Uchaguzi 2020 RC Gambo adaiwa kusuka mpango wa kuandaa wazee wa mila ili wamwombe agombee ubunge Arusha

Uchaguzi 2020 RC Gambo adaiwa kusuka mpango wa kuandaa wazee wa mila ili wamwombe agombee ubunge Arusha

Anataka aende akaitwe mheshimiwa tu kama kina Jah people na Kibajaj
Ubunge na Ukuu wa Mkoa upi una thamani zaidi kwa madaraka na kipato?

In God we Trust
 
Nimekukumbuka enzi hizo pale railway station mwanza ulivyo kuwa unachalika kwa kuuza chai buffet
Mbona Chadema iliwatuma Mtei, Mbowe na Ndesamburo rip wakampigie magoti Lowassa awe mgombea wao wa urais?

Siasa ni sayansi!

In God we Trust
 
Halafu wanaopanga hii mikakati wawe wanafikiria, huyo kivuo hawaoni ilo jina ukitanguliza pesa tu lazima avujishe siri zote..........
 
Katika hali isiyo ya kawaida mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo anadaiwa kuandaa wazee wa mila ya kimasai maarufu kama Laigwanan ili waweze kumwomba agombee ubunge katika jimbo la Arusha Mjini.

Wazee hao wa mila wanaodaiwa kukusanywa kutoka maeneo mbambali jijini Arusha ambayo ni Terat,Muriet,Mkonoo,Mateves,Oljoro,Sakina na kata ya kati ambapo wametengewa zaidi ya sh,20 milioni ili kukamilisha zoezi hilo.

Mkakati huo unasukwa kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa Ccm akiwemo mwenyekiti wa Ccm mkoa wa Arusha, Stephen Zelothe sanjari na mwenyekiti wa Ccm wilaya Joseph Masawe.

Taaarifa za uhakika zimeeleza kwamba wazee hao wa kimila wamepanga Mara baada ya bunge la jamhuri kuvunjwa rasmi watafika nyumbani kwake na kumwangukia ili agombee ubunge wa jimbo la Arusha Mjini.

Mmoja wa wazee wa kimila anayetoka kata ya Terat,Baraka Kivuyo ameelezea kwamba wameambiwa wafike nyumbani kwa kiongozi huyo eneo la Muriet huku wakiwa na mbuzi na kondoo kama ishara ya kumwomba kwa heshima ombi lao.

Hatahivyo,kiongozi Hugo ameelezea kwamba kumekuwa na nguvu kubwa inayoyumika kuwasukuma baadhi ya kiongozi wa kimila ili waende nyumbani kwa Gambo jambo ambalo limeibua sintofahamu katika mkakati huo.

"Kila wiki wanafika viongozi wa Ccm hapa ili kujua tunaendeleaje na mpango wetu wa kujikusanya na kwenda kumwomba Mkuu wa mkoa agombee ubunge" alieleza Kivuyo

Hatahivyo,alienda mbali zaidi na kudai kwamba pia kuna mkakati unaosukwa ili wazee hao wafike mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk John Magufuli ili wamwombe amruhusu Gambo agombee ubunge.

"Ikitokea kwamba Rais Magufuli anafanya ziara hapa Arusha basi sisi wazee tumeombwa na Gambo kwamba atatengeneza mazingira tufike mbele yake na kumwomba amruhusu kijana agombee ubunge" alisisitiza kiongozi Hugo

Mbio za ubunge katika jimbo la Arusha Mjini zinazidi kushika kasi ambapo mbali na Gambo baadhi ya makada wanaotajwa kulimezea mate jimbo hilo ni pamoja na mfanyabiashara maarufu,Philemon Mollel maarufu kama Monaban,wakili wa kujitegemea Albert Msando,wakili wa kujitegemea Edmund Mgemela,meya aliyejiuzulu Calist Lazaro,Dkt Batilda Buriani na wengine mbalimbali.

Mwisho

.View attachment 1453897
Acha fitna za kipumbavu ,kwani hao ndio wapiga kura?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila laheri RC Gambo!! Sasa ni zamu yako ya kuchukua Jimbo, Wananchi wa Arusha wanataka siasa za kimaendeleo.
 
Kikubwa ni kufutwa kwa Chadema Arusha mjini

Chadema imechelewesha maendeleo Arusha

Mkuu wa nchi na mwenyekiti wako anasema “maendeleo hayana chama”. Walio chini yake na hata bungeni wanasema “serikali inatekeleza ilani ya CCM”.

Pale mnaposhindwa kuleta maendeleo sehemu fulani ya nchi - mnasema ni wapinzani!!

Dhana hizi haziwezi kuwa zote za kweli. Sioni maendeleo yaliyoletwa na CCM maeneo mengi ya nchi ambapo upinzani haukuwahi hata kuwa na diwani!!!
 
Back
Top Bottom