Ras Mtimanyongo: Kimsingi Kariakoo ni eneo la sokoni (Wamachinga) tangia Uhuru, Wafanyabiashara kwao ni Samora na Kitumbini

Ras Mtimanyongo: Kimsingi Kariakoo ni eneo la sokoni (Wamachinga) tangia Uhuru, Wafanyabiashara kwao ni Samora na Kitumbini

Swali langu nauliza wale jamaa wanawapeleka wapi?

Kwa Dar es salaam ni maeneo gani ya wazi wametengewa kufanya shughuli zao?
Waende masokoni wakalipie vizimba kama wafanyavyo wafanyabiashara wengine, walipe na kodi pia! Watengewe maeneo kwa umaalumu gani walionao? Ni kundi gani hapa TZ limepangiwa eneo maalumu la kufanyia mambo yao? Wao ni vilema hadi wadekezwe hivi?
 
Hawakudanganywa mkuu....

Ardhi ni mali ya dola....na biashara hufanyiwa juu ya ardhi.....dola imeamua waondoke kwa faida pana ya kila mmoja wetu......

#Zama Mpya
Wakati dora inawaruhusu ilikuwa sio kwa faida pana.
 
Waende masokoni wakalipie vizimba kama wafanyavyo wafanyabiashara wengine, walipe na kodi pia! Watengewe maeneo kwa umaalumu gani walionao? Ni kundi gani hapa TZ limepangiwa eneo maalumu la kufanyia mambo yao? Wao ni vilema hadi wadekezwe hivi?
Uchaguzi ukikaribia mtawatafuta tu.
 
Msanii Ras Mtimanyongo anasema kamwe Wamachinga hawawezi kuondoka Kariakoo kwa sababu ndio sokoni kuanzia nchi hii ijitawale.

Mtimanyongo anasema Wafanyabiashara kwao ni Samora zamani Independence avenue na Kitumbini na ndio maana hadi sasa hata vijiduka vya kariakoo ni vya ujanja ujanja tu.

Mtimanyongo anasisitiza kuwa kifuatacho kiwe TRA kusaka maghala ya hao wajanja wajanja wa kariakoo huko Vingunguti na Buguruni kama kweli wanataka kukusanya kodi.

Mungu ni mwema wakati wote!
Mshamba wewe!
Tupe picha ya mmachinga mwaka 1965.
Siye tulikuwepo.
Political expediency ya kuruhusu anarchy ndio imesababisha kuungua hata hili soko jipya- its no accident.
 
Dola iko kwa ajili ya ustawi wa Tanzania bwashee....

Awamu hii imeamua hivyo mkuu .....ubishi wa nini kaka?!!

Tuiendee kinyume dola yetu pendwa?!!
Ina maana serikali haina mipango ya kudumu kuhusu wamachinga kwamba kila awamu na mipango yake.
 
Sio wapiga kura hao, wapiga debe tuuu
Dah leo wamekuwa wapiga debe wakati mliwauzia hadi vitambulisho. Ila mimi siwatetei ni ujinga wao.

 
Ina maana serikali haina mipango ya kudumu kuhusu wamachinga kwamba kila awamu na mipango yake.
Serikali na wananchi ni lazima tushirikiane katika kuyatafuta majawabu......

Ni siku za karibuni CHIFU MKUU HANGAYA alipoongelea TOZO ZA MIAMALA YA SIMU kuwa zinakwenda KUJENGA NA KUBORESHA BARABARA ZIELEKEAO mashambani ili kuzidi kukiinua KILIMO alipingwa na baadhi yetu wananchi.......
 
Back
Top Bottom