RC Makonda: Idadi ya maambukizi imepungua Dar, kuna watu walinunua majeneza na kupiga picha ili kuzua taharuki

RC Makonda: Idadi ya maambukizi imepungua Dar, kuna watu walinunua majeneza na kupiga picha ili kuzua taharuki

Huyu jamaa niliacha kitambo kumsikiliza baada ya kutambua kuwa hazimtoshi...so hata alichoongea leo sijui ni nini ila kwa heading tu nahisi ni upupu...
 
Cheee,.usawa huu ukanunue tuu majeneza halafu uchimbe chimbe then what???baba k haupo serious aki vile..
 
Kama anajua kizungu akayafute ile habari ya aljezira aone ilala manicipal vifo vilikuwa zaudi ya 250 vya covid alafu anasema nini
 
Huku Gwajima, kule Bashite. Watu wanapukutika bado anaaminisha wat kuna ununuzi wa majeneza

Nni tusi kubwa kwa maelfu ya wafiwa! wanaomboleza, misiba kila kona bado kuna dhihaka kama hii....
Unajuwa kama huu ugojwa auja kupata au kupata moja ya ndugu zako wa karibu unachukulia kama mzaha hivi Au unaona kuwa haukuhusu hivi kwaiyo tunaweza kuongea vyovyo inavyo jisikia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vijana waache kuzusha habari mbaya za uongo
Mabeberu hawatawasaidia
Mpumbavu kuliko huyo bashite wako! Yaani anataka kumdanganya Nani ilihali wanakozika kule kondo Kuna watu walioshuhudia maziko ya usiku Hadi waziri mkuu alithibitisha na kupiga marufuku!

Eti maambukizi yamepungua, haimaanishi hata kidogo na keshaona taharuki ya watu wanaodondoka na kufia barabarani ndio anakuja na huu upoyoyo wake wa kuwazuga watu!
Bashite na ccm mnataka wafe wananchi wangapi ndio muwe serious kupambana?
 
Hivi kwa taarifa hizi wanatarajia watalii kuja Tanzania kweli? Hivi sisi ni spesho kiasi gani hata tupendelewe kiasi hicho wakati majirani zetu wanahangaika na huu ugonjwa?

Eti sisi maambukizi yamepungua wakati ndo tunazidi kupuuzia masharti, inawezekanaje? Yaani tunakuwa kama Mbuni tunajificha kichwa wakati mwili upo nje. Watu wanatuona jamani teknolojia ya leo huwezi kuficha vitu kijinga hivi.

Mwalimu Nyerere aliwahi kusema "Ukweli haupendi kudharauliwa, ukidharauliwa unatabia ya kulipa kisasi"

Wahenga walisema mficha maradhi kifo humuumbua. Madereva 23 wa kitanzania wamekwama kuvuka Namanga baada ya kukutwa na korona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huku Gwajima, kule Bashite. Watu wanapukutika bado anaaminisha wat kuna ununuzi wa majeneza

Nni tusi kubwa kwa maelfu ya wafiwa! wanaomboleza, misiba kila kona bado kuna dhihaka kama hii

Kwamba, kuna watu wananunua majeneza kueneza uvumi. Tanzania tumefikaje hapa?

Kila siku kuna kitu cha kushangaza dunia, siku hizi ukisoma Media za duniani ni mabaya ya Tanzania

Inafika mahali tunaona aibu hata kujiita Watanzania...
Daah,jamaa umenikumbusha katibu wangu,hivi Dr. Bashiru yuko wapi nimem miss sana katibu, jamaani.
Hebu katibu sema lolote ktk kipindi hiki cha korona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ungetoa tu data, tungeelewa wenyewe Kama imepungua hama bado siyo maneno ambayo hayana muunganiko.
 
Tanzania kuna waigizaji wazuri, wananunua jeneza, Ambulance, gari la Municipal la mazishi harafu wanaenda kushoot location ya makabuli, ngoja tusubilie hii movies

Corona haitoisha Tanganyika kwa mizaha hii, tuwe serious kidogo ndo tutaitokomeza
 
Back
Top Bottom