RC Chalamila: Kama huwezi kuishi kota za Magomeni, hamia Vingunguti

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Kila siku naona malalamiko kwenye ofisi yangu kutoka kwa wakaaji wa Magomeni kota mara wanalalamika bili ya Maji ni kubwa wameshindwa kulipa wengine wanalalamika kwamba bili ya taka imekuwa kubwa wakati hizo taka wanazalisha wenyewe hii inaonesha wameshindwa kukaa kwenye hizo kota.

Nashauri kama mtu ukiona huwezi kukaa kwenye majengo ya TBA ya Magomeni basi hama uende Vingunguti"

Your browser is not able to display this video.
 
Huu ndio ukweli ambao wengi hawatapenda kusikia, ila hili la maji, nilisikia Waziri akiliongelea!

Hapo Magomeni Manji alitaka kupaendeleza, JPM akaamua kufanya siasa, akatangaza kuwajengea hao wananchi nyumba hizo ili kumkomesha Manji, wakati mezani kulikuwa na option ya kuwafidia waondoke. Tangu lini serikali kuu ikajengea mwananchi wa kawaida nyumba?!

Sasa wameshakuwa kama watoto, wanalia lia kwa kila kitu, hata wakishindwa ku-pass wind, watalalamika, kuna siku watasema hakuna sehemu ya kuchezea kigodoro, serikali iwafikirie kuwajengea.

Its possible hata design ya mradi huo haukulenga wale wenye maisha ya kuunga unga, unit title inahitaji wanaojiweza, wanakuwa na uongozi au mfumo wa kulipia gharama za pamoja.. waanze kulipia kodi ya majengo na ardhi
 
Ipo siku ........aina jina wala saa .........pale masiha atakapo amua kuwafuta machozi wana wa adam........itakuwa kilio na kusaga fizi maaana meno hatakuwa hana tena
 
hizi nyumba walipewa bure,wamepanga au nini kinaendelea au waliuziwa wale wakaazi wa zamani wa vokota vibovu
 
yupo sahihi. hao watu wa kota za magomeni sijui wabebweje kwa mbeleko gani.
 
🤣🤣Utajua hujui
 
Kuna kupima mkojo huyu mpimeni kinyesi sio steji aliyofikia kwenye akili zake
 
Mani alitaka kufanya nn mkuu?
 
Zamani kwenye vile vikota walikuwa wanajiuzia mkaa, magenge, vitumbua na visheti. Huko ghorofani utauzaje mkaa. Mradi wowote wa kuwajengea maskini maghorofa huwa unafeli sababu masikini makazi yake ndiyo ofisi yake.
 
RC wa Kisasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…