mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,126
- 5,068
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera, ameagiza watendaji wa Vijiji na Kata walioshindwa kufikia kiwango cha ukusanyaji wa mapato ya ndani kupangiwa kazi nyingine.
Homera ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani mara baada ya Uongozi wa Halmashauri kutangaza majina ya watendaji waliofanya vizuri kwenye ukusanyaji wa mapato.
Amesema kuanzia leo watendaji walioshindwa kufanya vizuri wapangiwe kazi nyingine ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato kwenye Wilaya hiyo na kujenga miradi mbalimbali ya maendeleo.
“Nimefurahishwa na ubunifu wenu wa kuwapongeza watendaji wanaofanya vizuri kwenye ukusanyaji wa mazao naomba kila wilaya iige mfano huu lakini niweke wazi kuwa kwa wote ambao hawajafanya vizuri wapangiwe kazi aidha wapelekwe kwenye vituo vingine vya kazi wakajifunze namna ya kukusanya mapato,” amesema Homera.
Aidha Homera amewataka madiwani wa Halmashauri hiyo kuendelea kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ujenzi wa vyumba vya madarasa.
Chanzo: Nipashe
Amesema kuanzia leo watendaji walioshindwa kufanya vizuri wapangiwe kazi nyingine ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato kwenye Wilaya hiyo na kujenga miradi mbalimbali ya maendeleo.
“Nimefurahishwa na ubunifu wenu wa kuwapongeza watendaji wanaofanya vizuri kwenye ukusanyaji wa mazao naomba kila wilaya iige mfano huu lakini niweke wazi kuwa kwa wote ambao hawajafanya vizuri wapangiwe kazi aidha wapelekwe kwenye vituo vingine vya kazi wakajifunze namna ya kukusanya mapato,” amesema Homera.
Aidha Homera amewataka madiwani wa Halmashauri hiyo kuendelea kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ujenzi wa vyumba vya madarasa.
Chanzo: Nipashe