Refa mwingine tena atiwa hatiani na kamati ya Ligi kwa kuipendelea Yanga, afungiwa kuchezesha soka

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Huu ni mfululizo wa maamuzi yenye dosari ya kuipendelea Yanga unaofanywa na marefa katika ligi yetu,

Kamati ya ligi naona umeamua kutokucheka na kima, ili kuokoa ligi yetu kumezwa na rushwa kutoka kwa wawekezaji wahuni wanaotumia njaa za marefa na wachezaji wa timu ndogo

 
Bodi ilishatoa taarifa rasmi ya maamuzi ya mechi Hio kwa kumfungia aucho mechi tatu na faini ya laki 5, mbona hawakuweka adhabu ya refa kwenye official statement Yao ambayo walitoa hukumu kwenye mechi zaidi ya 7 hivi


Tatizo bongo ni ngumu sana kuamini hivi vyanzo vya habari uchwara.... Mtu anaweza kutoka kupiga zake nyeto akaanza ku tweet upuuzi tu
 
Uliangalia hio mechi au ulisikiliza TBC taifa?
 
Karudie kusoma hukumu hiyo kuna sehemu uliruka
 
Wapi ilipoandikwa kwa kuipendelea Yanga kwenye hiyo taarifa? Una ushabiki uliopitiliza na kuichukia Yanga kupita kiasi. Vipi waamuzi waliochezeshs kwenye kipigo chenu cha paka mwizi wamechukuliwa hatua gani? Au hawakuipendelea Yanga?
 
Yanga labda alipendelewa nini kwenye hiyo mechi ungesema kabisa. Kosa alilofanya Aucho ndiyo hilohilo alifanya Ajibu, ajabu na kweli kafungiwa mmoja na mwingine anadunda.
 
Wapi ilipoandikwa kwa kuipendelea Yanga kwenye hiyo taarifa? Una ushabiki uliopitiliza na kuichukia Yanga kupita kiasi. Vipi waamuzi waliochezeshs kwenye kipigo chenu cha paka mwizi wamechukuliwa hatua gani? Au hawakuipendelea Yanga?
Refa amefungiwa kwa kutoa maamuzi ambayo yalikuwa yanaipa unafuu Yanga
 
Kama uliangalia vizuri hiyo mechi aliyependelewa zaidi na refa ni Costal, Ajibu alimchezea rafu ya makusudi Aucho lakini hakuadhibiwa uwanjani wala bodi ya ligi haijamuadhibu pia, yule mchezaji Semfuko sijui alikuwa anacheza rafu za makusudi hata alimpiga ngumi Musonda akapewa kadi ya njano bodi ya ligi wameifuta kadi hiyo kwa maelezo kuwa sio yeye aliestahili kupewa kadi, ni nani alistahili tuwaulize bodi ya ligi.
Kwa kifupi ile mechi refa ilimshinda kabisa na sio kwamba aliipendelea yanga
 
Karia anatamani hata kuifuta kabisa yanga sema ndio hana uwezo huo aliikuta na ataiacha
 
Nilivyoona siku hiyo huyu mwamuzi aliikamia sana coastal hadi akatawaliwa na hisia kiasi cha kujaribu kuwatisha wachezaji wa coastal kwa kadi.Na kama coastal wangetangulia kufunga goli,wangepigwa kadi nyekundu hata mbili ili yanga wasawazishe

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…