RC Makalla umeyamaliza ya wamachinga, lakini vipi kuhusu Mbuzi wazururaji wa Dar?

RC Makalla umeyamaliza ya wamachinga, lakini vipi kuhusu Mbuzi wazururaji wa Dar?

Utalii huo ndg mbeya unakutana na nguruwe sema wale mbuzi watu wale mnyama anajuazje zebra
 
Na mbwa wazururaji mtaani ni hatari kwa afya za wananchi.

Mbwa wanaua tumeshuhudia watu wakipoteza maisha sababu ya kung’atwa na mbwa tena wengine hadi mbwa wao sembuse mtu bali?!
 
Machinga ameyamaliza wapi?
Pita Manzese wakati huu uone Uhalisia.
 
hao wapo karibia miji yote ya TZ.........wanazalisha mbole maeneo ya bustani
 
Hii dunia siyo yenu pekee yenu

Hata wanyama wana haki ya kuishi

Na wawepo mijini

Ova
 
Wote tumeona kwamba mkuu wa mkoa RC Makalla na serikali kwa ujumla wamewakomalia wamachinga waondoke maeneo ambayo hawatakiwi kisheria.

Hiyo sawa; lakini kuna suala hili la mbuzi wa Dar ambao wanajichunga wenyewe Magomeni, Mbagala, Mbezi, Shekilango nk ambao nao wanaleta uchafuzi wa mazingira na sintofahamu ukizingatia wanajichunga wenyewe pamoja na kuwa na uwezo wa kufuata sheria za usalama barabarani kama trafic lights, zebra nk.

Lakini, hatujawahi sikia serikali ikitoa tamko juu ya hawa jamaa na sasa wanazidi kuongezeka mjini Dar. Labda RC Makalla angetuambia kwanini na hii mifugo isifukuzwe mitaani ili ikakae maeneo yanayowahusu kama walivyofanyiwa wamachinga?
Mbona hawazibi biashara za watu, wao wanatembea kuliona jiji.
 
Na mbwa wazururaji mtaani ni hatari kwa afya za wananchi.

Mbwa wanaua tumeshuhudia watu wakipoteza maisha sababu ya kung’atwa na mbwa tena wengine hadi mbwa wao sembuse mtu bali?!
Hata binaadamu wanaua, tumeshuhudia binaadamu wakiua wapita njia bila sababu.
 
Tatizo la mbuzi wengi wa Dar, sio mbuzi kama mbuzi.

Wale ni binadamu ndio maana wanavuka barabara kwenye zebra, wanajua kufuata mataa ya kuongozea magari, wanaenda makaburini kuwaombea marehemu, wanakula nyama na mikate nk nk nk

Kama huamini siku moja jifanye kama zuzu umkamate mmoja afu umcharaze bakora. Ila usije ukasema sijakuonya
Hatari Sana.
 
Mbuzi wa pale mtongani,kwanza hawali vyakula vya hovyo hovyo,wao ni mikate,vipisi vya sigara na hadi soda wanakunywa! Mzee Kibere ndiyo mwenye Mali!
Miaka ya 98 pale kulikuwa na mzee anaitwa mzee Uliza, ndio mbuzi wake waliogopeka ila sio kivilee, huyo uliemtaja zaidi ya alikuwa mtemi,hakuwa na uchawi wowote,
 
Wote tumeona kwamba mkuu wa mkoa RC Makalla na serikali kwa ujumla wamewakomalia wamachinga waondoke maeneo ambayo hawatakiwi kisheria.

Hiyo sawa; lakini kuna suala hili la mbuzi wa Dar ambao wanajichunga wenyewe Magomeni, Mbagala, Mbezi, Shekilango nk ambao nao wanaleta uchafuzi wa mazingira na sintofahamu ukizingatia wanajichunga wenyewe pamoja na kuwa na uwezo wa kufuata sheria za usalama barabarani kama trafic lights, zebra nk.

Lakini, hatujawahi sikia serikali ikitoa tamko juu ya hawa jamaa na sasa wanazidi kuongezeka mjini Dar. Labda RC Makalla angetuambia kwanini na hii mifugo isifukuzwe mitaani ili ikakae maeneo yanayowahusu kama walivyofanyiwa wamachinga?
Mbuzi wazururaji wapo kwenye miji mingi
 
Wote tumeona kwamba mkuu wa mkoa RC Makalla na serikali kwa ujumla wamewakomalia wamachinga waondoke maeneo ambayo hawatakiwi kisheria.
Makalla ameshindwa na Wamachinga ; anamuhadaa Samia kwa kuwaondoa katikati ya jiji [cbd] na Kariakoo basi!! kwingine kulikobaki kama kawa machinga wanatamba!!

Ameshindwa kwasababu wenyeviti wa mitaa ndio wafaidika wakubwa wa biashara hizo zisizo rasmi!! Tumemsaidia hata kumtajia sehemu zinazotakiwa kusafishwa lakini anapata kigugumizi akisikia Sehemu husika ni za NYERERE!! Watu wanatumia Jina la NYERERE vibaya kwa manufaa Yao!
 
Acha Imani potofu, hakuna cha mpemba wala nini, ni ujinga tu unawasumbua wengi kuamini uchawi wakati haupo, jifunze tabia za wanadamu na viumbe wengine, halafu jifunze jinsi mfumo wa dunia unavyo fanya kazi ili uondokane na Imani potofu
Hakuna uchawi mkuu, we bebelea mbuzi mmoja wa mpemba kamchinje ule
 
Kumbuka panya walikubaliana wamfunge paka kengele shingoni ili akipita wasikie sauti wakimbie, mpaka Leo hakuna aliyemkaribia paka kumfunga kengele.
 
Hizo sio mbuzi mkuu! Mmoja juzi nimekaa bar kaja kaagiza safari kubwa ya baridi kapiga na mchemsho! Mezani kulikuwa na kipisi cha fegi kaila! Mbuzi gani kabla ya kuvuka barabara zinaangalia kushoto kulia na kwenye taa wanazingatia usalama!
images%20-%202021-11-11T095656.380.jpg
View attachment 2006660
 
Back
Top Bottom