RC Makonda aagiza Wazee na Viongozi wa Dini kutopanga foleni kwenye ofisi za Umma

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu kumekucha salama?

Huko Arusha Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda ameagiza kupewa kipaumbele kwa Viongozi wa dini na Wazee wote wa Mkoa wa Arusha pale watakapokuwa kwenye Ofisi zote za Umma Mkoani humo kwa ajili ya kutafuta huduma.

Mbele ya waumini wa Msikiti Mkuu wa Bondeni Jijini Arusha mwisho wa wiki, Ijumaa Oktoba 25, 2024, Makonda alisema: "Nawaomba viongozi wote wa Serikali hakuna kiongozi wa dini wala mzee wa Mkoa wa Arusha anayestahili kapanga foleni kwenye ofisi yoyote ya Umma anapotafuta huduma, Wazee wa miaka 60 wao wakifika wanaenda moja kwa moja kwenye ofisi, haya ni maagizo yangu"
Your browser is not able to display this video.
Soma: RC Makonda aandaa hafla ya Wakuu wa Taasisi za Umma na Wafanyabiashara Arusha
 
Being old is not being disabled, wafuate utaratibu kama wengine cheap politics mbaya sanaa.......
 
Mkiambiwa huyu jamaa yenu anapwaya mnapiga makelele
 
Hapo kwa senior Citizens sawa ila hao viongozi wa dini. Hapana kwanza hao ndiyo hata huduma wasipewe kazi unafki tu.
 
Viongozi wa dini wa level gani?! Mi Mzee wa Kanisa la waadventista wasabato nina qualify?
 
Hili jambo lipo na limekuwepo toka dahari, maana ni utamaduni wa Watanzania!
 
Je viongozi aa wapagani? Wataoanga foleni?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…