Rasmi nimeligundua hili, Mungu na Shetani hawapo: Dini ni utapeli

Infropreneur 14:7
Ulimwengu na vyote vilivyomo duniani except man-made things ni vya kipekee. Havijaumbwa na yeyote yule na wala havihitaji muumbaji.

14:8- Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na muumbaji, Hata muumbaji wa kila kitu lazima awe na muumbaji wake mwingine.

14:9- Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo muumbaji, Maana kitazua maswali ya kiliwezaje ku exist chenyewe pasipo muumbaji. Ili muundo wa ulazima huu ufuatwe na kila kitu na u apply kwenye kila kitu.

14:10- Na kama si lazima kwamba kila kitu kilichopo kina muumbaji, Hata Jua☀️ na ulimwengu kwa ujumla HAVINA Muumbaji.
 
pole sana kwa kuchelewa kujua mkuu
 
Hata wewe tunaona mwili wako tu hakuna haonaye roho yako Wala nafasi. Je sababu nafasi yako haionekani tusema hauna nafasi?
 
Kuamini kwamba hakuna Mungu wala Shetani ni kuwatukuza hao hao unaowaona wanapotosha dunia. Kwamba wanatengeneza na kukuza technology kwa akili na uwezo wao.

Anyway, soma kitabu cha Henoko, utaelewa zaidi.
 
Kwamba mungu kamtoa mwanaye aje aukomboe Ulimwengu...
Mungu huyu ndo kamuumba shetani lakini kamshindwa akaamua kumtoa mwanaye aje ili sisi tuokolewe?..
Halafu huyu huyu mungu ndo atatoa hukumu siku ya mwisho..
Halafu huyu huyu mwanaye ndo mungu mwenyewe.....
 
Mzazi wa kwanza kabisa duniani alizaliwa na nani?
Hakuna mzazi wa kwanza kabisa duniani wa binadamu wote.

Kwa sababu zifuatazo;

1- Utofauti wa vinasaba (DNA) 🧬 baina ya watu.

Kama binadamu wote tungekuwa tumetokana na mzazi mmoja tu, Basi wote tungekuwa na vinasaba vinavyo fanana. Lakini sivyo, Binadamu tuna tofautiana vinasaba. Hivyo hii ni dhahiri kuwa hakuna mzazi wa kwanza.

2- Utofauti wa rangi zetu sisi binadamu.

Kuna waafrika weusi, wazungu weupe, wahindi weupe, weusi na wekundu. Kuna wajapani, wachina, wakorea, wafilipino, waarabu n.k Utofauti huu ni uthibitisho tosha kwamba hakuna mzazi wa kwanza kwa watu wote.

Kama mzazi wa kwanza kwa watu wote angekuwepo basi kusingekuwa na utofauti huu wa rangi. Binadamu wote tungekuwa na rangi moja na kufanana wote dunia nzima.

3- Uwepo wa hali za kurithi kama ualbino.

Kuna binadamu huzaliwa na ualbino. Na wengine huzaliwa kawaida. Sasa kama binadamu wote tungekuwa tumetokana na mzazi mmoja tu, Either wote tungekuwa maalbino, Au kusingekuwa na maalbino. Wote tungekuwa kawaida tu.

4- Magonjwa ya kurithi.

Kuna familia zina magonjwa ya kurithi na familia zingine hazina. Hivyo huu ni uthibitisho tosha kwamba hakuna mzazi wa kwanza kwa binadamu wote.

Hivyo, Hakuna mzazi wa kwanza duniani wa binadamu wote.
 
Hata wewe tunaona mwili wako tu hakuna haonaye roho yako Wala nafasi. Je sababu nafasi yako haionekani tusema hauna nafasi?
Roho ni dhana ya kufikirika tu. Haipo katika uhalisia.

Nafsi ni dhana ya kufikirika tu. Haipo katika uhalisia.

Roho haipo.

Nafsi haipo.
 
Roho ni dhana ya kufikirika tu. Haipo katika uhalisia.

Nafsi ni dhana ya kufikirika tu. Haipo katika uhalisia.

Roho haipo.

Nafsi haipo.
Ushawahi kuuona upepo au pumzi?. Pia unaweza kusema havipo sababu havionekani?
 
Ushawahi kuuona upepo au pumzi?. Pia unaweza kusema havipo sababu havionekani?
Angalau kitu kinaweza kuwepo kwa namna mojawapo ya kuonekana, kushikika, kusikika, kuhisika na kupimika.

Upepo upo kwa kuhisika, kupimika na kusikika.

Upepo ukivuma unasikika, Pia tunauhisi.

Upepo unapimika. Tunaweza kupima upepo kwa kutumia vifaa kama Anemometer na Windvane.


Sasa huyo Mungu hayupo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika yupo.

Huyo Mungu Haonekani, Hashikiki, Hasikiki, Haisiki na wala Hapimiki.

Mungu huyo ni mawazo ya kufikirika tu, imaginations just an illusion.

Mungu hayupo katika uhalisia bali katika mawazo na imani za kufikirika tu.

Mungu huyo mmemtunga huko vichwani mwenu tu, na wala huwezi kuthibitisha uwepo wake.
 
Ona sasa, Mimi nazungumzia maisha wewe unaleta story za kwenye Biblia.
Ushaathirika hakuna kitu utaelewa maana unareference moja tena inayokujenga katika kuamini badala ya kujua.
Bwana Yesu alisema "kama tu ya duniani mmeshindwa kuyaelewa mtaelewaje nikiwaambia ya mbinguni?. " Nimekukupa ushuhuda binafsi ukapinga na hu kuelewa utalewa vipi ya kwenye Biblia?.
 
Bwana Yesu alisema "kama tu ya duniani mmeshindwa kuyaelewa mtaelewaje nikiwaambia ya mbinguni?. " Nimekukupa ushuhuda binafsi ukapinga na hu kuelewa utalewa vipi ya kwenye Biblia?.
Unachekesha sana Mtumishi.
 
Haya sawa
 
Biblia inasema yaliyofunuliwa ni yetu yaliyofichwa ni ya Mungu mwenyewe.

Maswali uliyoniuliza ni sawa na umuulize kuku asili ya anayemfuga (mwanadamu)

bila Shaka hatojua Ila mmiliki anaweza jua asili yake na ya Hugo kuku na akifa Amanda wapi ( tumboni) .

Kama ufahamu wa ngombe, kuku, mbuzi, bata ulivyo mdogo juu ya mwanadamu ndivyo ufahamu wa mwanadamu ulivyo mdogo juu ya Mungu hivyo hivyo, na ukijaribu kumfanya kuku ajifunze kuhusu mwanadamu utaishia kumuua tu ndio maana Biblia inasema hakuna aliyemuona Mungu akaishi ikimaanisha ufahamu huu wa milango 5 hauwezi muelewa Mungu maana uko limited Sana Ila utakapotoka katika mwili huu roho yako itamwona USO kwa USO ndipo wengine watafurahi milele kukutana na muumba wao na wengine aibu, mateso, na dhiki ya milele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…