Niache Nteseke
JF-Expert Member
- Apr 29, 2020
- 2,162
- 2,616
Sub.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
unamaanisha udongo mkavu wakujengea?Katika ubandikaji wa tiles sakafuni, kitaalam inatakiwa kwanza uweke timanzi (hii ni kama gauge ya kufanya sakafu yako iwe na usawa mmoja chumba kizima), kisha mwaga udongo (mortar) pote chumba kizima, shindilia vizuri kwa kufata timanzi zako kisha ndipo uanze kuweka tiles zako kwa kutumia udongo mwepesi na mwembamba (hii itakuwa ni kama gundi ya kati ya sakafu na tiles)
Ukitumia mfumo huu, tiles zako zitakuwa imara na hutosikia tiles zako zikilia kama ngoma unapotembea juu yake kwa sababu tiles zimelala katika udongo ambao umeshindiliwa vizuri. Lakini pia kwa mfumo huu, kazi ya ubandikaji inakuwa rahisi zaidi kwa sababu unazilaza tiles zako katika sehemu ambayo umeshaifanyia levelling tayari.
Mafundi wengi wanamwaga udongo kwa tiles moja moja, na kuigonga tiles ikiwa juu ya huo udongo kutafuta level kitu ambacho kinafanya udongo usambae pembeni na wakati mwingine kuacha uwazi ambao baada ya muda itafanya tiles zianze kulia kama ngoma. Na kingine mfumo huu wa kumwaga udongo kwa tiles moja moja unatumia muda mwingi, na uimara wake ni wa mashaka
Ikiwa unahitaji Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Hiii inatukumba arusha na sijui solution nzur ni ipi mm kama mjenzi mtarajiwa.. udongo wa huku unatanuka na kusinyaa ukitanuka unapasuka hapo solution n nnMoja kati ya vitu vya kuzingatia kabla hujanunua kiwanja ni pamoja na aina ya udongo uliopo k atika hicho kiwanja
Udongo mzuri ni ule wenye asili ya kichanga ambao wenyewe hauna kawaida ya kutanuka na kusinyaa pindi kunapotokea mabadiliko ya kiwango cha maji badala yake huruhusu maji kuzama chini kirahisi kutokana na nafasi kubwa iliyopo kati ya punje moja na nyingine
Udongo wa mfinyazi sio mzuri katika ujenzi, una kawaida ya kutanuka na kusinyaa hivyo husababisha nyufa katika kuta
Baada ya hapo, ni kibandika tiles kwa udongo mwepesi. Huo udongo mkavu tayari umeshashindiliwa na kuwekwa level.unamaanisha udongo mkavu wakujengea?
Amejichanganya mkuu take it easyIla mkuu na wewe siku nyingine tumia tafsiri ya vipimo kama fundi kweli! Utasemaje urefu unakuwa mdogo kuliko upana? Inakuwaje 3.7m unaita urefu na 4.3m unaita upana?
Nisaidie namba yako Afsa.Bila shaka ulikuwa unamaanisha apartment sivyo? Tuwasiliane mkuu, mimi nadesign nyumba ya aina yoyote kwa kufata maelekezo ya mteja (na kumshauri pia, mana kuna muda mteja anatoa maelekezo ambayo yanakinzana na aspects of designing)
Oya mwamba achana nae watu km hao wapi wengi sn ambao kazi Yao ni kukatisha watu tamaa Sasa ukianza kuangaika nao utakikuta muda mwingi unamaliza Kwa ajili Yao badala ya kufikiria ya msingi na kufanya kazi zako. Kwa upande wng nakuunga mkono ndg endelea kutuelimisha, tupo wengi ambao hatujui mengi au lolote kuhusu ujenziSawa ndg, All in all jaribu kuheshimu kitu kinachompatia mtu riziki hata kama kwako hakikufai kwa maana ni Mungu Mwenyezi ndiye aliyempangia apate riziki kupitia kitu hicho. Haijalishi una mali kiasi gani, una cheo gani maisha ni mapito hivyo hakuna sababu yoyote inayoruhusu binadamu kudharauriana. Ramani yangu ni takataka sawa, lakini kuna elimu pia naitoa hapo mbali na kuuza ramani (hata hiyo pia haikufai?)
Tupo pamoja mkuu, uwepo wao ndio unatupatia changamoto ya kupambana zaidiOya mwamba achana nae watu km hao wapi wengi sn ambao kazi Yao ni kukatisha watu tamaa Sasa ukianza kuangaika nao utakikuta muda mwingi unamaliza Kwa ajili Yao badala ya kufikiria ya msingi na kufanya kazi zako. Kwa upande wng nakuunga mkono ndg endelea kutuelimisha, tupo wengi ambao hatujui mengi au lolote kuhusu ujenzi
Vent pipeNi muhimu sana kuweka vent pipe katika mfumo wa maji taka ili kuzuia harufu kurudi ndani ya nyumba ( kwa wale wanaotumia vyoo vya ndani)
Unaweza ukaweka T connector kwenye kile kipande cha bomba kinachounganisha P-trap na chemba halafu ukaweka bomba refu kuelekea juu (usisahau kuweka na mfuniko wake ambao unakuwa na matundu pembeni ili mvua inaponyesha maji yasiwe yanaingia kupitia hilo bomba) nkipata picha nitawaletea ili iwe rahisi kueleweka
Pia unaweza ukaweka vent pipe na kwenye karo la choo ili kupunguza joto na pressure ya hewa iliyopo ndani
Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Sent using Jamii Forums mobile app
Zina kazi kubwa sana, upepo ukipita na kutokea upande wa pili inaondoka na joto na kuregulate jotoRekebisha hizo vent za huko kwenye paa, hazina kazi yoyote zaidi ya kuozesha ceiling board
Kokoto za duara hazifai kutumika kwenye ujenzi; au nasema uongo ndugu zangu?Katika uchanganyaji wa zege, ukitumia kokoto ambazo umbo lake ni la duara utatumia cement mifuko michache ukilinganisha na kokoto zingine (kwa ujazo wa zege na uwiano (ratio) unaofanana), hii ni kwa sababu nafasi iliyopo kati ya kokoto na kokoto (void space) katika hizi kokoto za duara ni ndogo kulinganisha na kokoto zingine
Hoja yako haina mashiko, labda ungeeleza msingi wa nini.Baada ya kupanga mawe (hardcore) katika msingi, inashauriwa umwage mchanga mwingi ndipo uje umwage zege la jamvi (oversite concrete). Hii ni kwa sababu unapopanga mawe, ile nafasi iliyopo kati ya jiwe na jiwe zege inaweza isipite kwenda kuziba hizo nafasi. Kama hiyo sakafu itapata mgandamzo mkubwa (mfano gari ikapita) inaweza kusababisha hiyo sakafu kutitia kutokana na uwepo wa uwazi (matundu) uliopo chini yake
Kama unahitaji ramani za kitaalamu na makadirio ya vifaa vya ujenzi tuwasiliane
Std nyumba haipaswi kupungua ngazi 4 yaani msingi uinuke futi 2 au 60cm kutoka usawa wa ardhiHii nyumba ni kwa ajili ya maeneo yenye slope au foundation inapandishwa juu hata kwenye tambarare ili zipatikane hizo ngazi?
Bacteria wanaochakata uchafu hawahitaji oxygen ili kuishi au bacteria wa kwako ni special?Kitaalam haishauriwi maji ya jikoni (kuoshea vyombo n.k) kwenda ktk shimo la choo kwa sababu maji ya jikoni yana mafuta ambayo hutengeneza tabaka juu ya maji na kuzuia hewa isiingie chini. Umeng'enyaji wa uchafu uliopo ktk shimo la choo hufanywa na bacteria ambao hao bacteria wanahitaji hewa ili waendelee kuishi.
Utakapomwaga maji ya jikoni kwenye karo la choo, lile tabaka la mafuta litafanya bacteria wakose hewa na kupelekea kufa hivyo karo litakuwa linajaa haraka (mara kwa mara) kutokana na kwamba umeng'enyaji wa uchafu haufanyiki au unafanyika kwa kiasi kidogo kutokana na uchache wa hewa na bacteria uliopo chini.
Vinginevyo itabidi ujenzi wa septic tank (lile shimo la pembe nne) uweke buffer wall kati kati (Mechanism ya Buffer wall nitaielezea siku nyingine, subscribe huu uzi uendelee kupata dondoo mbali mbali kuhusu ujenzi)
Kwa mahitaji ya ramani, makadirio au ushauri tuwasiliane tafadhali +255(0)624068809
Wasomi wa kileo utawajua tu.Boss vipi kuhusu apparent ya chumba kimoja master, on the side kina laundry room
Na kina sehemu multi purpose (jiko sitting place na dining place)