Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

unamaanisha udongo mkavu wakujengea?
 
Hiii inatukumba arusha na sijui solution nzur ni ipi mm kama mjenzi mtarajiwa.. udongo wa huku unatanuka na kusinyaa ukitanuka unapasuka hapo solution n nn
 
Oya mwamba achana nae watu km hao wapi wengi sn ambao kazi Yao ni kukatisha watu tamaa Sasa ukianza kuangaika nao utakikuta muda mwingi unamaliza Kwa ajili Yao badala ya kufikiria ya msingi na kufanya kazi zako. Kwa upande wng nakuunga mkono ndg endelea kutuelimisha, tupo wengi ambao hatujui mengi au lolote kuhusu ujenzi
 
Ni muhimu sana kuweka vent pipe katika mfumo wa maji taka ili kuzuia harufu kurudi ndani ya nyumba ( kwa wale wanaotumia vyoo vya ndani)

Unaweza ukaweka T connector kwenye kile kipande cha bomba kinachounganisha P-trap na chemba halafu ukaweka bomba refu kuelekea juu (usisahau kuweka na mfuniko wake ambao unakuwa na matundu pembeni ili mvua inaponyesha maji yasiwe yanaingia kupitia hilo bomba) nkipata picha nitawaletea ili iwe rahisi kueleweka

Pia unaweza ukaweka vent pipe na kwenye karo la choo ili kupunguza joto na pressure ya hewa iliyopo ndani

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tupo pamoja mkuu, uwepo wao ndio unatupatia changamoto ya kupambana zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vent pipe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati mwingine mkanda wa zege sio lazima uwekwe nondo za juu na za chini, ni vile tu kwa sababu ringi hatizoweza kukaa kwa kufunga nondo za chini pekee ndio maana unakuta zinafungwa nondo chini na juu.

Wengine hutumia nondo za milimita 12 upande wa chini, na juu wanatumia nondo za milimita 10 hivyo inapunguza gharama (hii ni kama mkanda wako ni singly reinforced beam).

Katika mkanda, zege huwa inakabiliana na compressional forces upande wa juu, na nondo huwa inakabiliana na tension forces upande wa chini hivyo kama zege uliyotumia inaweza kukabiliana yenyewe na compressional force bila msaada wa nondo, basi hakuna haja ya kuweka nondo mbili juu na nondo mbili chini, ni bora ukaweka nondo tatu chini, nondo moja juu ukatumia ringi za pembe tatu ambapo mkanda wako utakuwa imara zaidi kuliko mtu aliyefunga nondo mbili juu, nondo mbili chini. (Hapa nazungumzia singly reinforced beam)

Upande wa Doubly reinforced beam, mkanda nondo zake zinafungwa chini na juu na hii hutumika pale zege yenyewe inashindwa kukabiliana na compressional forces hivyo inahitaji msaada wa nondo upande wa juu. Katika doubly reinforced beam, nondo za juu zinakuwa na kazi ya kubeba mzigo pia lakini kwa singly reinforced beam, nondo za juu zinakaa kwa ajili ya kushikilia ringi

Utajuaje kama mkanda wako ni singly au doubly reinforced beam? Hapo sasa ni mpaka mahesabu yafanyike (tuishie hapo kwa leo)

Ramani, Makadirio, Ushauri tuwasiliane



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kokoto za duara hazifai kutumika kwenye ujenzi; au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hoja yako haina mashiko, labda ungeeleza msingi wa nini.
Nyumba gani gari itaingia au kukanyaga?

Ongelea godauni labda
 
Bacteria wanaochakata uchafu hawahitaji oxygen ili kuishi au bacteria wa kwako ni special?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…