Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Mimi ninaona Ancelloti ndio anayezungua, huwa ni muoga sana kufanya mabadiliko., jana tulikuwa na viungo Wanne uwanjani ila jamaa walishika dimba, shida ni kuwa hao viungo wote watatu wana uchezaji unaofanana., Modric na Ceballos walivyoingia ndio game ilibadilika, niliona tunacheza mpira mzuri tu unaoeleweka.
Kama atakuja Kocha mwingine msimu ujao ni lazima afumue midfield yetu.

tatizo kuu la timu lipo kati, midfield zote ni za style moja amabazo sio rafiki kwa mazingira ya timu, Camavinga, Valverde na Belingham lazima wawili wakae nje modric na Rodrygo wachukue nafasi.
 
Alicheza

Mwanzo tulikua na viungo wanne wa sifa moja ila majukumu yao yalikua tofauti.

Kipindi cha kwanza Madrid walicheza mfumo wa 3-4-2-1.

Yaani Camavinga na Federico Valverde walisimma kati kati kama 6 na 8.

Miltao alibana kulia huku Vasquez akisogea Eneo la kiungo.

Rudiga alibana kushoto huku Garcia nae akipanda Eneo la kiungo.

Beki ya kati alisimama Aurelian Tchouameni.

Attacking midfielders walisimaa Vini na Jude.

Foward akasimama mbappe.

Lengo lilikua ni kuushika mchezo na kwa Plan hii ilikua nzuri sema haikulipa kwa sababu kuna maeneo waliwekwa watu sio sahihi.

Ndiomana Kipindi cha pili Carlo hakubadili tu wachezaji Bali na mfumo mzima wa uchezaji wa timu kwa ujumla.

Mimi sipendezwi na kuchelewa kwake kufanya mabadiliko tu wakati mapema tu timu inashikwa na Anaona kabisa mchezaji flan kapwaya ila anaacha tu.

Mfano Hii Mechi Federico Valverde alipaswa kupunzika kusubiri El classico kijana katumika sana
Valverde kuanzia game inaanza hakuwepo kabisa uwanjani, na Ancelloti ni kama amekariri kuwa Valverde ni lazima acheze., una Ceballos nje na Arda Güler unamforce vipi mtu kucheza wakati unaona kabisa amechoka., halafu ile game hata haikutaka mambo mengi, ila sasa kwa plan ya Kocha akajikuta anaufanya mchezo uwe mgumu.
Kama kwenye El classico ataenda na plan ile, tusitarajie makubwa., yaani team haikueleweka kama inashambulia ama inajilinda, kwasababu kote tulipwaya.
 
Valverde kuanzia game inaanza hakuwepo kabisa uwanjani, na Ancelloti ni kama amekariri kuwa Valverde ni lazima acheze., una Ceballos nje na Arda Güler unamforce vipi mtu kucheza wakati unaona kabisa amechoka., halafu ile game hata haikutaka mambo mengi, ila sasa kwa plan ya Kocha akajikuta anaufanya mchezo uwe mgumu.
Kama kwenye El classico ataenda na plan ile, tusitarajie makubwa., yaani team haikueleweka kama inashambulia ama inajilinda, kwasababu kote tulipwaya.
Mi nilishangaa alivyomtupa Bellingham pembeni nilichoka sana,afu kati viungo wagumu wote.kama vipi arda awe anaanza afu jude ajichange ila ndo hivo kocha ni kama ana uwoga flani ivi.
 
Leo babu ameishi humu wazee mnasemaje.
 

Attachments

  • FB_IMG_1729617985822.jpg
    FB_IMG_1729617985822.jpg
    81 KB · Views: 6
Mpangilio ni huh hapa.

Kabla ya mechi kuanza atoke nani aingie nani?
 

Attachments

  • FB_IMG_1729619230272.jpg
    FB_IMG_1729619230272.jpg
    103.5 KB · Views: 5
Usengerema huu maninaaa...yale yale ya miaka ya Lewando yanajirudia...Miltao anangalia mpira unampita mbele maninaa....hii timu tulisema ipo siku tutapata aibu ya mwaka,ngoja El clasico uone vile tutapigwa kama ngoma😡😡🤬...timu inacheza utasema haina kocha.
 
Hakuna timu hapa. Toka msimu umeanza hii timu mbovu hakuna improvement yeyote ile. Ujio wa Mbappe na kustaafu kwa Kroos kumeondoa balance ya timu. Tunatoka kapa msimu huu. Hakuna timu hapa.
 
HT: Tumecheza hovyo,timu utasema haijafanya mazoezi ya pamoja,kila eneo kila mtu anacheza kivyake,watu wanajipigoa cross mradi tu mpira utoke mguuni,tumeshindwa kupangua kabisa ngome za hawa jamaa kwa sababu tunacheza kibinafsi mnooo..
Hili suala lipo tokea tuanza msimu na sioni Ancelloti alibadilisha hii hali., kwasababu ni muoga wa mabadiliko, team ina shida ya kutengeneza nafasi kwa washambuliaji, viungo wanaocheza huo uwezo hawana., kwasababu Valverde hana hizo skills, Bellingham nae ni mfungaji mzuri ila hana mipango., Modric anaweza ila umri umemtupa mkono, ila ana option ya kumchezesha Arda Güler, huo uwezo anao ila sasa Mzee Ancelloti anaogopa kujaribu kitu kipya.,

Anaweza kuanza na Camavinga, ubavu mmoja akampa Modric/Valverde/Ceballos na Mwingine Bellingham., juu ya hao akampa Arda kazi moja tu ya kutengeneza mipango kisha kule mbele aamue kuanza na Vinicius na Mbappe ama Rodrygo, wawili hapo.
Kwenye beki hatuna option zaidi ya wale wawili, ama ampe nafasi Tchouamen acheze na Rudiger., kwasababu Militão bado akili haijakaa sawa.,
 
Hili suala lipo tokea tuanza msimu na sioni Ancelloti alibadilisha hii hali., kwasababu ni muoga wa mabadiliko, team ina shida ya kutengeneza nafasi kwa washambuliaji, viungo wanaocheza huo uwezo hawana., kwasababu Valverde hana hizo skills, Bellingham nae ni mfungaji mzuri ila hana mipango., Modric anaweza ila umri umemtupa mkono, ila ana option ya kumchezesha Arda Güler, huo uwezo anao ila sasa Mzee Ancelloti anaogopa kujaribu kitu kipya.,

Anaweza kuanza na Camavinga, ubavu mmoja akampa Modric/Valverde/Ceballos na Mwingine Bellingham., juu ya hao akampa Arda kazi moja tu ya kutengeneza mipango kisha kule mbele aamue kuanza na Vinicius na Mbappe ama Rodrygo, wawili hapo.
Kwenye beki hatuna option zaidi ya wale wawili, ama ampe nafasi Tchouamen acheze na Rudiger., kwasababu Militão bado akili haijakaa sawa.,

Timu haina creative players kama walivyokuwa Kroos na Modric. Hawa kina Tchou, Camavinga na Jude ni nguvu nyingi creativity hawana. Hiyo ni changamoto itatusumbua msimu wote. Defense tuombe Alaba arudi ASAP ana utulivu wa kutosha. Mbappe is not up to speed yet.
 
Back
Top Bottom