Taifa lenye utawala wa kidemokrasia lina elimisha kuhusu faida za kufanya mazoezi. RC angeandaa elimu na kutafuta air time kwenye TV na Radio.
Jumamosi ni sabato ya bwana siku ya saba ya Juma,ambapo tunamuabudu Mungu ktk roho na kweli, This RC should respect faith and belief of others,God is bigger than our different careers,
Kusoma ni jambo moja na kuwa na akili nzuri ni jingine.LLB (UDSM), MBA (UDSM)....ndo wasomi wetu hao!
Hivi lile tamko la kifanya usafi kila mwezi liliishia wapi?Mkuu wa mkoa wa Iringa Salum Happi amesema jopo la madaktari wa mkoa wa Iringa wamemweleza kuwa mkoa huo unanyemelewa na magonjwa nyemelezi kama kisukari nk.
Kufuatia hali hiyo RC Happi amewaagiza Wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha kila Jumamosi ya pili ya kila mwezi inakuwa ni siku ya mazoezi ya Umma ambapo watumishi wote na wananchi kwa ujumla watapaswa kufanya mazoezi.
Watakaopuuza hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Chanzo: Channel ten
Maendeleo hayana vyama!
Dar es salaam bado linaendelea Jumamosi ya mwisho ya kila mwezi hasa pale Kariakoo maduka yanafunguliwa saa 4, inaboa sana!Hivi lile tamko la kifanya usafi kila mwezi liliishia wapi?
Je ile amri ya makamu rais ya kufanya mazoezi nayo iliishia wapi?
Aisee!! hatari sana,walimu ndio guinea pig ya wanasiasa!!Hatua za kisheria.
Sheria gani bwana wewe???
Wapeni hamasa watu wenu wafanye mazoezi ila msiwalazimishe.
Najua mtaanza kuwalazimisha walimu maana ndio guinea pig wenu wa kujaribu kila kitu.
Hivi hawa "uchwara" wanapata wapi jeuri hii"Mkuu wa Mkoa wa Iringa Salum Hapi amesema jopo la madaktari wa mkoa wa Iringa wamemweleza kuwa mkoa huo unanyemelewa na magonjwa nyemelezi kama kisukari nk.
Kufuatia hali hiyo RC Hapi amewaagiza Wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha kila Jumamosi ya pili ya kila mwezi inakuwa ni siku ya mazoezi ya Umma ambapo watumishi wote na wananchi kwa ujumla watapaswa kufanya mazoezi.
Watakaopuuza hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Chanzo: Channel ten
Maendeleo hayana vyama!