Ramadhan Special Thread

Ramadhan Special Thread

Nani Anawajibika Kufunga


Maulamaa wamekubaliana kufunga ni wajibu kwa mwenye akili timamu, Baleghe, mwenye afya na mkazi wa mji. Tukiongezea wanawake waliotwaharika na hedhi na nifasi.

Kwa wale ambao Swawm si wajibu juu yao ni wale ambao hawana akili timamu, hawajabaleghe.


Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) amesema:

“Kalamu (kurekodiwa ‘amali) imeinuliwa (hairekodi) kwa watu watatu: anayepatwa na usingizi mpaka aamke, mtoto mpaka afike umri wa kubaleghe, na aliorukwa na akili mpaka atakapopata akili timamu.”
[Hadiyth imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jami´, na. 3513 na Imerikodiwa na Abu Daawuwd].


Ama kwa wale wasioweza kufunga ni kutokamana na maneno Yake Allaah:

ﻓَﻤَﻦ ﺷَﻬِﺪَ ﻣِﻨﻜُﻢُ ﺍﻟﺸَّﻬْﺮَ ﻓَﻠْﻴَﺼُﻤْﻪُ ﻭَﻣَﻦ ﻛَﺎﻥَ ﻣَﺮِﻳﻀًﺎ ﺃَﻭْ ﻋَﻠَﻰ ﺳَﻔَﺮٍ ﻓَﻌِﺪَّﺓٌ ﻣِّﻦْ ﺃَﻳَّﺎﻡٍ ﺃُﺧَﺮَ


“Basi atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu, au yuko safarini (akafunga baadhi ya siku); basi (akamilishe) idadi (ya siku anazotakiwa kufunga) katika siku nyinginezo.

” [Suwratul-Baqarah 02: 184].


Ikiwa mgonjwa au msafiri atafunga basi inawatosheleza, ama wakichukua ruhsa ya kula hapo wameondolewa uzito. Ama wakiamua kufunga kwa kuwa wanataka kufunga hapo pia wako sawa.
 
Asalam alyekum Ndugu zangu katika imani, Mwezi mtukufu wa ramadhani ni mwezi wa toba kwetu waislam hivyo tunatakiwa tuzidishe unyenyekevu kwa Allah na tuombe rehma na maghufira kwa mole wetu mlezi wa viumbe vyote.Ndugu zangu waislam tusisahau kutoa sadaka na zakka ili tupate thawabu.Tusimame sana usiku kwa sasa na dua pia tusome sana Quran tukufu.Eeh mola wetu tunaomba utufanyie wepesi
 
Uzuri Wa Kutekeleza ´Ibaadah Ya Kufunga Mwezi Wa Ramadhaan


Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anhu) alimsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) akisema:

“Yeyote atakayefunga mwezi wa Ramadhaan kwa Imani na kutarajia malipo kutoka kwa Allaah basi Allaah Atamsamehe madhambi yake yote yaliyopita.” [Imeripotiwa na Al-Al-Bukhaariy na Muslim, An-Nasaaiy na Ibn Maajah].

Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema tena, alimsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) akisema:

“Allaah amesema: “Kila ‘Amali ya mwanaadam ni yake yeye mja Wangu ila Swawm. Ni yangu Mimi na mimi ndiye Nitakayemlipa mja Wangu.”


Swawm ni kinga.

Itakapofikia siku mmoja wenu amefunga ajiepushe na kufanya kitendo cha jimai na mabishano na watu. Na yeyote atakayetaka kupigana naye basi amwambie “Mimi nimefunga.” Naapa kwa jina la Allaah, Harufu inayotoka katika mdomo wa mwenye kufunga ni nzuri kwa Allaah kuliko harufu ya Misk. Kwa Mwenye kufunga ana furaha mbili: Furaha anapofungua Swawm yake na furaha pale atakapoonana na Mola Ameridhika kwa kufunga kwake.”
[Imeripotiwa na Al-Al-Bukhaariy na Muslim na An-Nasaaiy]


Sahl ibn S’ad (Radhiya Allaahu ´anhu) alimsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) akisema:

‘’Peponi kuna mlango unaitwa Ar-Rayyaan. Wale wenye kufunga wataingia peponi kupitia lango huu siku ya Qiyaamah na hakuna mwengine atakayepita katika mlango huu ila (wafungaji).

Itaambiwa: ‘’Wako wapi waliokuwa wakifunga?” Watasimama na watapita katika mlango huu na watakapomalizika kuingia wote (wafungaji) utafungwa na hakuna mwengine atakayepita hapo tena.“
[Imeripotiwa na Al-Al-Bukhaariy na Muslim, At-At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na An-Nasaaiy].
Jazakallah kheir
 
Ni kupi bora: Kutofunga au Kufunga?


Ikiwa mgonjwa au msafiri hawatoona tabu yoyote katika kufunga, basi kufunga kunapendekezwa. Ama wakikhofia kupata tabu kutokamana na kufunga, basi hapo kutofunga kunapendekezwa.

Abu Sa’iyd al-Khudriy ameelezea:

‘’Tulikuwa vitani na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) wakati wa Ramadhaan. Wengine katika sisi walikuwa wamefunga na wengine walivunja Swawm zao.

Wale waliofunga hawakuwaona waliovunja Swawm zao kuwa wako makosani na waliokula pia hawakuwaona waliofunga kuwa wako na makosa. Waliona wenye uwezo wa kufunga (walifunga) na hilo ni jambo zuri. Na ambao hawakuweza kufunga walivunja Swawm zao kwa udhaifu wa kufunga (hawakufunga) na hili pia ni jambo zuri.’

’ [Imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Sunan At-At-Tirmidhiy na. 574. Pia imerikodiwa na Imaam Muslim].


Ushahidi wa wanawake wasio Twahara kuwa hawafungi ni Hadiyth ya Abu Sa´iyd ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) amesema:


’’Je, si kwa kesi kwamba anapopatwa na damu yake ya mwezi, haswali wala hafungi? huo ni upungufu katika Dini yake.

’’ [Imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy, katika Mukhtaswar Swahiyh Al-Al-Bukhaariy na. 951. Imerikodiwa na Imaam Al-Al-Bukhaariy].


Ikiwa mwanamke asiyo Twahara atafunga basi swawm yake haikubaliki kwani katika masharti ya kukubalika swawm ya mwanamke ni awe katika Twahara. Mwanamke pia itamlazimu alipe siku alizokosa kufunga. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:


“Tulipokuwa tukipatwa na siku zetu za ada wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) tuliamrishwa kulipa Swawm za siku tuliokosa kufunga na hatukuamrishwa kulipa Swalah tulizokosa.

’’ [Imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Sunan At-Tirmidhiy na.630. Imerikodiwa na Imaam Muslim, Abu Dawuud, At-Tirmidhiy na An-An-Nasaaiy].


itaendelea....!
 
Mwezi Wa Ramadhaan Unathibitishwaje Kuonekana Kwake?


Mwezi wa Ramadhaan unathibitishwa kuonekana kwake na mtu mmoja mwenye kujulikana kwa ukweli na kumcha kwake Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) au kwa kutimiza siku thelathini za mwezi wa Sha’abaan.

Ibn ´Umar amesema watu walikuwa wakitafuta kuandama kwa mwezi. nikamjulisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) kuwa mimi nimeuona mwezi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) akafunga na akaamrisha watu wafunge.
” [Hadiyth Swahiyh. Angalia Kitaab I’rwa al-Ghaliyl na. 908 na Imeripotiwa na Abu Daawuwd].


Ikiwa mwezi haukuandama, kwa sababu ya kufunikwa na mawingu au kwa sababu nyingine basi hapo mwezi wa Sha’abaan utatimizwa kwa siku thelathini kama alivyoripoti Abu Hurayrah katika Hadiyth iliyo hapo juu.

Lakini mwezi wa Shawwaal unatangazwa kuonekana kwa mashahidi wawili.’ ´Abdur-Rahmaan bin Zayd bin Al-Khattwaab amesema:

“Nilipokuwa nikikhutubia siku ambayo ni ya shaka (kama mwezi wa Ramadhaan kama umekwisha ama la), nikasema: “Nilikaa na Maswahaba zake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) nikawauliza wao. Wakaniambia mimi kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) alisema:

‘’Fungeni kwa kuonekana mwezi na fungueni kwa kuonekana mwezi na tekelezeni ´Ibaadah ya Hajj kwa haki zake. Ikiwa kuna mawingu basi timizeni siku thelathini. Na Ikiwa Waislamu wawili watachukua kiapo kwa kuonekana kwa mwezi basi fungeni na mfungue kwa kushuhudia kwao mwezi.’’
[Hadiyth Swahiyh. Angalia Kitaab cha Shaykh Al-Albaaniy, Swahiyh al-Jamiy’ Asw-Swaghiyr na. 3811. Pia Imeripotiwa na Imaam Ahmad na An-Nasaaiy bila kipande kinachosema ‘’Waislamu wawili.’’].


Mtawala wa Makkah, Al-Haarith bin Hatwiyb amesema:

“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam) alituambia sisi tekelezeni ´Ibaadah ya Hajj kwa haki zake munapouona mwezi. Na ikiwa hamkuuona mwezi lakini mashahidi wawili wa kuaminika wakishuhudia kwa kuona mwezi tunatekeleza ´Ibaadah ya Hajj kutokana na ushahidi wao.’’

[Hadiyth Swahiyh angalia Shaykh Al-Albaaniy, Swahiyh Sunan Abiy-Daawuwd, na. 205. Imeripotiwa na Abu Daawuwd].


Tukiangalia ripoti mbili hizi,
’’Ikiwa waislamu wawili watachukua kiapo kwa kuona mwezi, basi fungeni na fungueni’’ katika Hadiyth ya Abdur-Rahmaan bin Zayd na:
‘’Na ikiwa hamkuuona mwezi lakini watu wawili wenye kujulikana kwa ukweli wakasema wameuona mwezi tunatimiza haki za ´Ibaadah ya Hajj kutokana na ushahidi wao.’’ katika Hadiyth ya Al-Haarith wanaonyesha kwa kutilia mkazo, kuwa haifai kuanza kufunga au kumaliza kufunga kutokamana na ushahidi wa mtu mmoja pekee. Juu ya hilo, tangu kuanza kwa kufunga imeondolewa uzito kutokana na ushahidi (uliotolewa hapo juu), inawacha suala la kumaliza kufunga, ambalo halina ushahidi kwamba linatoshelezwa kwa ushahidi wa mtu mmoja pekee.

Huu ni ufupi wa mjadala unaopatikana katika Kitabu ‘Tuhfah Al-Ahwadhiy’ [Mjalada wa 3, uk. 373-3749].


Tanbihi: Ikiwa mtu atauona mwezi yeye peke yake, hafungi mpaka watu wafunge na hamalizi kufunga mpaka watu wamalize kufunga kama ilivyoripotiwa na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anhu), kwamba amesema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa Sallam):


‘’Swawm (kufunga) ni siku ambayo watu wanafunga. Na kumaliza kufunga ni siku ambayo watu wanamaliza kufunga. Na kuchinja ni katika siku ambayo watu wanachinja.’’

[Hadiyth Swahiyh. Angalia Swahiyh Al-Jami’ Asw-Swaghiyr, na. 3869].

Imehifadhiwa na Imaam At-At-Tirmidhiy ambaye amesema:

‘’Baadhi ya Maulamaa wanaifasiri Hadiyth hii kwa maana:

“Kuanza kufunga na kumaliza kufunga kunatekelezwa na watu wote kwa pamoja na wakati mmoja.”
Ni kweli mkuu hapo ndipo kuna kuwaga na mtafaruku hapo
ila kikubwa hitirafu zipo zilikuwepo na zitakuwepo
Na ktk hitirafu kuna zinazo kubalika na zisizo kubalika.mf:Hitirafu isio kubalika kuna watu wana dai Mitume inaendelea ,Baada ya Muhammadi swalla allah alayhi wasallam alikuja Mwingine (Mirriza Ghuram Ahmedy) n.k. hizi hazikubaliki

Hitirafu ya Mwezi ni hitirafu inayo kubalika kikubwa yapaswa kufunga kutokana na ulivyo amina sio kwa kumuhufia mtu fulani au nyumbani wao wanaanzaga basi na mm nitaanza kwa kuhufia nyumbani.au sianzi kwa kuhufia nyumbani au mtu fulani .Siai Tunafunga kwa ajili ya Allah .
 
Ni kweli mkuu hapo ndipo kuna kuwaga na mtafaruku hapo
ila kikubwa hitirafu zipo zilikuwepo na zitakuwepo
Na ktk hitirafu kuna zinazo kubalika na zisizo kubalika.mf:Hitirafu isio kubalika kuna watu wana dai Mitume inaendelea ,Baada ya Muhammadi swalla allah alayhi wasallam alikuja Mwingine (Mirriza Ghuram Ahmedy) n.k. hizi hazikubaliki

Hitirafu ya Mwezi ni hitirafu inayo kubalika kikubwa yapaswa kufunga kutokana na ulivyo amina sio kwa kumuhufia mtu fulani au nyumbani wao wanaanzaga basi na mm nitaanza kwa kuhufia nyumbani.au sianzi kwa kuhufia nyumbani au mtu fulani .Siai Tunafunga kwa ajili ya Allah .
ni kweli kabisa na ndomana tunasisitizwa tusome ili kuijua dini yetu ,maana ukisoma hutoburuzwa wala hutofauta mkumbo,
maana dini haiendeshwi kwa rai za mtu au kufata mkumbo ,

Unaposoma basi unajua unachokisimamia

Kukhtilafiana kupo na kulikuwepo ila hakumaanishi tufarakane
 
Hivi Ramadhan waislamu wanafunga au wanabadili muda wa kula? Na je mnaposema Ramadhan ni mwezi wa kutenda mema je miezi mingine ni ya kutenda mambaya? Asalam Allykum
Wanafunga...
Kubadili mda ina maana tungekua tunakunywa chai saa moja usiku,,lunch saa saba usiku afu dinner sa 12 asubuhi.
Tunafunga na kufungua kwa kuzama na kuchomoza kwa jua?!

Miezi mingine sio ya kutenda mabaya,ila mwezi Wa ramadhan matendo mema yanalipwa Mara kumi zaidi kulinganisha na miezi mingine.

Una swali lingine umeacha kiporo tukujibu?
 
Back
Top Bottom