RC Makonda: Yeyote anayeenda katika eneo la manunuzi lazima avae barakoa. Kwenye misongamano watu wakae umbali wa mita 2

RC Makonda: Yeyote anayeenda katika eneo la manunuzi lazima avae barakoa. Kwenye misongamano watu wakae umbali wa mita 2

Vifo na maambukizi ya Corona ni matokeo ya Serikali kushindwa.

Mwezi May watu wajiandae kuona umma unavyopukutika!

JokaKuu Pascal Mayalla tindo
Mkuu Nguruvi3 at this juncture, lets stand as one kusaidia. Je, Watanzania wenye uwezo wa kusaidia, jee tuisaidiaje serikali yetu ili ishindindwe?.

Kwa vile sasa ni April na umma haupukutiki bali unaambukizwa, na kwa vile umeishajua kuwa mwezi May umma utapukutuka, hivyo unashauri tujiandae kuona umma unavyopukutika!, kwanini usisaidie kuzuia umma wa Watanzania usipukutike?.

Usaidizi huo, sio lazima uwe kama ule wa Rostam Aziz or Mo Dewji, bali hata kwa kuandika tuu humu jf na vyombo vyetu vya maamuzi watasoma na kufanya uamuzi wafuate au waache, ili itakapofika hiyo May, tutakapo anza kuona na kushuhudia jinsi watu wanavyopukutika, angalau tutasema, tuliona kabla, tukaonya, tukashauri, tukapuuzwa na sasa haya ndio matokeo.

Kwenye situation hii tuliofikia, swali langu hili
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums

Ni valid hata kwenye janga hili la Corona.
P
 
Pascal Mayalla, Well said, tuisaidie Serikali, tusikae kusema tutashuhudia, kupukutika kwa watu, tutekeleze maagizo ya Viongozi, na tuisaidie Serikali kusimamia hayo maagizo sisi kwa sisi.

Nyoka ameingia ndani ya nyumba Lazima tusaidiane kumtoa.

Sema Kuna shida kidogo, barakoa Serikali imeacha wahujumu uchumi walangue Bei juu Sana kisa Corona. Hapa panahitaji matamko pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko hapa najaribu kubalizi mitaa ya mkoa wa Dar es Salaam na kuangalia kama agizo la mkuu wa mkoa Paul Makonda limezingatiwa la kuvaa barakoa kila anayetoka nyumbani kwake.

Wananchi wameitikia kweli kweli ,si barabarani ,kwenye daladala, sokoni watu wote wamefunga barakoa!
Hii inatuma ujumbe gani kwa Chadema?

Ikumbukwe Mara baada ya Makonda kutoa agizo hilo chadema walianzisha nyuzi mbambali humu za kupinga agizo hilo na kuwashawishi wananchi wampuuze Makonda!

Sasa wananchi badala ya kumpuuza Makonda wamewapuuza chadema na kusababisha wahahe kila kona.

Kwa hali hii ya kupuuzwa na wananchi kila wito wanaotoa chadema kwisha kwisha kabisa ndembendembe na kifo cha chadema ni cha kikatili mno, hamna chama cha siasa kingine kilichowahi kufa kikatili namna hii kwa kupuuzwa na wananchi kila kona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada yakuombeleza msiba wa kada wa CCM mwezenu aliyekufa Leo kwa ugonjwa wa..... Wewe unaleta nyuzi za umbea.
 
Niko hapa najaribu kubalizi mitaa ya mkoa wa Dares salaam na kuangalia kama agizo la mkuu wa mkoa Paul Makonda limezingatiwa la kuvaa barakoa kila anayetoka nyumbani kwake.

Wananchi wameitikia kweli kweli ,si barabarani ,kwenye daladala, sokoni watu wote wamefunga barakoa!
Hii inatuma ujumbe gani kwa Chadema?

Ikumbukwe Mara baada ya Makonda kutoa agizo hilo chadema walianzisha nyuzi mbambali humu za kupinga agizo hilo na kuwashawishi wananchi wampuuze Makonda!
Sasa wananchi badala ya kumpuuza Makonda wamewapuuza chadema na kusababisha wahahe kila kona.

Kwa hali hii ya kupuuzwa na wananchi kila wito wanaotoa chadema kwisha kwisha kabisa ndembendembe na kifo cha chadema ni cha kikatili mno, hamna chama cha siasa kingine kilichowahi kufa kikatili namna hii kwa kupuuzwa na wananchi kila kona.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna wapumbavu kati yenu mnataka kuleta siasa kwenye majanga, hivi unafahamu matokeo ya unachokiandika hapa? Unajua kwamba watu aina ya Makinda walipaswa kujiweka au kuwekwa mbali na hili swala?
Hivi unafahamu kwa maneno na matendo ya viingozi aina ya Makonda kuna wajinga kuliko ninyi wamedhamilia kujiambukiza COVID-19 ili waambukize watu wengi zaidi?

Mnadhani kwa kuandika andika kizembe tu mnamfurahisha mtu lakini hamjui madhara yake?
 
Back
Top Bottom