RC Chalamila: Tulidhibiti Wizi wa Transfoma kwa kuwanywesha Wezi Mafuta ya Transfoma

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Albert Chalamila amesema vitendo vya wizi wa mafuta ya transfoma katika mkoa wa Dar es salaam vilikirthiri, hivyo ili kukomesha vitendo hivyo waliamua kuwa yeyote atakayekamatwa anafanya vitendo hivyo atanyweshwa mafuta ya transfoma na mpaka sasa hakuna wizi wa transfoma Dar es Salaam

RC Chalamila amesema hayo katika ufunguzi wa kongamano la 10 la Jotoardhi linalooendelea katika ukumbi wa mikutano wa JNICC, jijini Dar es salaam, lililofunguliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango leo Oktoba 23, 2024.
Your browser is not able to display this video.


Pia Soma

 
Huyu mtu kweli kichwani bado Yuko mzima???
Mtu kuugua kichaa siyo lazima mpaka avae chupi kichwani, wakati mwingine matendo au maneno yake tu ni uthibitisho tosha kuwa mtu fulani anaugua kichaa.
 
Huyu mtu kweli kichwani bado Yuko mzima???
Mtu kuugua kichaa siyo lazima mpaka avae chupi kuchwani, wakati mwingine matendo au maneno yake ni uthibitisho tosha kuwa mtu fulani anaugua kichaa.
Yaani nimesikitika sana, kwa kauli yake hii alipaswa kabla hajaridisha Mic awe amesha tumbuliwa...☹️
 
Kiongozi wa umma anaongea vitu vya ajabu. Aisee kuna haja ya kukazia vet
Huyu ni decision maker wa mkoa? And tunashangaa maamuzi ya ajab ajabu yanayokea wapi
 
Huyu jamaa simkubali hata robo,ni lopo lopo sana ,Sasa kama anakili kuua watu mama Samia anasubiri nini kumuondoa ofisini huyu muuaji?

Watu wenye bichwa ka la charamila mara nyingi akili zao Huwa zimeyumba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…