Rasimu ni maoni sio Katiba

Rasimu ni maoni sio Katiba

Katiba mpya inabidi kuhusisha watu wanaojitambua na sio wanasiasa nadhani tungewapa watu makini wafanye hiyo Kazi na sio kuwapa wana-siasa hiyo Kazi


Mabadiliko Makubwa yanabidi kuanzia Katika kuondoa Mfumo wa Kuondoa mambo ya Ajabu Kama Ccm na washirika wake .
 
Mkuu sibishani na wewe. Rasimu ya Warioba ninayo na imejadiliwa sana wakati wa Bunge la Katiba. Kuchangia hapa ni mawazo tofauti na yalokuwepo huko. Nisome toka mwanzo wa mada hii upate wewe kunielewa.

Rasimu ya Warioba inapendekeza serikali 3 na ndio kisa cha bunge kuvunjika. Hata mimi sikubaliani nayo! Sasa unataka mpaka niiweke rasimu hapa ndio utaweza kuchangia ?
Ok sawa,

Wewe unapendekeza ziwe ngapi?
 
Hilo Baraza la wazee ambalo umeliita Senate mbona lita ongeza gharama kwa umma hasa kwenye matumizi ya kodi kulipa mishahara, posho nk mbona unataka kumpa mwananchi mzigo wa Kodi na wakati huo huo ukisema uendeshaji wa serikali 3 utakuwa na gharama ?

Yapi yatakuwa manufaa ya Baraza hilo katika taifa ukizingatia tuna Bunge na Baraza la mawaziri ?
Baraza la wazee kwa mtazamo wangu sio lazima liwe na mwakilishi wa kila wilaya kwa sababu ya ukubwa wake. Wapo wazee wenye sifa, ama kutokana na utumishi wao sehemu mbalimbali, au kutokana na uwezo wao wa kiuongozi katika mahala husika.
Kuwa na double check sio kitu kibaya. Umuhimu wake uwe kuangalia na gharama za uendeshaji wa hilo baraza pia
 
Baraza la wazee kwa mtazamo wangu sio lazima liwe na mwakilishi wa kila wilaya kwa sababu ya ukubwa wake. Wapo wazee wenye sifa, ama kutokana na utumishi wao sehemu mbalimbali, au kutokana na uwezo wao wa kiuongozi katika mahala husika.
Kuwa na double check sio kitu kibaya. Umuhimu wake uwe kuangalia na gharama za uendeshaji wa hilo baraza pia
Njia yoyote ile itumike muhimu wawe watu wenye misimamo ya katika kusimamia na kuilinda UTAWALA BORA.

Hatuwezi kuijenga nchi yetu kwa kutegemea viongozi ambao hawawajibiki na hakuna chombo kinacho watazama kwa makini mienendo yao.

Malalamiko mengi ya Wananchi ni tabia na matendo ya baadhi viongozi ambao wakisha pewa dhamana hujiona hakuna mtu wa kuwagusa hata kama wameitia hasara Serikali katika kusaini mikataba mibovu, dhulma za ardhi, mali zao zihakikiwe kama wanavyodai. Kifupi, Miiko na Maadili ya viongozi yawe na chombo kitakacho wawajibisha.
 
Njia yoyote ile itumike muhimu wawe watu wenye misimamo ya katika kusimamia na kuilinda UTAWALA BORA.

Hatuwezi kuijenga nchi yetu kwa kutegemea viongozi ambao hawawajibiki na hakuna chombo kinacho watazama kwa makini mienendo yao.

Malalamiko mengi ya Wananchi ni tabia na matendo ya baadhi viongozi ambao wakisha pewa dhamana hujiona hakuna mtu wa kuwagusa hata kama wameitia hasara Serikali katika kusaini mikataba mibovu, dhulma za ardhi, mali zao zihakikiwe kama wanavyodai. Kifupi, Miiko na Maadili ya viongozi yawe na chombo kitakacho wawajibisha.
Ni kweli kabisa. Kwa sasa hatuna pakuwawajibisha maana kuna loopholes nyingi. Balance and check is critical for good governance.
Especially kama kutakuwa na vyombo vingine vyenye nguvu na vinavyosimama kisheria, kuangali utendaji wa serikali na watu wake, bila kuwa compromised
 
Ili kukomesha rushwa na kulindana, vyombo vinavyopambana na rushwa vilindwe kisheria kuanzia muundo wake, na utendaji wake wa kazi.
Ni ngumu sana kwa sasa kupambana na rushwa na matumizi mabaya ya mali za umma sababu baadhi ya wanaoweza kuwa washiriki, ni watu wenye madaraka na wenye uwezo wa kuwadhibiti katika ufanisi wa kutekeleza majukumu yao. Kama kweli tunaipenda nchi yetu, lazima tuchukie rushwa maana inadumaza maendeleo. Na lazima tuweke ndani ya sheria mama namna ya kudhibiti, kupambana na hata kuwashughulikia wala rushwa, bila kujali vyeo na madaraka yao
 
Miradi ya maendeleo katika mkoa kuwepo sio sababu ya wakuu wa mikoa waliochaguliwa na wananchi wasiisimamie simply because hawakuchaguliwa na Rais!! Aferall usimamizi wa miradi ya maendeleo ni kazi ya watendaji, unfortunately our civil servants who are supposed to be apolitical serving any party in power have been politicized by ccm; kiasi kwamba watendaji hao ni wanachama wa vyama vya siasa! Watendaji wote wa civil service wizarani na mikoani WOTE wawe apolitical.

Kwanini Mkurugenzi awe mteule wa Rais badala ya kuwa part of the civil service; yote hii ilikuwa ni kuhodhi madaraka kwa mtu mmoja and in the process tunazalisha CHAWA ambao hawaleti maendeleo bali wizi!! Miradi ya Serikali kuu na miradi ya Halmashsuri yote inatumia fedha za wananchi sioni sababu kwani usimamizi wake uwe tofauti ; hii yote ni kuongeza gharama za usimamizi na kuongeza nafasi za matumizi mabaya ya fedha!

Baraza la Senate linaweza kua na ufanisi tu pale upatikanaji wa hao Senators utakuwa kwa utashi wa wananchi kwa kuwachagua bila mizengwe ya vyama vya siasa.

Katiba ilenge kupunguza madaraka ya Rais ambae hivi sasa ni omnipotent; moja sapo ni hilo la kuteua Regional na District commissioners!! Msiwe kwenye hiyo kamati kutetea status quo!!! Nchi hii imaeharibiwa sana na current arrangements.
Nakubaliana na wewe kwenye teuzi za rais kwa hawa Wakurugenzi wa taasisi na mashirika ya Umma. Badala ya teuzi wafanyiwe interview na boards aidha kupitia wizara inayohusika.

Lakini tatizo la Tanzania mkuu wangu ni michongo. Ukiwapa watu madaraka wanachonga mzinga! Watapeana ajira wenyewe ili mchongo usimame. Yaani Tanzania ni pasua kichwa, rahisi sana kusema tumpunguzie rais madaraka lkn hayo.madaraka ulompunguzia unampa nani?

Atakaye pewa atafanya mabaya zaidi. Elewa hoja sii kuwa na nguvu kubwa bali Uwajibikaji.

Leo wanao ongoza ufisadi ni Wakurugenzi. Watu wenye elimu na kila sifa ya ufanyaji kazi lakini mzigo! Nani wa kuwasimamia?

Ukisema Mkuu wa Mkoa asiteuliwe na rais tueleze sababu isiwe tu unataka kumpunguzia madaraka lakini hakuna impact katika ufanisi wa kazi.

Isitoshe hawa ni reflection yetu sisi sote. Mtu akiwa bench ni mpole, mtu wa watu, siku anateuliwa sii yule tena utadhani kakabidhiwa rungu.

Mwisho niseme tu, rais anapounda serikali yake, huteua watu ambao wataifanya kazi kwa niaba yake. Wakuu wa Mikoa na Wilaya ni sehemu ya idara zake.
 
Nakubaliana na wewe kwenye teuzi za rais kwa hawa Wakurugenzi wa taasisi na mashirika ya Umma. Badala ya teuzi wafanyiwe interview na boards aidha kupitia wizara inayohusika.

Lakini tatizo la Tanzania mkuu wangu ni michongo. Ukiwapa watu madaraka wanachonga mzinga! Watapeana ajira wenyewe ili mchongo usimame. Yaani Tanzania ni pasua kichwa, rahisi sana kusema tumpunguzie rais madaraka lkn hayo.madaraka ulompunguzia unampa nani?

Atakaye pewa atafanya mabaya zaidi. Elewa hoja sii kuwa na nguvu kubwa bali Uwajibikaji.

Leo wanao ongoza ufisadi ni Wakurugenzi. Watu wenye elimu na kila sifa ya ufanyaji kazi lakini mzigo! Nani wa kuwasimamia?

Ukisema Mkuu wa Mkoa asiteuliwe na rais tueleze sababu isiwe tu unataka kumpunguzia madaraka lakini hakuna impact katika ufanisi wa kazi.

Isitoshe hawa ni reflection yetu sisi sote. Mtu akiwa bench ni mpole, mtu wa watu, siku anateuliwa sii yule tena utadhani kakabidhiwa rungu.

Mwisho niseme tu, rais anapounda serikali yake, huteua watu ambao wataifanya kazi kwa niaba yake. Wakuu wa Mikoa na Wilaya ni sehemu ya idara zake.

Hivi muundo wa sasa unakidhi mahitaji ya wakati huu? Tunahitaji DC na group lake, RC na group lake, RAS, wakurugenzi wa wilaya etc?
Kazi zao haziingiliani? Au tunahitaji watu wote hao? Ninaamini katika kufanikisha maamuzi kwa wakati na kwa muda unaostahili. Sio kila jambo lina haraka na sio kila jambo linahitaji kuchelewa sababu ya mlolongo mrefu wa kutoa maamuzi. Pengine muundo wa kazi za serikali kwenye Tamisemi nao unaweza kupewa jicho, kama utaingiliana na jukumu la muundo wa sheria mama inayokusudiwa. Msisitizo ukiwa ni uwajibikaji tena kwa wakati
 
Naomba kutoa tu tahadhari kuhusu huu mjadala ulioanzishwa na anayeitwa Mkandara.

Mkandara anaibeza rasimu ya Warioba akidai ilizingatia maoni ya baadhi tu ya wananchi na si wote. (Milioni 60!)

Hivi Mkandara atatumia njia gani kuwafikia hao wananchi wote anaodai hawakupata fursa ya kutoa maoni?

Swali la pili anamwakilisha nani katika hii harakati ya kuiponda rasimu ya Warioba na kupinga baadhi ya maoni yaliyomo?

Swali la tatu anabeza rasimu ya Warioba kwa niaba ya nani? Kama ni kikosi kazi nanusa harufu isiyo na afya hapa!

Hiki kikosi ambacho kinatumbua mabilioni ya kodi zetu, kiliteuliwa na mpiga zumari au kilichaguliwa na wananchi?

Tuwe makini sana na hizi ghilba za CCM, hiki kikosi hakina tofauti na kamati yoyote ile ya CCM. Eti rasimu ya Warioba haifai!
 
Naomba kutoa tu tahadhari kuhusu huu mjadala ulioanzishwa na anayeitwa Mkandara.

Mkandara anaibeza rasimu ya Warioba akidai ilizingatia maoni ya baadhi tu ya wananchi na si wote. (Milioni 60!)

Hivi Mkandara atatumia njia gani kuwafikia hao wananchi wote anaodai hawakupata fursa ya kutoa maoni?

Swali la pili anamwakilisha nani katika hii harakati ya kuiponda rasimu ya Warioba na kupinga baadhi ya maoni yaliyomo?

Swali la tatu anabeza rasimu ya Warioba kwa niaba ya nani? Kama ni kikosi kazi nanusa harufu isiyo na afya hapa!

Hiki kikosi ambacho kinatumbua mabilioni ya kodi zetu, kiliteuliwa na mpiga zumari au kilichaguliwa na wananchi?

Tuwe makini sana na hizi ghilba za CCM, hiki kikosi hakina tofauti na kamati yoyote ile ya CCM. Eti rasimu ya Warioba haifai!
Kwanza kabisa niombe samahani kama nimekukwaza wewe na wengine wote mnaoipitisha Rasimu ya Warioba bila kuzingatia kuwa ni Rasimu hiyo hiyo ilotukwamisha kuipata Katiba Mpya.

Yale yalikuwa maoni ya Wananchi sio Katiba hivyo hata sisi tuna wajibu wa kuchangia iwe yanakubalika au laa lakini tumekuwa sehemu ya kutoa mawazo yetu.

Ikisha mkuu kukwama kwa rasimu hakukutokana na maelezo yangu isipokuwa walopewa dhamana ya kuipitia na kuichambua hawakufikia maamuzi ya pamoja, upande wa pili wakidai kuna mapungufu ambayo hayakuzingatiwa.

Sote tulimsikia Rais Mstaafu JK na baadhi hata wajumbe wa bunge lile wakitupiana maneno ya kashfa na dharau.

Sikuhusika katika matukio yote yale na wala hakuna pahala nimeidharau rasimu ya Warioba isipokuwa naelewa sehemu ambazo zilileta utata baina ya Wajumbe wa Bunge lile.

Kwa kutambua hivyo nimezitaka kwa uchache ili sisi tuzijadili kwa kina badala ya kuunga mkono hoja au maoni ambayo huelewi kama yanalenga misingi ya UTU wetu na UTAWALA BORA.

Na kikubwa zaidi, kwa sababu tunategemea kuwepo mchakato mpya utakao fanyika hivi karibuni, nimeona sisi wqna JF, tutumie fursa hii kuweza kusikia maoni ya wengine ambao aidha hawakupata nafasi ya kuchangia ama mawazo yao yaliachwa kwa sababu hayakupata asilimia kubwa.

Naamini wapo Watanzania wengi tu ambao wanaweza kusaidia upatikanaji wa Katiba Mpya kwa maoni yao haswa sehemu ambazo zilileta mtafaruku Mkubwa baina ya wajumbe wa Bunge maalum la Katiba.

Mfano, chukulia Serikali 3 ilikwamishwa wakati ile Pendekezwa ikipitisha Serikali 2. Katika mvutano huo sidhani kama tulipewa faida nanhasara za serikali 3 au 2 zaidi ya maoni tu.

Mimi binafsi maoni yangu ni serikali 1 na sababu nimezitaja japo nafahamu HAIWEZEKANI kutokea. Lakini pia nimeeleza kwa nini siafiki serikali 2 au 3. Kwa kufanya hivyo, sifanyi dharau yoyote ya mawazo ya Wananchi wengine walopendekeza mifumo hiyo.

Ahsante
 
Asante ndugu Mkandara..
Mosi: tufahamu kuwa nchi yetu haina maendeleo kutokana na kukosa falsafa sahihi ya uongozi au kukosa uongozi kabisa.
Pili: Hoja yangu iko kwenye MUUNDO WA SERIKALI.
Muundo uliopo una mapungufu makubwa sana. Ni muundo usio tofauti na wa kikoloni ambapo muundo huo ulihakikisha maslahi ya mkoloni yanalindwa na si ya mwananchi. Hali kadhalika, muundo uliopo ni wa kuhakikisha maslahi ya serikali ndiyo yanalindwa. Ukiangalia vema, utakuta ofisi ya raisi inawakilishwa hadi ngazi ya chini kabisa kwenye kitongoji/mtaa.
Ningetamani kwenye katiba mpya, maslahi ya mwananchi yapewe heshima na nafasi inayostahili. Iko hivi:

Mwananchi aongozwe na mtu aliyemchagua. Maana yake, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi hawatakiwi tena kwenye katiba/sheria zitakazotungwa kutokana na katiba mpya.
Uongozi wa mikoa uchaguliwe na wananchi, kuwe na mabunge kila mkoa. Kila mkoa uwe na taasisi kamili zenye uwezo stahiki mfano elimu, mahakama, ardhi, kilimo, afya, maji, nishati, polisi nk.
Wabunge wa wananchi katika mikoa wawe kweli wamechaguliwa kihalali.

Nguvu ya ofisi ya Rais iishie kwenye wizara.. mfano sasa hivi raisi anateua viongozi wapatao elfu tatu au zaidi, hii siyo sahihi hata kidogo, ndo maana machawa wameongezeka.
Bunge la jamhuri lipunguziwe nguvu na ukuwa, pia lijikite katika masuala ya msingi kama kusimamia serikali kuu na masuala ya kimataifa. Yaliyobaki yatashughulikiwa na mabunge madogo ya mikoa.

Nitarudi tena, asante
 
Rasimu ya Warioba ipo, wewe kama mwananchi una mawqzo gani tofauti katika mapwndekezo ya sura ibara zike. Kumbuka sisi wote tuna mitazamo tofauti na hatukubaliani kwa mengi na ndio maana rasimu ile ilisukumwa uvunguni. Je, leo hii tutawezaje kupata suluhu katika Mambo yale yale yalokwama mwanzoni pasipo hata kuwafikia Wananchi.
Shida ilikuwa ya maccm. Kimsingi ile rasimu ya Warioba ilikuwa njema sana.. shida ni kwamba ilihatarisha maslahi ya genge la wahalifu eachache liitwalo ccm. Baasi. Leo hii tungekuwa mbali sana
 
Asante ndugu Mkandara..
Mosi: tufahamu kuwa nchi yetu haina maendeleo kutokana na kukosa falsafa sahihi ya uongozi au kukosa uongozi kabisa.
Pili: Hoja yangu iko kwenye MUUNDO WA SERIKALI.
Muundo uliopo una mapungufu makubwa sana. Ni muundo usio tofauti na wa kikoloni ambapo muundo huo ulihakikisha maslahi ya mkoloni yanalindwa na si ya mwananchi. Hali kadhalika, muundo uliopo ni wa kuhakikisha maslahi ya serikali ndiyo yanalindwa. Ukiangalia vema, utakuta ofisi ya raisi inawakilishwa hadi ngazi ya chini kabisa kwenye kitongoji/mtaa.
Ningetamani kwenye katiba mpya, maslahi ya mwananchi yapewe heshima na nafasi inayostahili. Iko hivi:

Mwananchi aongozwe na mtu aliyemchagua. Maana yake, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi hawatakiwi tena kwenye katiba/sheria zitakazotungwa kutokana na katiba mpya.
Uongozi wa mikoa uchaguliwe na wananchi, kuwe na mabunge kila mkoa. Kila mkoa uwe na taasisi kamili zenye uwezo stahiki mfano elimu, mahakama, ardhi, kilimo, afya, maji, nishati, polisi nk.
Wabunge wa wananchi katika mikoa wawe kweli wamechaguliwa kihalali.

Nguvu ya ofisi ya Rais iishie kwenye wizara.. mfano sasa hivi raisi anateua viongozi wapatao elfu tatu au zaidi, hii siyo sahihi hata kidogo, ndo maana machawa wameongezeka.
Bunge la jamhuri lipunguziwe nguvu na ukuwa, pia lijikite katika masuala ya msingi kama kusimamia serikali kuu na masuala ya kimataifa. Yaliyobaki yatashughulikiwa na mabunge madogo ya mikoa.

Nitarudi tena, asante
Unapo zungumzia Muundo una maana ya Muungano wenyewe au Serikali ngapi? Maana elewa Tanzania ni nchi ndogo ukilinganisha na nchi zingine kwa maana ya Ukubwa wake na watu wake.

Nchi nyingine marais hana mamlaka hayo kwa sababu bchi hizo zina muungano wa nchi zaidi ya mbili yaani kuna states!

Na ukitazama mamlaka ya rais wa nchi hizonutayaona madogo kwa sababu baadhi ya kazi zake zinafantwa na viongozi wa States hizo. Kwa hiyo unadhani kwamba rais wao hana mamlaka makubwa kumbe ukitazama kiongozi wa State husika ana mamlaka makubwa juu ya wananchi wake.

Sisi rais wa JMT ni kama rais wa Bara zaidi maana Zanzibar ina rais wake. Mama Samia pamoha na kwamba ni rais wa JMT ni sawa kabisa na kuwa rais wa Bara kwa sabahu Bunge letu hujadili mambo yote ya Muungano na yasokuwa ya Muungano kwa Bara.

Binafsi niseme hivi, naweza kuunga mkono Serikali 2 japo naitaka 1 zaidi ya 3 kwa sababu Tumepunguziwa matumizi makubwa kwenye serikali 3. kama tungekuwa na serikali 3 ingetulazimu kuwa na ikulu 2. Kwanza ofisi ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( na watumishi wake) kisha tuna Ikulu ya rais wa Tanganyika (Bara) sijui makao makuu yake yangekuwa wapi! Double the expenses.

Hapa tunazungumzia mabilioni ya fedha kuhudumia ofisi hizi mbili wakati hizi serikali 2 tumeua ndege wawili kwa jiwe moja. Rais mmoja akihudumia ya JMT na Bara.

Haya bado upande wa Wabunge na Mawaziri nako gharama ingeongezeka maradufu kuhudumia serikali ya 3. Huwesi ongeza Serikali ati ukalubguza matumizi huo uongo. Watupe hesabu zake..

Najiuliza ni sababu gani haswa tunataka serikali 3? Huwq sipati jibu zaidi ya uhasama na fitna baina ya Watanzania wa Bara na Visiwani.

Infact wala sio Wananchi bali Wanasiasa wa siku hizi ndio huchombeza migogoro yote hii kugombania nafasi chache ya Uongozi zilizopo.

Leo Mama Samia kaingia na kaweka baadhi ya viongoI wa Bara na Visiwani katika Serikali yake, misifa inamwagwa! Zile kero ziko wapi? Nikagundua kumbe ni mtego hapa ni FURSA basi hakuna zaidi.

Kama lengo la Waasisi wetu ilikuwa kuunganisha WATU ambao kwa asili ni wamoja toka enI za Utawala wa Washiraz tena Mpaka Rwanda, Burundi na Kongo kwa nini sisi tusiwe mfano wa kqqnza kabisa Afrika kurudisha Mipaka yetu kama walivyoikuta Wakoloni?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unatumiwa sana kisiasa kututenganisha. Kwa nini na sisi tunakubali yaishe ili turudishe mila.na tamaduni za Watawala wetu?.

Maoni yangu mimi ni SERIKALI MOJA na ili tufanikiwe zaidi Zanzibar iwe freeport kama Dubai ambako hakuna tax kabisaaa isipokuwa kila kitu unachoweza kupata Dubai au China kinapatikana Zanzibar.

Daraja lijengwe baina ya Dar - Zanzibar ( kama inawezekana), Ukivusha mzigo wako Bara ndio unalipishwa kodi moja tu, na kodi hiyo inatufaidisha zote Bara na Visiwani.
 
Nikuulize, Unapotaka kuunda Majimbo nini haswa malengo yake? Tutafadikaje na majimbo hayo na zipi hasara zake!
Baadhi ya Malengo;
1 - ni kusogeza uwajibikaji wenye maana karibu zaidi kwa Wenye-nchi (Wananchi).
2 - kutenganisha majukumu, mipango ya maendeleo na utekelezaji wake, etc ya Kitaifa (yanayohusu Taifa zima) na ya kijimbo (Yanayohusu au Yaliyo na maana katika Jimbo)
3 - Kusaidia kupunguza mzigo mkubwa wa majukumu aliyonayo Raisi, kutoka majukumu ya sasa yanayohitaji Raisi mwenye uwezo wa "kiMungu" ili kutelekezeka ipasavyo, kwenda majukumu yanayoweza kutekelezeka na Bin-Adamu mwenye uwezo wa wastani na kuendelea.
4 - Kusaidia kupunguza madhara ya makosa yanayofanywa na viongozi wa Kitaifa ( na hata yatakayokua yanafanywa na viiongozi wa Kimajimbo.
5 - Kuipa Serikali ya Kitaifa/Kuu (Kwa kushirikiana na Serikali za Majimbo) wajibu na nafasi ya kutunga, kusimamia na kurekebisha Miongozo mbalimbali, ambayo itatumika kama Mahitaji ya kima cha chini katika upangaji na utekeleza wa shughuli za maendeleo nchi nzima.
6. N.K

Kama ikiwa nia ni Majimbo yajitegemee kiuchumi ina maana watumishi watakuwa answerable kwa kiongozi wao. Share ya mapato ya kodi itafanyikaje?
- Kuwe na mambo ya Kitaifa na mambo ya Kimajimbo. Watumishi watawajibika kwa wasimamizi wao. Ajira zao, Mishahara yao itatoka sehemu waliyo ajiliwa. Mfano mwalimu wa shule ya msingi A katika Jimbo A, atawajibika kwa Mwalimu mkuu wa shule hiyo, na kulipwa na Jimbo A. Mhasibu wa TCRA tawi la Jimbo A, atawajibika kwa Mhasibu-mkuu, makao makuu ya TCRA, na atalipwa mshahara kutoka serikali kuu.

- Mapato katika Majimbo yagawanywe, ili kiasi kibaki katika Jimbo na Kiasi kiende Serikali kuu.
Misaada ya maendeleo itafantikaje?
Lengo liwe kutotegemea misaada, huku tukiwa na nchi Tajiri kabisa. Hata hivyo, misaada huja kwa lengo fulani.
Misaada itumike kutegemea malengo ya misaada hiyo.
Pia kama lengo lake ni kugawana madaraka, fikiria ikiwa leo Serikali za mitaa zinaongoza kwa ubadhilifu wa fedha za miradi, itakuwaje tukiwa na Majimbo ambayo rais hana mamlaka nayo?
Itengenezwe miongozo ya kifedha itakayo hakikisha ubadhilifu unazuiwa kabla haujatokea, na Ukitokea miongozo irekebishwa kuhakikisha hautatokea tena.
Kama zamani miakanya 70 tulishindwa Madaraka mikoani ikawa shida mkulima kusafirisha mazao toka mkoa mmoja kwenda mwingine. Tukavunja mfumo ule, tumeleta Serikali za mitaa, nazo tumeshudia wananchi wakilalamikia tozo na ushuru. kwa nini turudie makosa? Kwa nini tusiandike Katiba inayo wajali Wananchi kuondoa urasimu huo?

Binafsi yangu naamini Majimbo yanaweza tokea Nigeria. Mifano ipo mingi kwa nchi za Kiafrika kugawanyika.kutokana na Majimbo. Kuanzia Ethiopia, Sudan, Somalia kote huko majimbo yameandamana na Ukabila. Kenya ni swala la muda tu.

Sisi tumeweza kufuta Ukabila na Udini kwa nini unataka mfumo ambao unaweza kurudisha hali ya hatari kwa usalama wa raia? Kama ya Zanzibar yanatushinda tunataka serikali 3 ili.kila.mtu na chake tutawezaje Majimbo?
  • Naamini, mfumo wa Majimbo hautakosa changamoto. Lakini faida zake zinahalisha, uthubutu wa kujikita katika kutatua changamoto hizo.
  • Tanganyika ina historia yake. Mfumo wetu wa Majimbo, utakone na hali, historia na mahitaji yetu.
 
Muungano wa Serikali 3 utawatenganisha WATU wa Tanganyika na Zanzibar. Hilo.nakuhakkkishia hata kabla halijapitishwa.

Kumbuka lengo halisi la Muungano wa nchi zetu ilikuwa Kuunganisha WATU wake. Kama tutaunda Serikali 3 ina maana tumekubali kila nchi ibebe msalaba wake. Hapo ndio utawasikia Watanganyika nao wakidai Wazanzibar warudi kwao! Hawa Wazazibar wanafuata nini, nao kule Wabara rudini makwenu. Trust me itatokea wala sii swala la kupigia ramli..

Wenzetu Ulaya, wameweza kabisa kuondoa Ukabila na Ukanda. Mwananchi mkazi wa NewYork au Texas regardless ya race au uzawa wote ni WAMAREKANI na kujitambulisha kama Wamarekani. (Am American) muulize unatoka wapi atasema USA.

Angalia UK kinachiwakeka pamoja ni nguvu ya dola tu lakini Wana ubaguzi ndani ya nchi zao na kuna under ground movements kudai kujigawa.

Na Sisi itakuwa hivyo hivyo, mimi Mtanganyika, mimi Mzanzibar maana tayari dalili zipo wazi machoni mwetu lakini hatutaki kuamini. Nakuhakikishia jina la Tanzania litapotea kabisa kama Tanganyika.

Nia na dhumuni la Katiba hii iwe kuutujenga katika UTANZANIA tuwe proud na nchi yetu badala ta kuchukia kuwa kuitwa Mtanzania.
  • Hata sasa kuna huo mgawanyo, kuna Wanzanzibar na (so-called) Watanzania Bara. Muungano wa serikali 3 utafasema, huyu Mtanzania Bara, ni Mtaganyika (pamoja na mambo mengine) - ni Muungano usio na unafiki.
  • Nafikiri, Watu wenye nia ya kuungana, wakiungana ni jambo zuri. Hatahivyo, Sidhani kama ni sahihi kuwalazimisha watu waungane.
  • Ni wazi kuwa Wazanzibar hawataki Tanganyika na Zanzibar ziungane kwa nchi moja (niko tayari kukosolewa kwa hili). Muungano tulionao sasa, hauitendei haki Tanganyika, ukiachana na mapungufu mengine, na ndio maana kunapendekezo la serilkali 3.
 
Baadhi ya Malengo;
1 - ni kusogeza uwajibikaji wenye maana karibu zaidi kwa Wenye-nchi (Wananchi).
2 - kutenganisha majukumu, mipango ya maendeleo na utekelezaji wake, etc ya Kitaifa (yanayohusi Taifa zima) na ya kijimbo (Yanayohusu au Yaliyo na maana katika Jimbo)
3 - Kusaidia kupunguza mzigo mkubwa wa majukumu aliyonayo Raisi, kutoka majukumu ya sasa yanayohitaji Raisi mwenye uwezo wa "kiMungu" ili kutelekezeka ipasavyo, kwenda majukumu yanayoweza kutekelezeka na Bin-Adamu mwenye uwezo wa wastani na kuendelea.
4 - Kusaidia kupunguza madhala ya makosa yanayofanywa na viongozi wa Kitaifa ( na hata yatakayokua yanafanywa na viiongozi wa Kimajimbo.
5 - Kuipa Serikali ya Kitaifa/Kuu (Kwa kushirikiana na Serikali za Majimbo) wajibu na nafasi ya kutunga, kusimamia na kurekebisha Miongozo mbalimbali, ambayo itatumika kama Mahitaji ya kima cha chini katika upangaji na utekeleza wa shughuli za maendeleo nchi nzima.
6. N.K


- Kuwe na mambo ya Kitaifa na mambo ya Kimajimbo. Watumishi watawajibika kwa wasimamizi wao. Ajira zao, Mishahara yao itatoka sehemu waliyo ajiliwa. Mfano mwalimu wa shule ya msingi A katika Jimbo A, atawajibika kwa Mwalimu mkuu wa shule hiyo, na kulipwa na Jimbo A. Mhasibu wa TCRA tawi la Jimbo A, atawajibika kwa Mhasibu-mkuu, makao makuu ya TCRA, na atalipwa mshahara kutoka serikali kuu.

- Mapato katika Majimbo yagawanywe, ili kiasi kibaki katika Jimbo na Kiasi kiende Serikali kuu.

Leo liwe kutotegemea misaada, huku tukiwa na nchi Tajiri kabisa. Hata hivyo, misaada huja kwa lengo fulani.
Misaada itumike kutegemea malengo ya misaada hiyo.

Itengenezwe miongozo ya kifedha itakayo hakikisha ubadhilifu unazuiwa kabla haujatokea, na Ukitokea miongozo irekebishwa kuhakikisha hautatokea tena.

  • Naamini, mfumo wa Majimbo hautakosa changamoto. Lakini faida zake zinahalisha, uthubutu wa kujikita katika kutatua changamoto hizo.
  • Tanganyika ina historia yake. Mfumo wetu wa Majimbo, utakone na hali, historia na mahitaji yetu.
Ni rahisi sana kusema unapounda.majimbo unataka.kuwasogegezea karibu Wananchi huduma lakini kuna huduma zilokaribu na Wananchi kuliko Serikali za Mitaa?

Kumbuka tu kwamba hakuna kubwa.ambalo Seeikali ya Majimbo.itafanya dhidi ya Serikali Kuu kuliko serikali za mitaa ambazo zina ukubwa mdogo na kata chache zaidi lakini ndiko Ubadhilifu mkubwa unatokea.
Now, imagine unaongeza wigo kuwa na Majimbo mathlan Shinyanga, Mwanza, Geifa, Mara na Bukoba! Halafu uunde serikali yake na Bunge lake! Patakuwa na wabunge wa jimbo hilo pia Wabunge wawakilishi Bunge la JMT. Fedha hizi za matumizi haya makubwa zitatoka wapi?

Ikiwa.mimi napingana na Seeikali 3, halafu unanambia acha 3 tuunde Majimbo ina maana unaunda Seeikaki Isopungua 6 zenye viongozi na Wabunge wake kisha bado wa Kitaifa!

Kwani Mikoa na Wilaya zina kasoro zipi? Bila shaka ni UTUMISHI yaani hakuna UWAJIBIKAJI. Kama haya yanakosekana na WATU ni walle wale tulonao huoni kwamba tatizo ni WATU sio UTAWALA?

Sisi watumishi ndio tatizo hata kama.tutagawa nyumba kwa nyumba shida zitabakia palepale. Tatizo ni TAASISI zeru haziwajibiki. La kufanya ni.kutafuta mbinu ziwajibike. Kila mmoja wetu aogope kuiibia serikali. Na ndivyo wenzetu waliweza kufanikiwa kwa sababu kila mtumishi ana wajibu na nishani ya kazi.
- Sisi ni Kanyaga Twende, tumechelewa mno..
 
Hili nalo ni swala zito sana maana leo hii tupo mil 60 utamilikishaje ardhi ambayo tuseme kuna watu wana eka mil moja ya shamba wakati mwingine hana hata nusu eka? Je unahitaji ardhi kwa sababu gani? Kama nyumba unaweza kununua ya ghorofani sio lazima iwe ardhi yako!

Kama kilimo huoni hatari ya wataondoshwa wakulima wadogo wadogo katika maeneo yao na kuzaa Wakulima matajiri ambao watauziwa ardhi hizo kutokana na tamaa ya kutokana na Umaskini wa wakulima mfano wa Kariakoo ilivyouzwa kwa matajiri?
n
Je, wafugaji wenye mifugo utawapa eka ngapi. Transpassing utazizuia vipi mtu akikatiaha shambani kwako? Najaribu kujenga hoja hapa kusikia majibu yako..
Naona umegusia maeneo kadhaa. Sidhani kama nina majibu yote, hata hivyo nijaribu kuelezea kidogo.
  • Tuko mil. 60, na idadi hii inategemewa kuendelea kuongezeka. Njia mojawapo ya kulinda ardhi kwa matumizi yajayo ni kuwa na Mipango miji, vijiji na hifadhi yenye lengo hili. Tunaweza kuliongelea hii zaidi iwapo itahitajika.
  • Nafikiri, yaliyobaki - hata sasa yanatokea. Tena nafikiri, ni muda sasa wa Kuamua kama tunataka tuwe Wajamaa, mabepari, mchanganyiko, etc (kwenye makaratasi, sera na vitendo) na kuacha kuwa wanafiki.
 
Ni rahisi sana kusema unapounda.majimbo unataka.kuwasogegezea karibu Wananchi huduma lakini kuna huduma zilokaribu na Wananchi kuliko Serikali za Mitaa?

Kumbuka tu kwamba hakuna kubwa.ambalo Seeikali ya Majimbo.itafanya dhidi ya Serikali Kuu kuliko serikali za mitaa ambazo zina ukubwa mdogo na kata chache zaidi lakini ndiko Ubadhilifu mkubwa unatokea.
Now, imagine unaongeza wigo kuwa na Majimbo mathlan Shinyanga, Mwanza, Geifa, Mara na Bukoba! Halafu uunde serikali yake na Bunge lake! Patakuwa na wabunge wa jimbo hilo pia Wabunge wawakilishi Bunge la JMT. Fedha hizi za matumizi haya makubwa zitatoka wapi?

Ikiwa.mimi napingana na Seeikali 3, halafu unanambia acha 3 tuunde Majimbo ina maana unaunda Seeikaki Isopungua 6 zenye viongozi na Wabunge wake kisha bado wa Kitaifa!

Kwani Mikoa na Wilaya zina kasoro zipi? Bila shaka ni UTUMISHI yaani hakuna UWAJIBIKAJI. Kama haya yanakosekana na WATU ni walle wale tulonao huoni kwamba tatizo ni WATU sio UTAWALA?

Sisi watumishi ndio tatizo hata kama.tutagawa nyumba kwa nyumba shida zitabakia palepale. Tatizo ni TAASISI zeru haziwajibiki. La kufanya ni.kutafuta mbinu ziwajibike. Kila mmoja wetu aogope kuiibia serikali. Na ndivyo wenzetu waliweza kufanikiwa kwa sababu kila mtumishi ana wajibu na nishani ya kazi.
- Sisi ni Kanyaga Twende, tumechelewa mno..
Mikoa na Wilaya, kwa maoni yangu ni majimbo yanayofuata mfumo wa utawala wa kati (Central governance) ambayo ndio chanzo cha Tatizo.
 
  • Hata sasa kuna huo mgawanyo, kuna Wanzanzibar na (so-called) Watanzania Bara. Muungano wa serikali 3 utafasema, huyu Mtanzania Bara, ni Mtaganyika (pamoja na mambo mengine) - ni Muungano usio na unafiki.
  • Nafikiri, Watu wenye nia ya kuungana, wakiungana ni jambo zuri. Hatahivyo, Sidhani kama ni sahihi kuwalazimisha watu waungane.
  • Ni wazi kuwa Wazanzibar hawataki Tanganyika na Zanzibar ziungane kwa nchi moja (niko tayari kukosolewa kwa hili). Muungano tulionao sasa, hauitendei haki Tanganyika, ukiachana na mapungufu mengine, na ndio maana kunapendekezo la serilkali 3.
Sio kweli kabisa maneno haya ni ya Wanasiasa, uhasama.baina ya Watu wa Bara na Visiwani umetokana na Siasa za maji taka nitakwambia kwa nini.

Enzi za Sultan na hata kabla ya Mapinduzi Waarabu na hata Wapemba wengi tu walienda kuishi Bara wakifanya Biashara zao bila kubaguliwa. Kulikuwa na Wa Oman mikoani mpaka vijijini ukienda hata visiwa vya Ukerewe kulikuwa na Waarabu na Wapemba wameselea huko enzi na enzi. Wahenga tunajua maana tumeishi nao kama ndugu zetu.

Wabara nao wapo wengi walokwenda kuishi Unguja kabla hata ya Mapinduzi tena wengine wamekuja kuwa viongozi mpaka leo lakini wanaitwa Wazanzibar. Sababu tu ya kuzaliwa Zanzibar.

Hizi Siasa za Uzanzibar na Ubara zimekuja baada ya Udini kutaka kutugawa na sii Makabila, rangi au mipaka ya nchi bali Udini ulipoanza kuwa Siasa za nchi haswa kutokana na vitendo vya Marekani na Israel shiei ya Waislaam ndipo kukaibuka Udini ndani ya Siasa.

Zanzibar wanataka sana tuwe na Serikali 3 kwa sababu moja kubwa. Zanzibar inaubeba mzigo wake wa kuwa na Serikali 2 wakati Bara ina 1. Sijui kama unanielewa?

Zanzibar inahudumia serikali yake na kuna fungu lazima watoe kwenye mambo ya Muungano ya Serikali ya Muungano, wakati Bara Serikali Kuu ndio inashughulika na mambo yote ya Muungano na yasokuwa ya Muungano.

Zanzibar wanaumia kwa sababu ya muundo wa Serikali 2 wakati huo huo hawataki 1 bora ziwe 3 au tuvunje Muungano nao wabakie na 1.
Wanajiuliza kwa nini Bara nao wasibebe mzigo kama wetu? maana hesabu hazikukaa sawa kwao! Niliutoa mfano huko nyuma.

Ndio maana wanataka nasi tuwe na 3 ili tuwe na Serikali moja tu ya Muungano, halafu kila mmoja abebe mzigo wa Serikali yake hata kama sisi tunawabeba katika mengi ambayo wao hawayaoni.

Ukichukua muda kutafakari nayoyasema utanielewa lakini huwa ngumu sana kumfahamisha mtu undani wa mfumo huu unatusaidiaje Bara kuua ndege wawili kwa jiwe moja!

The only fair game ni kuwa na Serikali 1 kwa sababu nina imani kubwa kwamba Serikali 3 haziwezi kutuunganisha WATANZANIA bali zitatugawa zaidi
 
Mikoa na Wilaya, kwa maoni yangu ni majimbo yanayofuata mfumo wa utawala wa kati (Central governance) ambayo ndio chanzo cha Tatizo.
Mkuu hata hizi serikali za Majimbo zina viongozi wa Serikali Kuu ndani wakishughulika na mambo ya Jamhuri (federal) Ujue unapounda Majimbo kuna mambo mtafanya ya Serikali Kuu na mengine yataendeshwa na Serikali za Majimbo ni sawa kabisa na Muungano Wa Tanganyika na Zanzibar.

Kuwa na Serikali za Mitaa (halmashauri) ni bora zaidi kulingana na muungano wetu, kinachotakiwa ni kuboresha usimamizi na utekelezaji (check and Balance) yaani iwe ada kuhakikisha fedha inayotumika inalingana na matokeo.

Hakuna Jimbo (state) ambalo Halina Mkuu wa Mkoa au wilaya kwa majina yao ambao husimamia shughuli za Serikali Kuu (federal). Tena wao mambo yasokuwa ya Muungano huwa machache sana hususan huduma za kijamii kama vile Elimu, Afya, usafiri, ajira, barabara n.k haya ndio hujitegemea lakini sii mambo makubwa, pia hata katika hayo kuna fungu la matumizi hutoka Serikali Kuu.
 
Back
Top Bottom