RC Hapi: Jumamosi ya pili ya kila Mwezi itakuwa ni siku ya kufanya mazoezi watumishi wa umma na Wananchi wote mkoa wa Iringa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Salum Hapi amesema jopo la madaktari wa mkoa wa Iringa wamemweleza kuwa mkoa huo unanyemelewa na magonjwa nyemelezi kama kisukari nk.

Kufuatia hali hiyo RC Hapi amewaagiza Wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha kila Jumamosi ya pili ya kila mwezi inakuwa ni siku ya mazoezi ya Umma ambapo watumishi wote na wananchi kwa ujumla watapaswa kufanya mazoezi.

Watakaopuuza hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 kidikteta UCHWARA kingine na hili litafeli tu. Eti hatua za kisheria zitachukuliwa 🤣🤣🤣🤣🤣🤣atawafukuza kazi au kuwaweka rumande? MPUUZI kweli huyu!
 
Mpumbavu huyu dogo
 
Mazoezi ya mara moja kwa mwezi hayawezi kuepusha ugonjwa wowote.. Atakuwa anatafuta KiKi huyu.

Afu, wasiofanya atawashtaki kwa sheria ipi?!

Mi5 tena🙄
 
Kazi za msingi za serikali ni pamoja na kuwaletea maendeleo wananchi.Si upuuzi kama huo.Waletee wananchi maendeleo kwanza,mazoezi watafanya wenyewe.
 
Na hapa ndio unaona viongozi wasio na akili. Kwanza jumamosi ni Sabato takatifu kwa tunao amini hivyo.

Pili hivi mtu anashamba, jumamosi saa kumi na mbili asubuhi kawahi shambani kwake kwa kupamis siku za kazi. Hii si zaidi ya zoezi?

Wao wanafikiri watumishi wote tumebweteka kama wao. Nina kuku, mahindi, na mbogamboga nikakimbie wanjani kutafuta mini?
 
Asijisahau sana, atalazwa tena makaburini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…