Rasimu ni maoni sio Katiba

Rasimu ni maoni sio Katiba

Ni rahisi sana kusema unapounda.majimbo unataka.kuwasogegezea karibu Wananchi huduma lakini kuna huduma zilokaribu na Wananchi kuliko Serikali za Mitaa?

Kumbuka tu kwamba hakuna kubwa.ambalo Seeikali ya Majimbo.itafanya dhidi ya Serikali Kuu kuliko serikali za mitaa ambazo zina ukubwa mdogo na kata chache zaidi lakini ndiko Ubadhilifu mkubwa unatokea.
Now, imagine unaongeza wigo kuwa na Majimbo mathlan Shinyanga, Mwanza, Geifa, Mara na Bukoba! Halafu uunde serikali yake na Bunge lake! Patakuwa na wabunge wa jimbo hilo pia Wabunge wawakilishi Bunge la JMT. Fedha hizi za matumizi haya makubwa zitatoka wapi?

Ikiwa.mimi napingana na Seeikali 3, halafu unanambia acha 3 tuunde Majimbo ina maana unaunda Seeikaki Isopungua 6 zenye viongozi na Wabunge wake kisha bado wa Kitaifa!

Kwani Mikoa na Wilaya zina kasoro zipi? Bila shaka ni UTUMISHI yaani hakuna UWAJIBIKAJI. Kama haya yanakosekana na WATU ni walle wale tulonao huoni kwamba tatizo ni WATU sio UTAWALA?

Sisi watumishi ndio tatizo hata kama.tutagawa nyumba kwa nyumba shida zitabakia palepale. Tatizo ni TAASISI zeru haziwajibiki. La kufanya ni.kutafuta mbinu ziwajibike. Kila mmoja wetu aogope kuiibia serikali. Na ndivyo wenzetu waliweza kufanikiwa kwa sababu kila mtumishi ana wajibu na nishani ya kazi.
- Sisi ni Kanyaga Twende, tumechelewa mno..
Naanza kuwa na mashaka sana na wewe..
Serikali za mitaa unazoongelea hapa ni institutions za kipuuzi sana hapa Tanzania. Hazina uwezo wowote na hazitofautiani na zile za wakati wa ukoloni. Kimsingi serikali ndo inataka iwe hivyo.. kazi yake ni unyampala dhidi ya wananchi.. hakuna aliyezichagua, zinawajibika kwa aliyeziteua na si vinginevyo. Tunataka mkuu wa mkoa awajibike kwa wananchi moja kwa moja na si kwa Rais aliyemteua.
Hii ndo maana halisi ya kuwa wenye nchi ni wananchi
 
Mkuu hata hizi serikali za Majimbo zina viongozi wa Serikali Kuu ndani wakishughulika na mambo ya Jamhuri (federal) Ujue unapounda Majimbo kuna mambo mtafanya ya Serikali Kuu na mengine yataendeshwa na Serikali za Majimbo ni sawa kabisa na Muungano Wa Tanganyika na Zanzibar.

Kuwa na Serikali za Mitaa (halmashauri) ni bora zaidi kulingana na muungano wetu, kinachotakiwa ni kuboresha usimamizi na utekelezaji (check and Balance) yaani iwe ada kuhakikisha fedha inayotumika inalingana na matokeo.

Hakuna Jimbo (state) ambalo Halina Mkuu wa Mkoa au wilaya kwa majina yao ambao husimamia shughuli za Serikali Kuu (federal). Tena wao mambo yasokuwa ya Muungano huwa machache sana hususan huduma za kijamii kama vile Elimu, Afya, usafiri, ajira, barabara n.k haya ndio hujitegemea lakini sii mambo makubwa, pia hata katika hayo kuna fungu la matumizi hutoka Serikali Kuu.
Nahisi niliyochangia awali kiujumla hujayaweka kwenye context hapa.

Nahisi umeshafanya maamuzi ya jinsi ungependa muundo wa uendeshaji wa nchi uwe kwenye katiba mpya - sawa nii haki yako,
  • kama ni kweli basi mimi ninaishia hapa kuhusu muundo wa majimbo na hata muungano
  • kama si kweli, basi niombe tuzungumzie specific aspects za Majimbo na Muungano. Na napendekeza tuanze na definitions. mf. unaposema Jimbo, Serikali, Muungano, etc unamaanisha nini?
 
Nahisi niliyochangia awali kiujumla hujayaweka kwenye context hapa.

Nahisi umeshafanya maamuzi ya jinsi ungependa muundo wa uendeshaji wa nchi uwe kwenye katiba mpya - sawa nii haki yako,
  • kama ni kweli basi mimi ninaishia hapa kuhusu muundo wa majimbo na hata muungano
  • kama si kweli, basi niombe tuzungumzie specific aspects za Majimbo na Muungano. Na napendekeza tuanze na definitions. mf. unaposema Jimbo, Serikali, Muungano, etc unamaanisha nini?
Hapana mkuu nimezingatia sana, tofauti ni moja tu. Mimi nimeeleza faida na hasara za kila mfumo tunaotaka kuutumia na kwa nini nchi nyingine hufanya tofauti na sisi ambao tunataka kuiga vitu basipo kujua hasara zake.

Kisha hata rasimu ya Warioba au Pendekezwa haikuwahi kutueleza faida na hasara za mifumo yake! Mimi nimeeleza hapa walonisoma wanaelewa napingana kwa sababu zipi. Haina maana Serikali za Majimbo ni mbaya laa hasha isipokuwa ziliundwa kwa sababu tofauti.

Wenzetu hayo majimbo wameyatumia kutokana na nchi zao zilikuwa na ubaguzi, kuna tofauti za Makabila kwa mipaka na walikuwa maadui, hivyo walipopata Uhuru wa kuwa nchi moja walilazimika kuyaacha majimbo kwa sababu walishindwa kuondoa Ukabila. Hata Serikali zao ziliendelea kutumia Machief, Wafalme na Watemi kujadiliana.

Ulaya na Marekani, majimbo haya kila moja lilikuwa na Uhuru wake, wakaamua kuungana kuunda nchi moja yaani majimbo yaliunda serikali kuu ya pamoja mwanzo haikuwepo.

Sisi tayari tuna Jamhuri (Federation) tumesha unganisha WATU lakini leo hii tunataka kujigawa kwa sababu za KIUCHUMI.

Hii ndio hofu nayojaribu kuijenga hapa na naamini fikra hizi zinatokana na Umaskini. Familia maskini hugombania mirathi wakasahau kuwa wao ni familia moja ya uzawa mmoja.

Kibaya zaidi tutakuwa nchi ya kwanza duniani kukata majimbo baada ya kuwa na Jamhuri (Federation). Yaani baada ya kuunganisha watu, imefika muda wa kuwatenganisha hao watu kwa sababu za Kiuchumi!

Sasa tujiulize, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ndio ulotuunganisha WATU wa Bara na Visiwani japo bado kuna kero zake lakini haya ni Majimbo mawili yameungana.

Halafu tunataka kuikaka Bara iwe na utawala wa Majimbo! Wakati tuna Mikoa na Wilaya na Serikali za.mitaa hiyo Zanzibar itabakia kama kitu gani? Itakuwa NCHI au JIMBO? Na ipi nafasi yake ndani ya Tanzania ya Majimbo? Au ndio tutauvunja Muungano kwanza!

Kama nilivyosema awali, mimi nitakuwa upande wa pili wa sarufi, unapoleta hoja naipopoa kwa hasara zake kadri navyoelewa ili wewe mwandishi utupe madini zaidi, utueleze faida ya kuwa na MAJIMBO ilihali tuna Serikali za Mitaa ambazo ziko karibu zaidi na Wananchi. Tarizo letu sisi ni UWAJIBIKAJI tuna ubinafsi sana. Je, Majinbo yataondosha Ubinafsi na kuleta Uwajibikaji? Mimi sidhani majimboo ni muarobaini.

Usihamaki mkuu, mjadala hautaki hasira isipokuwa HOJA nazisoma zote tena huzisoma vizuri tu, kisha hutazama umuhimu na manufaa yake. Penye kupongeza napongeza na penye walakin najibu kwa HOJA.
 
Wanaowaza serikali mbili na tatu kwa upande wangu nawaona wakiangalia zaidi madaraka zaidi ya umoja.

Ndio maana nasema kama kweli tunataka tuwe kitu kimoja tuwe na serikali 1,TRA iwe na nguvu hadi Zanzibar.

Tuungane kiroho zaidi yaani tuwe wa1 kabsa hizi serikali mbili au tatu zimekaa kibaguzi sana na zina manung'unuko mengi sana ambayo kila upande unaona hautendewi haki.

Kwa upande wangu nawaona Wazanzibar ni ndugu zangu kabsaa na nataka tuwe na serikali 1 kusiwe na ubaguzi wa ukinunua kitu Zanzibar unakuwa kama vile umekinunua Uganda.
Labda nikuulze hivi. Mambo ya Tanganyika ni yapi hayatekelezwi leo? na Je, kuwepo Serikali 2 kinachopungua hapo ni kipi kama sii jina la Tanganyika maana kama ni utawala wa Mawaziri tunao mpaka manaibu na manispaa.

Labda nikupe fununu kidogo, tu. Nchi zilogawana majimbo zjna Serikali kubwa sana kwa maana ya Watumishi wake. Mfano, tukiwa na Serikali 3 hiyo Tanganyika italazimika kuwa na Wabunge 428 badala ya 214 ili.kuwakilisha majimbo yao kwenye Bunge la JMT na Bunge la Tanganyika. Tutalazimika kugharamia viongozi wote ngazi ya Tanganyika na ngazi ya Kitaifa.

Kwa nchi maskini kama yetu kesho tutadai Majimbo maana mikoa ya Kanda ya ziwa au kusini watapata hoja kwa sababu 2. Kwaza utajiri wao wa dhahabu au gas! Na pili Kujitawala! Hili neno kujitawala hubeba ubaguzi ulonakshiwa. Je, tuko tayari kupambana na hali hiyo ikitokea?

Kama nilivyosema. Lengo la kuunganisha NCHI hizi mbili ni WATU kama vile wazazi wawili wanapofunga ndoa basi kizazi chao huwa na Ubin mmoja. Tukianza kusema kuna Qatanzania na Wazanzibar, Itakuja Wasukuma na Wazaramo maana unarudisha kuitazama zaidi mipaka badala ya Watu..
Mkuu suala la mgombea binafsi ni suala nzuri kwa mantik hii
Mgombea binafsi hatapaswa kuwajibishwa na wana nchi moja kwa moja iwapo sheria itakuwa thabiti .




Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Naanza kuwa na mashaka sana na wewe..
Serikali za mitaa unazoongelea hapa ni institutions za kipuuzi sana hapa Tanzania. Hazina uwezo wowote na hazitofautiani na zile za wakati wa ukoloni. Kimsingi serikali ndo inataka iwe hivyo.. kazi yake ni unyampala dhidi ya wananchi.. hakuna aliyezichagua, zinawajibika kwa aliyeziteua na si vinginevyo. Tunataka mkuu wa mkoa awajibike kwa wananchi moja kwa moja na si kwa Rais aliyemteua.
Hii ndo maana halisi ya kuwa wenye nchi ni wananchi
Hapo utakuwa unanikosea maana sijasema mapungufu wa hizi Serikali zetu za mitaa bali ni mfumo ambao upo dunia nzima, huko nje wanaziita county.

Na hizo county ni Halmashauri kama sisi isipokuwa wenzetu viongozi wao walochaguliwa na Wananchi wanawajibika kwa Wananchi. Sisi bado kabisa madiwani wanawajibika kwa Vyama vya Siasa. Ukikataa kufuata chama unafutiwa Uanachama na hivyo unapoteza Udiwani au Ubunge.

Sheria hii kwenye Vyama vya Siasa lazima irekebishwe ifutwe kwa sababu tunaziona Halmashauri zikitumikia vyama na ndio.maana migogoro haiishi, unakuta mpaka wenyeviti wa vyama wanashirikishwa. Mbunge au diwani akiteuliwa na Wananchi, jnatakiwa chama kisiwe na mamlaka juu yake isipokuwa katika utekelezeaji wa ahadi na ilani ya chama.

Na Kama sikosei mwanzo wa Muundo wa Serikali za mitaa walikuwa wakikusanya fedha wao karika.mfukonwa Hlmashauri. Ikatokea kuwa fedha zilikuwa zinapotea, hazijulikani wala zilivyotumika. Ubadhilifu na ufisadi ulikuwa mkubwa toka juu hadi chini.

Nakumbuka report ya CAG wakati wa JK ilikuwa mbaya sana kwenye Seeikali za Mitaa. Halmashauri nyingi zilipata hati chafu, ikabidi warekebishe muundo ili fedha sasa zikusanywe Hazina kisha ndio zipelekwe huko.

Na ndipo Chadema walipokuja na sera ya Majimbo wakiamini ndio muarabaini wa kuzibana Halmashauri lakini binafsi yangu nasema siku zote tatizo ni sii mfumo bali ni WATU.

Tatizo la UTUMISHI katika urasimu, Ukiritimba, Ubadhilifu, Ufisadi, uzembe na nidhamu hayawezi kuboreshwa kwa kujenga mfumo ama kuboresha taasisi isipokuwa ni kusimika sheria, kanuni nantaratibu zinazowabana WATUMISHI kuwa Accountable na Responsible kwa Wananchi.

Watanzania hatutaki kuwekewa Sheria, hatutaki kanuni ama taratibu zinazotulazimu kuwajibika. Hatutaki kupangiwa maisha, muda, hatuwezi kujituma kufanya kazi bila kusimamiwa. Tuna majibu ya mkato hata katika kusimamia maisha ya Wananchi. Hili sio tatizo la kimfumo bali ni Watu wenyewe.

Hesabu zetu ni saa ngapi unaondoka kazini na kiasi gani mfukoni. SISI NDIVYO TULIVYO..
 
Naomba kutoa tu tahadhari kuhusu huu mjadala ulioanzishwa na anayeitwa Mkandara.

Mkandara anaibeza rasimu ya Warioba akidai ilizingatia maoni ya baadhi tu ya wananchi na si wote. (Milioni 60!)

Hivi Mkandara atatumia njia gani kuwafikia hao wananchi wote anaodai hawakupata fursa ya kutoa maoni?

Swali la pili anamwakilisha nani katika hii harakati ya kuiponda rasimu ya Warioba na kupinga baadhi ya maoni yaliyomo?

Swali la tatu anabeza rasimu ya Warioba kwa niaba ya nani? Kama ni kikosi kazi nanusa harufu isiyo na afya hapa!

Hiki kikosi ambacho kinatumbua mabilioni ya kodi zetu, kiliteuliwa na mpiga zumari au kilichaguliwa na wananchi?

Tuwe makini sana na hizi ghilba za CCM, hiki kikosi hakina tofauti na kamati yoyote ile ya CCM. Eti rasimu ya Warioba haifai!
Kuna shida gani kama rasimu ya warioba ikiangaliwa upya, kulingana na tulipofika sasa? Kwani Judge warioba aliandika msaafu?
 
Suala la elimu kwa viongozi wetu na wawakilishi wa wananchi lazima liwe kigezo cha kutaka kupata nafasi za umma. Watu ambao hawawezi kujua nini kimeandikwa kwenye makaratasi, halafu wasome na waamue kwa ajiri ya watu wote sidhani kama Taifa linanufaika nao.
 
Back
Top Bottom