Hechy Essy
JF-Expert Member
- Mar 30, 2023
- 640
- 2,413
- Thread starter
- #521
1. Hapana, hapo kila kimoja kina kazi yake...ukiweka vyote inakuwa bora zaidi ila ukishindwa kuweka vyote kutokana na hali ya uchumi, weka mkandaMkuu naomba kufahamu yafatayo;
1. Unapoweka Jamvi unakuwa huna haja ya kuweka mkanda?
2. Kipi naweza kuskip katika namna ya kupunguza gharama lakini nikawa nimelinda ubora ktk haya;
a/kuweka Jamvi
b/ kuweka mkanda
c/ kuweka lenta 2, nikaweka moja tu ile ya juu.
2. Inategemea na uimara wa tofali pamoja na aina ya udongo. Kuna tofali flani zilikuaga zinatumika sana miaka ya nyuma (zilikuwa zinatengenezwa kwa kutumia saruji, mchanga na vikokoto vidogo vidogo).
Enzi hizo gari la tofali likifika site, tofali zilikuwa zinamwagwa tu kama mchanga na hazivunjiki (baada ya hapo ndio zinaanza kupangwa)
Hizi tofali zilikuwa imara sana tofauti na hizi za sasa ambazo zinatengenezwa kibiashara zaidi (cement kidogo, mchanga mwingi). Watu wengi wakitumia hizi tofali kwenye msingi, huwa wanaskip kuweka mkanda kwa sababu uimara wake unakaribiana na uimara wa zege yenyewe, kama utatumia hizi tofali za kileo nakushauri uweke mkanda hata wa nondo 3 ili kujiweka salama zaidi
Upande wa kuweka jamvi, kama udongo wako uko vizuri na uchumi wako hauruhusu unaweza ukajaza kifusi chenye mawe mawe na kukishindilia vizuri, baada ya hapo ukamwaga zege nyembamba