Papushikashi
JF-Expert Member
- Feb 28, 2016
- 10,963
- 13,287
nani huyu?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
nani huyu?
Huruma sana !Kuzaa ni URIJALI iwe ndani ya ndoa au nje ya NDOA........
Sasa wewe mtoto wa ndani ya ndoa huna....
Nje ya ndoa huna.......
Hata vyeti USIWE navyo...........
Wewe ni MWANAMUME au MVULANA??
=====
Msomaji, vema pia ukasoma hapa > Mwanamama kupitia Uhuru FM, adai kuzalishwa na Askofu Gwajima na kutelekezwa!
=====
Makonda hua anafika office za clouds mara kwa mara. Siku zingine anashinda hapo mpaka jioni. Siku ya Alhamis Makonda alifika office za Clouds Cha ajabu siku hiyo alikaa mpaka usiku akawa anamtafuta soudy Brown na Qwisser wa SHILAWADU muda huo walikuwa bado hawajafika kazini basi akawa anazungukazunguka tu ofisi hii anatokea ile kama mfanyakazi wa Clouds.
Kwenye Mida ya Saa kumi hivi akakutana na kina Soudy pamoja na prodyuza wa kipindi wakawa wanaongea kwa uficho hivi na usiri tukajua tu ni mambo ya kawaida ya kuhitaji uprivate lakini siku ile ulikuwa unatia mashaka sana.
Kumbe Makonda alikuja na Story ya mwanamke mmoja ambaye yeye Makonda alisema huyo mwanamke amezaa na mchungaji Gwajima na ametelekeza akawa anataka arekodiwe na ubuyu uruke kwenye kipindi cha SHILAWADU.
Basi wakakubalia kwa kuwa ni habari itabidi huyo mwanamke arekodiwe na kipindi kiruke siku ya jana lakini kawaida ya Kipindi cha SHILAWADU ubuyu ukipatikana lazima kila mtu apewe Natural Justice ya kusikilizwa pande zote mbili sababu huwa ndiyo kawaida ya kipindi.
Makonda siku hiyo hiyo ya Alhamisi akamwambia Soudy ajiandae then huyo mwanamke mnayemuona kwenye video na mtoto aliletwa na wasaidizi wa Makonda ahojiwe na Soudy Brown tayari kwa kurushwa kwa kipindi.
Siku ya Ijumaa ambayo ilikuwa ni jana SHILAWADU wakamtafuta Gwajima kwa upande wake kama anaifahamu hiyo ishu na je mwanamke huyo aliyetajwa ni kweli kwasababu tunaelewa ugomvi uliopo kati ya Makonda na Gwajima isijekuwa SHILAWADU wanatumika kuwafitinisha watu vibaya!
kwa bahati mbaya Gwajima hakupatikana jana ijumaa kwa ajili ya kurekodiwa na kufanyiwa mahojiano.
SHILAWADU wakatumia busara mpaka apatikane Gwajima scene ya Dada mwenye mtoto ziende kwa pamoja na ya mchungaji Gwajima kama kawaida ya POVU inavyokuwaga.
Jana usiku sasa kumbe Makonda alikuwa anafuatilia kipindi cha SHILAWADU aone kama kile kipande kitaruka hewani wapi ndiyo akaamua kuja Clouds na magari mawili yeye mwenyewe Makonda na Watu kama nane hivi wakiwa na Bunduki aina ya SMG geti la kawaida mlinzi alifungua geti kwasababu amezoeleka Mh anakujaga mjengoni wakafunguliwa kisha wakaingia ndani.
Walipofika reception wakazuiwa kuingia ndani sababu hatuna utaratibu wa kuruhusu wageni baada ya saa Nne usiku kuingia ndani ya Ofisi kama siyo mfanyakazi wa CLOUDS.
Alipoona wanazuiwa wakatoa bunduki zao mlinzi akashurutishwa afungue mlango kwa nguvu sababu walimtishia na Silaha mlimzi akafungua mlango wakaenda naye hadi studio kipindi kilikuwa kinaendelea hewani.
Makonda akawatoa nje Soudy na Mwenzake Qwisser akawauliza kwanini video aliyowaletea haijachezwa wakaelezea utaratibu jinsi utaratibu ulivyokuwa Qwisser wakati anajielezea akapigwa mtama akaanguka chini wakavamia mitambo ya transmission kwenye traycaster wakitaka kile kipande kirushwe hewani prodyuza wa kipindi akamuambia Makonda kwanini anavunja utaratibu na kutumia nguvu na ameshapewa utaratibu akapigwa na kitako cha Bunduki mgongoni akaanguka chini bahati mbaya kipindi kilikuwa kimefika mwisho.
Wakamshurutisha Prodyuza wa SHILAWADU anaitwa Chriss awape kile kipande wakaondoka naye wakati wanaondoka Ruge alikuja na Polisi akaingia lakini tayari walikuwa wameondoka ofisini wamechukua hicho kipande cha Video ya huyo mwanamke.
Hizo video zilichukuliwa kwa nguvu na Makonda na hao watu waliokuwa na Silaha inasemekana Makonda ana timu yake wanazisambaza kwa kasi na hatujui lengo lake ni nini.
Hata mkihitaji footage za Camera zipo jinsi tukio lilivyokuwa usiku wa jana.
====
Kutoka kwa wadau wa Clouds Media
mkata Umeme. Anaangalia tu Paul Makonda anavyozama gizaninani huyu?
Alafu inasemekana wameingia usiku lakni view ya nje inaonekana vizuri kama ni mchana vileZoom picha hiyo mbona amekaa hapo huku akitetemeka.
Inaonekana Tshirt na mkono.mmoja na suruali.
Hiyo ni black and white huwezi tofautisha mwanga wa taa na mchana ila kama una akili angalia kipindi kilichoko kwenye tv hurushwa saa ngapiAlafu inasemekana wameingia usiku lakni view ya nje inaonekana vizuri kama ni mchana vile
Hivi yule kijana wa Shilawadu naye aliitwa kwenye list ya madawa ya kulevya najaribu kuconnect tu!!!Bashite anahaingika sanaaaaa.
Hadi Huruma.
waterloo huyu qengeh ni Le Mutuz Kwa,taarifa yakoo ana,id nyingi shenzyy sana hili kubwa jingaSafari hii lazima uwe kichaa
Kwani kinakuwaga live?Hiyo ni black and white huwezi tofautisha mwanga wa taa na mchana ila kama una akili angalia kipindi kilichoko kwenye tv hurushwa saa ngapi
This is a crime
Anapaswa kufunguliwa mashtaka.
Anajiongezea jinai mbali na ile ya vyeti
Umenikumbusha na hii ishu ya scorpion! Wadau walikuwa na maswali mengi juu yake, nahisi pia kuna mchezo wa huyu Bashite jinsi alivyoishikia kidedeaBashite ni hatari,Scorpion cha mtoto ati.!
Hujioni ulivyowehuka?Kisa!?
Watu wametembezewa mkong'oto na hadhi zao,wamechungulishwa burrel,unataka kusema nini we......Eti crime kwa lipi!?
Kuingia kwenye jengo kama alivyozoea au?
Makonda oyeeeee