Rangi ya jezi Taifa Stars?

Sibonike

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2010
Posts
17,296
Reaction score
18,027
Leo Taifa Stars wapo uwanjani mechi ya kirafiki na Malawi.
Wamevaa jezi nyeupe na strip ya blue lakini sehemu kubwa ni nyeupe. Japo sio lazima sana, nchi nyingi huchukua rangi kwenye bendera ya nchi. Hii nyeupe wametoa wapi? Ukiacha bendera kuna nembo au alama nyingine ya taifa walikotoa?
Au utashi wa viongozi wa TFF tu?
 
Halftime Malawi wapo mbele moja bila. Utadhani ndiyo wenyeji.
 
Mechi iliyopita walipewa sifa sana,naona leo sifa zimewalevya
 
Mechi iliyopita walipewa sifa sana,naona leo sifa zimewalevya
Leo wamelewa kweli. Malawi tuliowafunga Sauzi sio hawa. Walikuwa wana test Vijana. Leo imekuwa proper team tunahenya
 
Watoto wamelegea balaa, timu nzima anaeshughulika kiume ni samatta peke yake
 
Hii timu imekua kama Changudoa, kila mtu anapiga bao tu. Yaani atujawahi kufurahia football kwenye nchi hii. Kila siku majonzi tu, dah!
 
Kwanza nipeni matokeo ya World Cup, timu yetu inaenda Russia au la?
 
Mpango wa Malinzi kubadili jezi za timu ya Taifa ndio unaendelezwa na hawa wa sasa? Basi hakuna mabadiliko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…