RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

hapa cha msingi ni Let Zanzibar go, hakuna cha serikali tatu hilo ndio suluhisho...

Demokrasia ina gharama zake. Mfumo huo mpya wa serikali tatu ni cheaper(una gharama nafuu) kuliko wa sasa kwasababu:
1.Mfumo mpya una mawaziri wachache kuliko wa sasa.
2.Mfumo mpya una wabunge wachache kuliko wa sasa(375).
3.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye wizara husika kuliko wa sasa.
4.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye ofisi za bunge kuliko wa sasa.
5.Mfumo mpya utakuwa na uwajibikaji mkubwa kuliko wa sasa, ambao mamilioni ya pesa za walipa kodi yanapotea.

Hivyo basi, mfumo mpya wa dola unapunguza kwa kiasi kikubwa gahrama za uendeshaji wa dola.

Naipongeza tume kwa kufanya mambo kisayansi.
 
Rasimu ya katiba iliyozinduliwa jana inatupa matumaini bali binafsi naona serikali tatu ni mzigo kwa wananchi. Serikali ya muunganoitakua na wabunge 75 na mawaziri wasiopungua 15. Lakini serikali hii itategemea mapato yake kutoka serikali ya Tanzania Bara na Zanzibar. Watakaoumia zaidi kuibeba ni Tanzania Bara. Sielewi kabisa bunge na mawaziri wa muungano watakua wanafanya nini wakati kila upande wa hizo serikali mbili kuna wabunge na mawaziri wao. Naona pengine tuchague tu rais wa muungano halafu kila upande kuwe na waziri mkuu mtendaji atakaechaguliwa na wabunge wa serikali hiyo. Kwa staili hiyo tutaepuka mzigo mkubwa.

Peleka maoni yako kwenye baraza la katiba wilayani kwako, kama mzigo tumbo lako mzigo kwa nchi hii
 
Mkuu kuhusu idadi ya wabunge wala sio tatizo, wabunge waliopo sasa ni 351 lakini rasimu hii imependekeza wabaki 75 wa kiume na kike. Huoni ni idadi pungufu tano??? Think big[/QUOTE

You should think big as well. Kwani serikali za shirikisho hazitajuwa na wabunge? Hawata copy na kuamua kuwa na wawili kwa kila jimbo? Majimbo ya uchaguzi yatakuwaje? Hizo ghara zote za mabunge ya nchi washiriki na ya shirikisho si pesa za walipa kodi? Think big.
 
Pale uliposema wahuni wenye kuongea kwa sauti ya juu ulikuwa unamaanisha sugu,lema na msigwa????? Funguka plz

nimejitahidid kutumia lugha ya kifasihi lakini watanzani wanawajua wabunge wenye tabia za kihuni bungeni na kwenye jamii.
 
aisee kama unayo soft kopy ya hiyo rasimu tutupie na sie tuipate,

mkuu ni kweli ninayo lakini tangu saa kumi na mbili najitahidi kuitumbukiza inagoma sijui kama ni mtandao uko down au la.
 
Watanzania wakati umefika ni lazima tuondokane na mawazo mgando ya serikali mbili, ambazo utekelezaji wake ni mgumu sana kwa nyakati zetu hizi. Lazima tuambatane na fikra mpya na chanya za kuwa na taasisi zilizojengewa misingi ya kikatiba ya uwajibikaji. Demokrasia inayosemwa, sasa inatakiwa iingie kwenye matendo, kuliko kubaki nadharia tuu.

Mfumo huo mpya wa dola utapunguza sana gharama za uendeshaji wa Serikali na Bunge la Muungano kwa kiasi kikubwa, hivyo kuwapunguzia wananchi mzigo. Mfumo huo mpya wa serikali tatu ni cheaper(una gharama nafuu) kuliko mfumo wa sasa, kwasababu:
1.Mfumo mpya una mawaziri wachache(15) kuliko wa sasa(56).
2.Mfumo mpya una wabunge wachache(75) kuliko wa sasa(375).
3.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye wizara husika kuliko wa sasa.
4.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye ofisi za bunge kuliko wa sasa.
5.Mfumo mpya utakuwa na uwajibikaji mkubwa kuliko wa sasa, ambao mamilioni ya pesa za walipa kodi yanapotea.
6.Mfumo mpya hauna ofisi ya wazili Mkuu, hivyo gharama zote zilizopo sasa za kuiendesha ofisi ya PM na makandokando yake hazitakuwepo.

Hivyo basi, mfumo mpya wa dola unapunguza kwa kiasi kikubwa gahrama za uendeshaji wa dola.
Huu mfumo mpya ni mzuri na unaotekelezeka kirahisi, bila kuhitaji gharama kubwa. Mfumo huo upo Ujerumani,Marekani, Afrika kusini, Uingereza, India Nk

Mfumo huu mpya utatoa ajira nyingi kwa vijana wetu wasomi, kwasababu upatikanaji wa fursa za kazi hautakuwa unatawaliwa na mfumo wa kikilitimba, miungu watu, na kupendeleana kama ulivyo sasa. Kwani kwa sasa kupata kazi lazima uwe ulizaliwa ktk familia ya mwanasiasa fulani au unafahimia na mtu fulani maarufu, au utoe rushwa.

Naipongeza tume kwa kufanya kazi kisayansi.
 
Mkuu acha kuwapotosha watu! tulia soma vizuri rasimu! hao 15 ni wa shirikisho tu, bado wa Tanganyika! upo hapo?
 
Rasimu ya katiba iliyozinduliwa jana inatupa matumaini bali binafsi naona serikali tatu ni mzigo kwa wananchi. Serikali ya muunganoitakua na wabunge 75 na mawaziri wasiopungua 15. Lakini serikali hii itategemea mapato yake kutoka serikali ya Tanzania Bara na Zanzibar. Watakaoumia zaidi kuibeba ni Tanzania Bara. Sielewi kabisa bunge na mawaziri wa muungano watakua wanafanya nini wakati kila upande wa hizo serikali mbili kuna wabunge na mawaziri wao. Naona pengine tuchague tu rais wa muungano halafu kila upande kuwe na waziri mkuu mtendaji atakaechaguliwa na wabunge wa serikali hiyo. Kwa staili hiyo tutaepuka mzigo mkubwa.
nakubaliana nawe hakuna haja kabisa ya kuwa na serikali ya shirikisho kabisa kwani unazo tayari serikali pande zote mbili. hakuna haja ya kuunda serikali kwa ajili ya kusimamia mambo saba ni wasting of money badala yake kungeundwa kamisheni kwa ajili ya kusimamia mambo haya ya muungano.hakuna haja ya kuwa na wabunge wa kuchaguliwa na rais na suala la wabunge wawili mwanamke na mwanaume lifutwe pia kwani wanawake kila siku wamekuwa wakilalamka kutodharauliwa kwa kupewa vitu vya dezo kwahiyo katiba hii itaendeleza kumdharau kwa kumtengenezea nafasi wakati anao uwezo wa kugombania kama wengine na kushinda mifano ipo kibao.suala la Madaraka ya urais inabidi liangaliwe upya kwani itaendeleza urais wa kifalme ambao unazalisha viongozi ambao badala a kuumikia nchi wanamtukuza na kumtumikia rais wa nchi.
 
Hapa chenga tupu, kinga ya rais palepale ili aendelee kujiridhisha na masela wake, uteuzi wa mawaziri still chini ya rais japo inafuata professional na kupendekezwa na hao utumishi so either wapendekezaji waweke ndugu zao au wapendekeze majina ya masela wa rais. Nimeona mabadiliko ila sio kwenye maeneo yanayotuletea shida sahv.
 
Kuna wabunge flani wamewateua ndugu zao kuwa wabunge wa viti maalumu...mmoja amempa shemeji na dada yake, mwengine amempa mtoto wake na mkwe wake na mwengine kawapa nyumba kubwa na ndogo zake mbili zipo mjengoni....nadhani sasa tutaheshimiana

hii ndiyo uovu ambao ulikuwa unafanywa na wenye nafasi ya kuteua kwa kugawa viti maalumu kwa watu wao,kwa matakwa yao waliyokusudia.
 
mkuu ni kweli ninayo lakini tangu saa kumi na mbili najitahidi kuitumbukiza inagoma sijui kama ni mtandao uko down au la.
ikikubali irushe na nistue ninahamu nao niisome , na tume sijui kwa nini hawajaiweka kwenye website yao ! utafikiri tupo kwenye karne ya 47.
Hata hivyo nadhani mtu wa IT ya tume ya katiba hayupo makini haiwezekani kwenye website yao habari latest ni ya november 2012
 
Mkuu acha kuwapotosha watu! tulia soma vizuri rasimu! hao 15 ni wa shirikisho tu, bado wa Tanganyika! upo hapo?

Nashukura sana kwa comment yako isiyo na utafiti na yenye woga, mawazo mgando yasiyozingatia hitaji la wakati.

Zanzibar toka mwaka 1964 wanayo serikalia yao ambayo inaendesheka mpaka leo.
Tanzania bara(Tanganyika) inatakiwa iunde serikali yake kadiri ya uwezo na hitaji la kweli, siyo kupeana vyeo kwa hoja za kirafiki au kisiasa. Katika ulimwengu wa leo ambapo mambo mengi yanaendeshwa na private sector huhitaji kuwa na serikali kubwa.
Unless unataka kuwapa kazi ndugu na rafiki zako. Kwa Tanzania bara mawaziri 12 watosha kabisa. Idara katika wizara zepewe mamlaka makubwa ya kuamua mambo. This to me is the best solution.
 
Can we let zanzibar go please we cant afford to hve another gvt just for pleasing some people
 
Jamani naomba mwenye soft copy ya rasimu ya katiba mpya atututupie na sie tuisome.
mapemaaa tuanze kuitafakari.
 
nimesoma kwa makini rasimu ya katiba mpya kama itapita basi yawezekana ni kitanzi kikubwa kwa wanasiasa wengi na vyama vyao vya siasa,ni wazi kuwa ule utitili wa wabunge kwanza utakoma kwani hapo awali mtu yeyote hata kama ni muhuni lakini akiwa na uwezo mkubwa wa kuongea kwa sauti na hasira aliweza kuchaguliwa,lakini wengine waliweza kuteuliwa kushika ubunge kutokana na kuwa na mahusiano fulani mazuri na wanaoteua hali hii ilifanya wateuzi wengi kuteua hata watu wa hovyo kabisa.

lakini pia badhi ya vyama vimejaza wabunge wa viti maalumu kutoka maeneo fulani na kushindwa kuzingatia uwezo muhimu wa mhusika na hata uadilifu wake,kwa sasa majimbo yatakuwa machache na hata wabunge nao watapugua ambapo inatarajiwe kuwe na majimbo ishirini ya uchaguzi hali hii itafanya wapatikane wabunge wenye sifa stahiki hata kutoa rushwa haitawezekana mtu mwenye sifa stahiki na uadilifu uliotukuka ndiye atakayechaguliwa.

kwa mfano kutakuwa na wagombea wa urais watatu kwa maana ya tanzania zanzibar,tanzania bara na rais wa shirikisho,kwa vyama venye uhaba wa watu wenye uwezo wa kuongoza vitapata wakati mgumu sana najaribu kufikiri kutoka chadema nani atagombea zanzibar,nani atagombea bara,na nani atagombea urais wa shirikisho.hali hii pia yaweza kukikuta chama cha nccr mageuzi na vyama vingine pia vichanga.[/QUOTE

MMh mimi ninavyo kutazama katika ulichokiandika nikwamba wewe rasimu yenyewe hujaielewa na possibly wewe ni slow learner....Anyway hii rasimu inaelezea wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano na sio Tanganyika wala Zanzibar
 
ikikubali irushe na nistue ninahamu nao niisome , na tume sijui kwa nini hawajaiweka kwenye website yao ! utafikiri tupo kwenye karne ya 47.
Hata hivyo nadhani mtu wa IT ya tume ya katiba hayupo makini haiwezekani kwenye website yao habari latest ni ya november 2012

wamejitahidi sana yani latest ni nov? Mie nilijua itakuwa ileile ya april 2012,hyo ya jana uzinduzi wa rasimu wataiweka mwaka 2015 mwanzoni.
 
Bwana!! bwana!!! hebu mtu mwenye soft copy haitupie humu tuione.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom