaingiliana katika siku hizo ndani ya Shawwal, basi unaweza kupata ‎fadhila za swaumu zote hizo–kwa pamoja–kwa nia ya swaumu zote tatu kwa kila ‎siku husika. Hakuna junaha. Na hii ndiyo faida kubwa ya kudumisha ibada ‎ya kujitolea. Ukidumisha ibada ya kujitolea, ukatokewa na udhuru usiweze ‎kuitekeleza katika wakati wake, basi unapata thawabu kana kwamba ‎umeitekeleza katika wakati wake. Na papo, iwapo unataka kuchelewesha ‎kufunga Sita, hadi kuanzia siku nyeupe ndani ya Shawwal, na ikawa ndani ya ‎siku hizo mna siku za Jumatatu na Alhamisi, basi hakuna junaha kuanza ‎kufunga Sita katika masiku hayo, na hivyo unapiga ndege watatu kwa jiwe ‎moja. Maqbuul in shaa'Allah.‎

والله أعلم وبالله التوفيق‎ ‎
الحقير إلى الله تعالى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم

**********
‎3. Alhabib naomba kuuliza: Je, mwenye kufunga Sita kisha akafungua ‎katikati ya siku, anawajibika kulipa? Akiwajibika kulipa, je kuna fidia au ‎kafara ya kutoa?‎

JIBU

BISMILLAH

Swaumu ya kujitolea haina wajibu kulipwa, ndiyo maana ikaitwa Sunna ya ‎kujitolea. Lakini hakuna junaha iwapo umefungua kwa udhuru kuilipa siku ‎nyengine, kwa kufunga tu, pasi na kuweko fidia wala kafara. Huo ndio ‎msimamo wa jumhuri ya wanazuoni.

Hadithi ifuatayo inafafanuwa vizuri zaidi:‎
عن عائشة رضي الله عنها قالت : ( أهدي لي ولحفصة طعام وكنا صائمتين فأفطرنا ثم دخل رسول الله ‏صلى الله عليه وسلم فقلنا له يا رسول الله إنا أهديت لنا هدية فاشتهيناها فأفطرنا فقال رسول الله صلى ‏الله عليه وسلم : لا عليكما صوما مكانه يوما آخر ) رواه أبو داود 2457 ، والترمذي 735‏
Imepokewa kutoka kwa Bi ‘Aisha ‎رضي الله عنها‎ akisema: Tulitunukiwa ‎zawadi ya chakula, mimi na Hafsa, na tulikuwa tumefunga. Basi tukafungua. ‎Baadaye akarudi nyumbani Mtume ‎ﷺ‎ tukamwambia, “Ewe Mjumbe wa ‎Mwenyezi Mungu. Tuliletewa chakula, tukakipenda, basi tukafungua kwa ‎kukila!” Mtume ‎ﷺ‎ akasema, “Hakuna junaha juu yenu. Fungeni siku ‎nyengine badala yake.” Ameipokea Abu Daud na At-Tirmidhi.‎

Fidia ni kwa kutoweza kutimiza wajibu, na kafara ni adhabu ya kuvunja ‎sharia, kwa makusudi. Mwenye kufungua swaumu ya kujitolea, ‎hakuvunja jukumu la kutekeleza wajibu, na wala hakuasi kwa kuvunja sharia. ‎Isipokuwa ni makuruhu kufungua–pasi na sababu ya msingi–swaumu ya ‎kujitolea. Ni sawa na kujitolea mbele ya Mwenyezi Mungu kisha ukatoweka ‎na kuacha kujitolea kwako Kwake! Kama una sababu ya msingi, basi ‎hakuna junaha, unaweza kufunga siku nyengine iwapo swaumu hiyo si ‎swaumu ya tarehe maalumu, kama ‘Arafa, au ‘Ashuura. ‎

والله أعلم وبالله التوفيق‎ ‎
الحقير إلى الله تعالى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم

Imejibiwa na Sayyid Abdulqadir Shareef Aal Shaykh Abi Bakr bin Salim.‎

NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza ‎chochote, ‎na kuweka kwenye FB yako, WhatsApp, na kwenye ‎Makundi ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha Dini. ‎Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.‎

kcwajawema@gmail.com
 
Rosemarie wewe una matatizo,unahitaji kutoka uliko uje huku>je unajuaje leo ni jumamosi?Mungu wenu pale msalabani alipigwa sana na kutundikwa misumari,mkaja mkamtoa misumari mkampeleka kwenye pango,mkaja mkaiba mwili sisi tukawanyamazia na mungu wenu!Inakuwaje Mungu aumbe watu kisha wampige?wamsulubishe?Mungu hakuwa anajua lengo la hao aliowaumba?zile siku 3 mnazodai alikufa watu walikuwa wanaishije?Bila Mungu?Maana alikuwa amekufa!?pia nakueleza Sabato hata hamuijui,Nikuelimishe Ewe Naswara,Jumamosi=1,Jumapili=2,jumatatu=3,jumanne=4,jumatano=5.Alhamis=6.Ijumaa 7.Je ukianza kuhesabu unaanza ngapi?hata sabato Huijui.Lakini Nyie mna dini yenu na sisi tuna dini yetu!
Dah! Nimeipenda hii.. Kwa hiyo Yesu tulimuiba huko kabulini halafu tukampaliza kwenda mbinguni! 😀 Ubarikiwe sana!
 
Mwezi wa Ramadhan umeondoka na ikiwa wewe ni muumini wa kweli yapaswa usikitike kwani mwezi wa ramadhani una baraka zisizo kifani

Tumuogope Mungu na tusihadaike na dunia, ramadhani ni chuo kinachotufunza uchamungu, subra ukarimu upendo na kila aina ya tabia njema,ni kama Mtume(saw) alivyosema;
''sikutumwa mimi, ila kuja kutimilza tabia njema''

kwa hiyo ndugu zangu ikiwa sisi ni waislamu na bila shaka tunaona fahari kuwa waislamu basi tujue, tabia njema ndiyo pambo la muislamu.
ikiwa ulijizuia na zinaa wizi utapeli usengenyaji uwongo n,k kipindi cha ramadhani jua ya kwamba Mungu aliekataza hayo kipindi cha Ramdhan basi amekataza hayo miezi mingine yote.

Na usiku wa kuamkia usiku wa Iddi ni miongoni mwa siku tukufu mno na Mtume (saw) anasema "atakeuhuisha usiku wa Iddi kwa Ibada basi malipo yake ni jannah"
pia tusiwasahau kwa dua wazazi wetu kipindi hiki ikiwa wako hai ama wapo kaburini angalau jitahidi uwasomee surat ikhlaswi mara 3 na swala ya Mtume mara 3 InshaAllah
 
'' Na katika alama zake (Mwenyezi Mungu) ni (kupatikana) usiku na mchana na jua na mwezi; basi msilisujudie jua wala mwezi; bali msujudieni Mwenyezi Mungu aliyeviumba; ikiwa nyinyi mnamuabudu yeye''
Hayo sio maneno yangu nenda kasome Quran 41:37
Hivyo mnaposema waislamu tunaabudu mwezi tunawashangaa sana!!!

Labda tukukumbushe pengine umesahau, au waswahili husema 'nyani halioni kundule'
Wanaopaswa kuulizwa ni wale wanaoabudu SUN-DAY
Siku za jumapili kama hamuabudu jua mnaenda kumuabudu nani?
Kuna andiko lolote katika bible linaoamrisha watu kwenda nyumba za ibada SUN-DAY??????

rosemarie hilo swali nimekuuliza wala sitaki majibu ( kwani najua hauna), baki na dini yako nasi tuachie dini yetu!
ONE LOVE!
 
'' Na katika alama zake (Mwenyezi Mungu) ni (kupatikana) usiku na mchana na jua na mwezi; basi msilisujudie jua wala mwezi; bali msujudieni Mwenyezi Mungu aliyeviumba; ikiwa nyinyi mnamuabudu yeye''
Hayo sio maneno yangu nenda kasome Quran 41:37
Hivyo mnaposema waislamu tunaabudu mwezi tunawashangaa sana!!!

Labda tukukumbushe pengine umesahau, au waswahili husema 'nyani halioni kundule'
Wanaopaswa kuulizwa ni wale wanaoabudu SUN-DAY
Siku za jumapili kama hamuabudu jua mnaenda kumuabudu nani?
Kuna andiko lolote katika bible linaoamrisha watu kwenda nyumba za ibada SUN-DAY??????

rosemarie hilo swali nimekuuliza wala sitaki majibu ( kwani najua hauna), baki na dini yako nasi tuachie dini yetu!
ONE LOVE!
mi mkristo ila keep it up nmekukubali
 
Back
Top Bottom