RC Makonda: Idadi ya maambukizi imepungua Dar, kuna watu walinunua majeneza na kupiga picha ili kuzua taharuki

RC Makonda: Idadi ya maambukizi imepungua Dar, kuna watu walinunua majeneza na kupiga picha ili kuzua taharuki

Mungu wa Kipindi cha Kina Abraham, Adama na kina Mose angeendelea kuonyesha makali yake mpaka sasa hivi watu wengi wangekufa.

Huyu Paulo alikuwa anahubiri juzi jumapili kashika Bible.
Leo anaongea uongo wazi wazi wa Majeneza.. hapa DSM nani anaweza kupata ambulance au gari la mazishi.

Yani huyu Paulo angepigwa pigo moja angekufa kwa kumkebehi Mungu.

Bora aamue kuwa mwanasiasa aache kutumia mgongo wa Biblia ili aonekane kuwa ni mcha Mungu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Paul Makonda amenena yake kuhusu hali ya Corona mkoani Dar es Salaam. Akizungumza na vyombo vya habari amesema hali sasa inaelekea kuwa shwari, idadi ya wagonjwa inazidi kupungua na kuwatoa hofu wakazi wa mkoa huo.

Vile vile amesema alifanya uchunguzi na kugundua watu wenye nia ovu mtandaoni walinunua majeneza na kwenda kwenye maeneo ya makaburini na kuchimba chimba na kujifanya wanazika ili kuleta taharuki.

 
1)Unapewa habari moja usiyoweza kuithibitisha, inabidi uikubali kwa kuipa benefit of the doubt.

2) unaongezewa habari ya pili ambayo una nafasi kubwa ya kuithibitisha, Na unahisi kwa asilimia kubwa ni uongo.

Inakubudi uamini kuwa zote mbili ni za kutiliwa shaka

Aliposema mwenyewe Dar watu walikuwa wanapukutika bila shaka walipona wote na kupukutika kimaisha mara moja baada tu ya ile hotuba ya Chatto:

IMG_20200514_074852_720.jpg


Makonda: Dar hali si shwari, watu wanapukutika. Walio nje ya mkoa huu bakini huko! - JamiiForums

Itakuwa ni majibu chanya ya nyungu na ile mitishamba.

Hawa wanaopatikana huko mipakani ni wale wa mwisho mwisho kabisa tunapokwenda kumaliza kabisa huu ugonjwa.

Tusiwe na wasiwasi tuchape kazi, tuko vizuri!
 
Mmesema wenyewe na Dunia imewasikia kuwa vitendea kazi mlivyonavyo kwa kuweza kuwapima watu kama wana corona havina ubora; sasa hizo data kuwa idadi ya wagonjwa inazidi kupungua inapatikanaje? Acheni kuwafanya watanganyika kuwa mazuzu!!! Kaeni na ukola menu wa kuwaua wananchi wasio na hatia!!
upo sahihu mkuu, ila upande wa pili je hzo taarifa kua wagonjwa waliopimwa positive wameongezeka je imapatikanaje!? ujue hvi vitu haviitaji hasira na inaonekana kua kuna wazushi upande mmoja au pande zote!!. mitandao inadai vifo vinaongezeka ila tulioko mitaan dar hatusikii vifo, au wanakufa watu wa masaki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwenye macho haambiwi tazama, je aliwachukulia hatua gani baada ya kugundua hilo?
Swali zuri sn mkuu. Unajua tatizo hawa viongozi wetu kwenye akili zao wanajua wanaongoza watu wajinga ndiyo maana wanatunga upumbavu kama huu. Jambo rahisi tu wakamate wanunua majeneza ya yangefunguliwa watu waone hayana miili ndani. Hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao
 
Back
Top Bottom