RC Amos Makala mbona wamachinga wanarudi kwenye njia za miguu tena Dar es Salaam?

RC Amos Makala mbona wamachinga wanarudi kwenye njia za miguu tena Dar es Salaam?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Sio vizuri kutimuana kila wakati kwakuwa zoezi la kutimua watu linazaa kelele na bughudha nyingi kwa wananchi. Tulifurahia kuona watanzania wenzetu wafanyabiashara ndogondogo wameziachia barabara za magari na njia za miguu za watanzania wenzao walizokuwa wamezivamia kwa maslahi yao binafsi.

Lakini sasa hivi inasikitisha kuona machinga hawa wanaanza kurudi tena polepole mmojammoja kimyakimya kwenye njia za miguu. Watu hawa wanatabia ya kuambukizana ugonjwa wa kupanga vitu chini kwenye njia za waenda kwa miguu. Yaani anaanza mtu mmoja kupanga chini viatu 3 kutesti mitambo na akiona hali ni shwari anaongeza pea 3 kesho. Na wengine wakiona mwenzao kapanga chini bila kelele na yeye analeta bidhaa yake, na mwingine, mwingine hadi njia zote zinazibwa.

Leo hii ukipita pale Buguruni utaona wale wauza nets na mapazia walianza polepole mmojammoja na sasa karibia hali anarudi upya kama awali.

Ni vizuri surveillance iwe ya kudumu ili kupunguza kurudia upya zoezi lilelile baada ya muda mfupi. Pia ni vema watu watafute maeneo halali sasa ya kuanyia biashara ili kuepuka kurupushani karibu na uchaguzi.
 
Wawaboreshee maisha na miundo mbinu , ni mjinga Tu anayeweza kukubali kufa njaa sababu ya mwanasiasa anayetembelea mav8 , machinga ni kero Ila Kwa nchi yetu hii ya kuneemesha wachache , lazima wachuuzi waongezeke
 
Hawakujipanga mapema kabla ya kufanya maamuzi ya kuwahamisha.

Kiuhalisia ilitumika siasa zaidi ya mantiki, serikali yetu ione umuhimu wa kujenga miundombinu rafiki kwao ili kuleta tija.

Ilikuwa ni busara kama wangetenga maeneo rafiki yenye miundombinu inayofikika na huduma uhakika Kwa wamachinga,wao pia ni raia wa Tanzania,wanapaswa kulipa kodi zao kulingana na aina ya biashara wafanyayo.

Serikali iangalie mazingira rafiki yenye mzunguko mzuri(wingi wa watu),wawatengenezee na kuwapeleka huko.
 
Hawakujipanga mapema kabla ya kufanya maamuzi ya kuwahamisha.
Kiuhalisia ilitumika siasa zaidi ya mantiki, serikali yetu ione umuhimu wa kujenga miundombinu rafiki kwao ili kuleta tija.
Ilikuwa ni busara kama wangetenga maeneo rafiki yenye miundombinu inayofikika na huduma uhakika Kwa wamachinga,wao pia ni raia wa Tanzania,wanapaswa kulipa kodi zao kulingana na aina ya biashara wafanyayo.
Serikali iangalie mazingira rafiki yenye mzunguko mzuri(wingi wa watu),wawatengenezee na kuwapeleka huko.
sisi pia ni watanzania kama wao, tunahitaji haki yetu ya njia za kutembea kwa miguu tusigongwe na magari. Kusema hivyo ni sawa na mtu aje kwako kulala mlanoni kwako kwa kisingizio kuwa yeye hana sehemu ya kulala. Wamachanga sio kundi moja la watu kwamba ukiwapatie eneo lenye miundombinu basi umetatua kero yao. Hawa ni watu ambao idadi yao inaongezeka kila siku, ni maeneo gani utawayowapeleka ili watoshe wote? mfano, pale machinga complex kuna watu wako mule kwa zaidi ya miaka 15 sasa wakijiita machinga. Hivi ni kweli kwa miaka 15 yote wewe bado unastahili kuitwa machinga?, yaani hukui ili ipishe wengine (vijana) kwenye jengo.
 
Makala dhaifu hawezi jiji la Dar, Tutapata wapi akina Kandoro!!!!
Nadhani kuna upigaji fedha kwenye zoezi la kuwaondoa machinga, wanataka wajae tena ili waidhinishe fedha nyingine ya kuwaondoa.
 
Wawaboreshee maisha na miundo mbinu , ni mjinga Tu anayeweza kukubali kufa njaa sababu ya mwanasiasa anayetembelea mav8 , machinga ni kero Ila Kwa nchi yetu hii ya kuneemesha wachache , lazima wachuuzi waongezeke
Kama hivyo wawarudishie pia wale waliowanyang"anya nyavu zao za kuvulia wa kisingizio kuwa zina matundu madogo wakati hizi nyavu walizinunua kwa pesa zao halali kwenye maduka yanayolipa ushuru na kodi.
 
Makala alichemka kuondoa wengine na wengine kuwaacha........Kuna mitaa kkoo waliondolewa, wengine wakabaki.....saizi wamerudi kama zamani,kifupi zoezi limefail
 
Nadhani kuna upigaji fedha kwenye zoezi la kuwaondoa machinga, wanataka wajae tena ili waidhinishe fedha nyingine ya kuwaondoa.
Baadhi ya mitaa, viongozi wa machinga wanapitia posho......imekuwa chanzo Cha mapato
 
Hao wanalipishwa hapo na wagambo ni sawa na kusema wameruhusiwa kufanya biashara hizo sehemu na wagambo.
 
Back
Top Bottom