Mkuu Kubwajinga,
1. Lowassa, alirudishwa kwenye power na Mkapa, Mwalimu akiwepo, sasa anakuwaje good kwa uwaziri wa Mkapa, lakini sio u-pm wa muungwana? It was toka aliporudishwa na Mkapa, lakini uzuri ni kwamba sasa hayupo tena na ndio hivi tunalilia watinge kwenye mikono ya sheria.
{Mkuu wa Medani za kivita, Nakukumbusha kuwa awamu zote zilijenga msingi wa kuzalisha vijana wao,Benjamin ni product ya siasa za awamu ya kwanza ktk anga za kitaifa,naamini baadhi ya majina ambayo Mwinyi alipewa na Mwalimu alipokuwa anaondoka Ben alikuwamo na wengi wa aina hiyo. Hoja yangu hapa kaka ni kurejea kauli ya Alhaj Mwinyi alimuomba Ben asiwatupe Jakaya na Edward ,mzee huyu alitamka hadharani ktk mkutano mkuu ulitoa rais wetu wa awamu ya Tatu,kama kuna mwenye kumbu.interms of rejea ya speech ya Mzee Mwinyi baada ya Mkapa kuteuliwa mtakutana na ombi hilo rasmi, na ninapenda kukubaliana nawe kuwa Mwalimu hakumkutaka Edward tena ktk siasa za kitaifa na Mkapa alimridhisha kwa kumuweka pembeni ktk baraza lake la kwanza ila kuna fact ingine kuwa Edward na kaka yangu Guninita hawakukubaliana na kushindwa kwa JK na walionyesha vitendo ambavyo wakuu na wapambe wa mteule hawakuridhishwa navyo,kuna taarifa kuwa Edward na Guninita walilia kama watoto pale Chimwaga na kujikuta wakitamka yasiyotakiwa na wenzao hali hiyo ilimgharimu Edward na Guninita kukihama chama chetu baada kusakamwa na wapambe na yeye kutokuwa tayari kukubali matokeo hata yale ya nje ya ukumbi, Edward alionyesha ukomavu kwa kuwa mtulivu sana bungeni na daima aliegemeza hoja kuisaidia serikali,mfano issue ya Million 900 ya Mrema alikuwa ni Edward aliyejenga hoja za kitaalam bungeni mpka kuwashawishi wabunge wengi kufikia hatima ya skendo ile,1997 Ben alifanya marekebisho makubwa ktk baraza lake na hapo waliingia Masilingi,Edward na Iddy, ni kipindi hiki Ben alichoonyesha muelekeo wa maridhiano ya kichama kwa kurejesha pande zote ktk serikali yake na ni hapo Alhaj Mwinyi alipoona Ben amekumbuka ombi lake tena ktk kipindi julius yuko hai. }
2. Ninaamini 100%, kuwa muungwana hakuyajua ya Chenge na hela za nje zilizosemwa kwa mara ya kwanza last week na gazeti la Guardian la UK, na kumfanya Chenge ajiuzulu this week, sasa kama rais alikuwa anyajua hayo Chenge asingejiuzulu, kama vile Mkapa, alivyomtetea Ngasongwa.
{Dkt Ngasongwa ni mmoja wa wahanga wa ripoti ya jaji Warioba's report + Majungu ya akina Msola SUA + wajenzi wa fitina za siasa kwa kuzingatia wizara aliyokuwemo, lakini Dkt Ngasongwa alifahamu mchezo aliofanyiwa mapema, licha ya wazee wengi wa mkoa wa Morogoro na chamani kumshawishi kutojiuzuru yeye aliandika barua ya kujiuzuru wakati rais yuko nje ya nchi na alipofika aliikuta mezani na alipomwita na kumhoji Dkt Ngasongwa kwa kujiamini kuwa alipakaziwa kwa makusudi alishikilia msimamo huo wa kujiuzuru na kama ataonekana amehusika yuko tayari kuachia nafasi yake ya Ubunge , Mh.Rais kama anamuamini basi ni vema akubali kujiuzuru kwake na uchunguzi pia,na umma upewe taarifa juu ya kile alichotuhumiwa nacho,uchunguzi ulifanyika baada Ben kukubali kujiuzuru kwake na kuamuru afanyiwe uchunguzi,matokeo Tume ya maadili ya viongozi,hawa jamaa wanaohukumiwa hapa sasa wote walijiridhisha kuwa Dkt Ngasongwa hakuhusika na ufisadi wowote, sasa pengine hapa mkuu wa medani utusaidie ni vipi mkapa anafananishwa na issue ya Chenge kwa JK,ni ufafanuzi tu au ni ule msimamo wa kwanza athibitike then hatua zinafuatia ?}
Halafu, Besides the ishu hapa ni mkurugenzi wa usalama, sio Chenge, maana kuna ishu ya Chenge kuleee, kama ni proof basi labda wewe unayo inayosema kuwa rais alijua, au?
3. Mimi binafsi bado ninampa rais, the benefit of the doubt kwa sababu so far haijatokea ishu inayomgusa moja kwa moja, lakini itakapotokea kama kawaida yangu itakuwa ni kumkoma nyani!