RC Geita: Rais Magufuli ni Nabii aliyebarikiwa na Mungu wagombea wengine wanamsindikiza!

RC Geita: Rais Magufuli ni Nabii aliyebarikiwa na Mungu wagombea wengine wanamsindikiza!

Nasikia huyu jamaa akishamaliza kuwabatiza upinzani kwa maji anakuja kwenu kuwabatiza kwa moto!View attachment 1486002
Ahmada
FB_IMG_15918718110569346.jpg
 
Yeye hujiita malaika(kiongozi wa malaika), wengine humuita yesu, na wengine sasa wanamuita nabii.

hizi kufuru hazitaiacha nchi salama.
 
Mkuu wa mkoa wa Geita mh Gabriel amesema Roho mtakatifu mwaka 2015 alizunguka Tanzania nzima na alipofika Chato akaweka makao nyumbani kwake Dr Magufuli.

Gabriel ambaye alikuwa akishangiliwa muda wote huku akitunzwa kama mchungaji Lusekelo amesema Dr Magufuli ndiye Rais wa Tanzania hao wengine wanaochukua fomu ni wapambe tu wanaomsindikiza.

RC Gabriel Robert amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa kivuko katika hifadhi ya taifs kisiwa cha Rubondo mbele ya mgeni rasmi Katibu mkuu Kiongozi Dr Kijazi

Source Star tv

Maendeleo hayana vyama 10 Yatosha!
Dikteta Idd Amini alikuwa akibebwa na vijakazi na vipakasi wake na mwisho wake wote tunaujua.
 
Viongozi wa Tanzania wana matatizo, huyu yesu mpya mjini leo amekua nabii
 
Kauli ya kuthibitisha uovu wake hii hapa. Kawaacha Watanzania wengi wakiwa hawana sehemu ya kuishi kwa bomoa bomoa, kawaua wengi sana wakiwemo Ben, Azory Mawazo na mama yake Kabendera, kawabambikia kesi fake wengi kuwaharibia maisha yao. Achilia mbali wizi na ufisadi alioufanya hazina wa trillions za walipa kodi. Kadhulumu wahanga wa tetemeko, wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara.



Waovu ndio wanamuona ana roho mbaya!
 
kipindi cha kujipendekeza huu

Katibu mkuu kiongozi na uzinduzi wa Kivuko 😎
 
Mkuu wa mkoa wa Geita mh Gabriel amesema Roho mtakatifu mwaka 2015 alizunguka Tanzania nzima na alipofika Chato akaweka makao nyumbani kwake Dr Magufuli.

Gabriel ambaye alikuwa akishangiliwa muda wote huku akitunzwa kama mchungaji Lusekelo amesema Dr Magufuli ndiye Rais wa Tanzania hao wengine wanaochukua fomu ni wapambe tu wanaomsindikiza.

RC Gabriel Robert amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa kivuko katika hifadhi ya taifs kisiwa cha Rubondo mbele ya mgeni rasmi Katibu mkuu Kiongozi Dr Kijazi

Source Star tv

Maendeleo hayana vyama 10 Yatosha!
Hizi kufuru zina matokeo mabaya sana. Si sahihi kulichezea jina la Mungu, Roho wake wala viumbe vitakatifu vya kimbingu. Washauri wa Rais wajaribu kumshauri awaepuke, kuwakanya na kukaa mbali na wapambe wenye kumpa sifa za namna hii. Hakika BWANA huwa hachelewi kujibu.
 
Back
Top Bottom