RC Chalamila: Kujifanya wanasheria pamoja na kupenda kiingereza kunakwamisha maendeleo ya mkoa wa Kagera

RC Chalamila: Kujifanya wanasheria pamoja na kupenda kiingereza kunakwamisha maendeleo ya mkoa wa Kagera

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200


Hayo ameyasema wakati wa kikao cha ndani cha siasa kilichohudhuriwa na makamu mwenyekiti wa CCM bara bwana Kinana.

===

“Mkoa huu hauendelei kwa sababu nyingi, ila sababu kubwa ni hata ninyi ndugu zangu wahaya, wanyambo mnaoishi hapa kwa kweli kuna muda bado hatujajitambua kwamba tupo kwenye ushindani.”

“Tukipita hapa hata siku za kawaida mpaka saa 3 maduka hayajafunguliwa. Sasa unajiuliza, duka linafunguliwa saa tatu. Inamaana mnalala sana au mnafanyaje? Sasa na ninyi mbadilike, fungueni duka mapema ili tuingie kwenye ushindani.”

“Jambo lingine linalokwamisha mkoa huu pia Mhe. Makamu mwenyekiti, Kila mmoja hapa kwenye mkoa huu huwa ni mwanasheria, mnapenda sana kubishana. Eeeeh…Mambo mengi wanapenda kiingereza kingi kingiii, sasa naomba niwaambie, sitaki kiingereza waa sitaki makaratasi”

“Nataka namna gani utakavyo tumia elimu yako kuibadilisha kuwa maendeleo kwa wanakagera. Basi.”
 
Kingereza kinazuiaje maendeleo?

Yeye ni mkuu wa mkoa...Stendi ya Bukoba ni majanga..ashawahi itembelea akaona matatizo yake..

Yaan mtu unaletwa uongoze mkoa unaanza maneno na kejeli...solve matatizo ya mkoa hasa hapo Bukoba...mji barabara zake mbovu, stendi ni ya matope na kero nyingine kibaoo

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Kingereza kinazuiaje maendeleo?

Yeye ni mkuu wa mkoa...Stendi ya Bukoba ni majanga..ashawahi itembelea akaona matatizo yake..


Yaan mtu unaletwa uongoze mkoa unaanza maneno na kejeli...solve matatizo ya mkoa hasa hapo Bukoba...mji barabara zake mbovu, stendi ni ya matope na kero nyingine kibaoo

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app

Unategemea idiot na mlevi kama yule alete maendeleo? He has been dumped there to frustrate wanaKagera. Samia hebu ondoa hilo takataka lako
 
Ukimsikiliza Chalamila kwenye hiyo clip utabaini mtoa Mada ana chuki binafsi na Rc Chalamila.Ila ukiwa Kiongozi nchi hii inatakiwa uwe na moyo wa chuma.

Wameelezwa ukweli wanaanza kuleta maneno, hapo ujumbe waache uvivu waongeze kasi ya kuchapa kazi wafungue maduka mapema sana biashara zifanyike sio unaduka sababu ni lako ukafungue saa nne, wachukue ushauri wasonge mbele siri ya maendeleo ni kazi kwa bidii
 
Kagera iko mpakani mwa Uganda, Rwanda, Burundi lakini watu wa kagera kwaufupi wamelala sana wavivu
Unavyoongea kama vile kagera ni nchi nyingine

Hebu nenda katumie hio fursa ya mipaka maana hujakatazwa....
Kabla ya kuwaketukana watu wa kagera hebu angalia vzr mfumo wa ufanyaji wa biashara za mpakani ndo utajua kwa hali iko hivyo

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom